Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Upendo Furaha Peneza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. UPENDO F. PENEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi hii, na naomba pia niweze kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipatia tena fursa nyingine na kuweza kuzungumza ndani ya Bunge hili Tukufu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na kusoma ripoti ya committee maalum iliyoundwa na Rais nimepata kutambua ya kwamba yawezekana kama nchi na katika vipindi vilivyopita na leo hii katika juhudi zinazofanywa na Rais wa sasa za kutafuta mapato mbalimbali lakini Serikali kwa vipindi vilivyopita ilishiriki kikamilifu kusababisha ukwepaji wa mapato ndani ya Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kusema kauli hiyo ukiangalia katika mikataba ambayo iliingiwa na nchi hii, katika mkataba wa Bulyanhulu ambao uliingiwa mwaka 1994 kutokana na ripoti maalum ya committee ya Rais inaonesha ya kwamba suala la fuel levy ama mapato au misamaha ya kodi inayotokana na mafuta yanayotumiwa mgodini ilipitishwa kama government notice mwaka 1999. Lakini mgodi huu ulipata mkataba mwaka 1994 ambapo Bulyanhulu ni sehemu ya migodi ambayo inapokea misamaha ya kodi kwenye mafuta. Mwaka 2014 Bunge hili hili tukufu lilitunga sheria na kuilinda mikataba ile ambayo imepita kwamba watu hawa hawafai kuguswa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nitoe ushauri kwa Serikali kwamba tusifike hatua tukasema tufunike kikombe tuendelee na mambo mengine, lakini kuna haja ya kupitia pale tulipotoka tuweze kuona kwamba kama kuna mapato mengine tunaweza tukayapata na tusifunike tu kwamba mikataba tulishaifanya basi, sehemu maalum ziangaliwe kuangaliwa ili kuweza kuongeza mapato ndani ya Taifa letu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kuna suala la service levy, mapato yanayolipwa na migodi ambayo ni asilimia 0.3 ya turn over ya migodi hiyo. Kwa miaka iliyopita Serikali iliweka fixed cost kitu ambacho ni tofauti kabisa na Sheria ya Serikali ya Mitaa ya mwaka 1982. Wakaweka fixed cost ya dola za Kimarekani 2,000 ambazo ndizo zinazofaa zilipwe katika Halmashauri zetu. Lakini mwaka 2014 yalifanyika mabadiliko na sasa service levy inalipwa kwa 0.3, ile ile ya turn over. Sasa naitaka Serikali iweze kusimamia na kuhakikisha kwamba inazisaidia Halmashauri hizi ili kuweza kutambua ni kiasi gani ambacho ni turn over wanayostahili kama Halmashauri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua Halmashuri zetu hazina uwezo mkubwa kwa hiyo Serikali iweze kulifanya hilo na kuweza kusaidia. Lakini vilevile tuna TMA na wao wahusike kuangalia, isiishie tu udhibiti kwa maana ya madini lakini waangalie katika eneo kubwa la kuangalia kiasi gani ambacho Halmashauri zetu zinastahili ili kuleta maendeleo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kwa Wizara zingine hasa ile inayohusiana na Mambo ya Serikali za Mitaa ni muhimu pia wakatambua ya kwamba dhahabu au madini yoyote yale hayatarudi tena kuwepo kwenye ardhi. Kwa hiyo, ni vyema basi tukaweza kuzishauri Halmashauri zetu, tukashiriki kikamilifu ili walau kiasi kinachotolewa kwa ajili ya service levy kitumike kwa ajili ya kuendeleza Halmashauri, kuweka mikakati au uwekezaji mkubwa ndani ya Halmashauri zetu lakini pia kuendeleza huduma za kimaendeleo badala ya hizo hela kutumika kwenye OC ili Serikali nayo ipange mambo mengine lakini pesa zitumike kwa shuguli za maendeleo zilizokusudiwa kwa ajili ya wananchi wa eneo husika. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi natoka Geita na katika maeneo ambayo yanapata shida kubwa sana kutokana na uwekezaji wa kampuni ya Geita Gold Mine, ni wananchi wa Geita. Wananchi hawa katika maeneo ya Katoma, Nyamalembo na Compound. Wananchi hawa wamekuwa wakiathirika na mitetemo, vumbi inayotoka migodini. Vilevile nyumba zao zimekuwa zikiathirika kwa nyufa. Mheshimiwa Naibu Waziri aliweza kuwatembelea wananchi hao na akagundua kasoro ambazo zipo na akaona matatizo ya kuchafuka kwa maji kwa maeneo ambayo wananchi wanaishi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini cha kusikitisha, Mheshimiwa Naibu Waziri alitoa agizo kuwa mgodi kwanza kuziba mtaro ili maji yasiende kwenye