Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Agnes Mathew Marwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. AGNESS M. MARWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Kipekee zaidi naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri Muhongo kwa kazi kubwa anayoifanya. Kwa kweli Mheshimiwa Muhongo unastahili sifa na nafasi hiyo ulistahili hasa ndiyo maana umerudishwa tena pamoja na majungu yote yaliyotokea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niendelee pia kuishukuru au kupongeza Wizara ya Nishati na Madini kwa kazi kubwa wanayomsaidia Waziri Muhongo pamoja na Naibu wake kwa sababu kumekuwa kuna mgogoro wa muda mrefu sana kati ya wananchi wa Tarime kule mgodini na wawekezaji wa Mgodi wa Acacia. Lakini Mheshimiwa Waziri amekuwa ni chachu kubwa ya kuonyesha yeye anasababisha ule mgogoro unafikia mahali anaumaliza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa maana hiyo basi Mheshimiwa Waziri kwa juhudi zake nilizoziona au wananchi walizoziona Mheshimiwa Waziri alituma watu waende wakaangalie matatizo ya wananchi, Mheshimiwa Waziri alimteua akiwemo Mbunge wa kule kule mgodini kaka yangu Heche na yeye pia alikuwa kati ya watu walioenda kule kuangalia matatizo ya wananchi, kwa hiyo nafikiri mambo yatakuwa mazuri tu nikupongeze sana Mheshimiwa Waziri endelea hivyo hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaona hapa kwenye mkataba wa Mgodi wa Acacia. Mgodi wa Acacia ulikuwa na leseni ya utafutaji wa madini ndani ya Halmashauri ya Tarime katika Kata ya Turwa na Kinyamanyori. Kwakuwa leseni hiyo muda wake ulishakwisha naiomba Serikali ikabidhi maeneo yale kwa wananchi ili waendelee na uchimbaji mdogo mdogo. Na Serikali kwa mpango wake endelevu iliyonao mzuri wa kuwasaidia hao wachimbaji wadogo wadogo, wachimbaji hao watakaporudishiwa eneo hilo iwasaidie mashine za kisasa kama ilivyo kwa maeneo mengine ili uchimbaji wao uwe na tija na uwanufaishe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuombe Mheshimiwa Waziri, pamoja na juhudi zake kubwa sana za kuanzisha mradi wa REA ambao umewasaidia ndugu zetu wengi sana Vijijini ikiwemo Mkoa wa Mara; Mheshimiwa Waziri nikuombe kuna baadhi ya vijiji mkoani Mara ambavyo vimebaki; kwa mfano Wilayani Rorya kuna vijiji vya Kemwame, Kibui, Mkengwa na Baraki Tarafa ya Suba vimekwama baada ya kuwa vimewekewa nguzo toka mwaka 2015 na kinachoendelea wananchi wale hawakijui mpaka sasa hivi wamebaki kwenye sintofahamu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuombe Mheshimiwa Waziri atakapofunga hoja yake anipe majibu juu ya suala hili la umeme, ni lini wananchi wa Wilaya ya Rorya wataupata umeme? Lakini pia anipe majibu ya kuwarudishia wachimbaji wadogo wadogo wa Tarime eneo lao ili nao waifadike nalo? Kwa sababu kuna wachimbaji wengi wadogo wadogo kule ambao wanaitwa tu wachimbaji wadogo wadogo lakini hawana maeneo ya kuchimba kwa sababu yale maeneo ni ya watu, watu ndio wameyamiliki. Kwa hiyo, nikuombe kipekee zaidi unishughulikie sana suala, hili usiliache.
Mheshimiwa Mwenyekiti na ndugu zangu wapendwa, Wabunge wenzangu; mwisho naomba kumalizia kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna watu ambao wameniwekea wimbo kwenye simu yangu unasema CHADEMA, CHADEMA peoples power nina imani kabisa ni wale majirani zangu. Lakini watani wangu naomba niwaambie mimi ni nyara ya CCM, kwa hiyo huo wimbo hautafanya chochote. Tunapoingia humu ndani Bungeni bangi tuweke pembeni na kazi tuweke pembeni.
Kwa hiyo, ndugu zangu niwaambie hamtanikatisha tamaa, CCM ina vijana, ina wazee ina watoto ina kila mtu na CCM ni ile ile mwaka 2020 mtaisoma namba. Ahsante mimi ndiye Agness kutoka Mkoa wa Mara, nyara ya CCM ahsanteni.