visima vya maji, lakini pia kuhakikisha ya kwamba wananchi hawaendelei kunyanyasika katika eneo lao. Lakini nikutaarifu kwamba ni kitu cha kushangaza, mgodi huu una kiburi cha ajabu yaani hata agizo la Serikali hawakuweza kulitimiza na mpaka leo hii hicho hakijafanywa na badala yake Serikali inaangalia namna mbadala ya kuongea nao, badala ya kusaidia maisha ya wananchi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia kuna kesi mbalimbali ambazo zimejitokeza Geita, Mheshimiwa Waziri unafahamu kuna wananchi wa Maili Mpya katika eneo lile. Wananchi ambao walifukuzwa kwa kudhalilishwa, maeneo yao yakafukiwa, mgodi umechukua hilo eneo, lakini bado kuna wananchi wa Katoma ambao wengine hawakulipwa fidia hata kidogo, wamefukuzwa katika maeneo yao. Sasa haiwezekani kwamba tuna Serikali; kuna kipindi niliendelea kuitembelea nchi ya Norway katika mafunzo wakatuambia kwamba wafanyakazi walivyokuwa wananyanyaswa walifananisha manyanyaso yao na wafanyakazi wa Kiafrika wanaonyanyaswa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini leo tunanyanyaswa sisi ndani ya nchi yetu na wawekezaji hawa hawa bila kuzingatia haki za binadamu na uhuru wetu na afya zetu ndani ya Taifa letu. Kwa hiyo, ninaiomba sasa Serikali iweze kuangalia ni namna gani mtawasaidia wananchi wa Geita. Kutakuwa hakuna maana kwa wao kumpigia Rais Magufuli kura nyingi na kwa imani kubwa waliyonayo tena Rais kutoka nyumbani, halafu wakabaki na manyanyaso makubwa yanayofanywa na mgodi wa Geita Gold Mine. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile Mtaa wa Nyakabale ni eneo ambalo liko ndani ya beacon ya mgodi. Eneo hilo wananchi wa Nyakabale kama unavyofahamu limefungiwa hata nyia yake. Wananchi hawawezi kutumia njia maalum waliokuwa wanatumia zamani kuelekea mjini, badala yake mgodi umeweka mabasi asubuhi na jioni, mgodi ume-limit movement ya wananchi katika eneo husika. Pia limechimbwa shimo la takataka ndani ya eneo lao ambapo sumu za mgodi zinamwagwa ndani ya Nyakabale katika Kata ya Mgusu. Hii inaathiri afya za wananchi wa Geita, zinaathiri afya za wananchi wa Nyakabale. Ninaomba Serikali mfuatilie hilo ili hali iweze kukomeshwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mwisho ni suala la wachimbaji wadogowadogo. Katika kipindi kilichopita Serikali iliwahamisha wananchi wa Samina na kusema kwamba inawapatia eneo lingine la uchimbaji. Kwa masikitiko makubwa sana Serikali ilitoa eneo ambalo halijapimwa na ilitoa pia sehemu ambayo utafutaji wa madini kwenda chini uko mbali sana. Sasa Serikali yetu hii naiomba inavyotoa maeneo ya madini yaliyo karibu kwa wawekezaji wawafikirie wazawa Watanzania ili waweze kufanya shughuli za uzalishaji.
ushirikishwaji katika maeneo ya uchimbaji wadogo wadogo. Kwa sababu wanawake wanapiga mawe, wanawake wanafanya shughuli za kwenye makarasha, wanawake wanafanya shughuli mbalimbali katika maeneo ya migodi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba pia Wizara iweze kuliangalia hilo katika hizo ruzuku wanawake wa Geita pia ziweze kuwafikia na ziweze kuwasaidia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia wananchi wa Nyarubuso, ni wananchi wanao athirika kutokana na shughuli za ellusion ama uchenjuaji wa dhahabu. Serikali naomba itoe elimu nzuri kwa wananchi wa Geita, kwamba pamoja na uchenjuaji huo lakini waweze kufanya shughuli ya makusudi ya kwamba uchenjuaji usiathiri vyanzo vya maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mwisho ninaiomba Serikali itoe kauli humu ndani, Ilitoa ahadi kwa wananchi wa Geita kuwapatia magwangala ama mabaki ya dhahabu, lakini tunafahamu Serikali haijafanya uchunguzi kujua ni kiasi gani watapata dhahabu katika magwangala hayo. Ninaomba Serikali itoe kauli ili mchanga huo basi wananchi kwa sababu wamekosa maeneo ya kuchimbia, sasa wanatafuta mabaki ya mchanga wa dhahabu kutoka katika kampuni ya Geita Gold Mine. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itoe kauli ili kauli iliyotangazwa na Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu tuweze kuelewa ina faida ama haina faida na lini itatekelezwa kwa wananchi wa Geita ili walao kama hamjawapatia maeneo walau wapatieni huo mchanga ili waweze kujifanyia shughuli zao za maendeleo, ahsanteni sana.