Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Vedasto Edgar Ngombale Mwiru

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. VEDASTO E. NGOMBALE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi, lakini nachukua nafasi hii pia kuwashukuru Wajumbe wa Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kwa kunichagua kuwa Mwenyekiti wao. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na uzalishaji wa umeme katika kinu cha Somangafungu. Uzalishaji wa umeme katika mtambo huu kwa kweli umekuwa wa kusuasua, umeme unaozalishwa pale unatumika katika Wilaya ya Kilwa na Wilaya ya Rufiji lakini mpaka sasa umeme umekuwa ni wa kukatika katika kila mara. Tulifanya mazungumzo na Mkurugenzi wa TANESCO alikuja pale akatuambia kwamba tayari vipuli vimepatikana kwa ajili ya kufanya marekebisho ya mitambo pale, lakini mpaka sasa hakuna kinachoendelea alituambia baada ya mwezi mmoja mambo yatatengamaa lakini bado umeme unakatikatika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, niongelee kuhusiana na suala zima la umeme vijiji. Katika jimbo langu kuna baadhi ya kata na vijiji havijapata umeme kwa mfano kata ya Miteja - kijiji cha Kikotama, kata ya Mingumbi - kijiji cha Nambondo, kijiji cha Chapita, kijiji cha Nampunga, kata ya Namayuni - kijiji cha Nahama, Namakolo, Naliyomanga, kata ya Chumo - kijiji cha Hongwe, Ingirito na Kinywanyu, kata ya Kipatimo - kijiji cha Mtondowa Kimwaga, Nandete, Pondo, Mkarango bado havijapata umeme, kata ya Kibata kata yote kijiji cha Kibata, Hanga, Nakindu, Mwengehi, Namtende vyote havijapata umeme. Kata ya Kandawale - kijiji cha Kandawale, Ngarambi, Namatewa Natipo havijapata umeme. Kata ya Njinjo - kijiji cha Msitu wa Simba, Kipindimbi havijapata umeme, kata ya Miguruwe - kijiji cha Mtepela na Kingombe na Zinga Kibaoni havijapata umeme.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia katika kata ya Kinjumbi kuna vijiji vya Pungutini, Kitope havijapata umeme. Lakini pia katika Jimbo la Kilwa Kusini kwa Mheshimiwa Bwege kuna kata saba yenye vijiji 31 havijapata umeme, kata ya Pande, kata ya Limalyao, kata ya Nanjilinji, kata ya Likawage, kata ya Mandawa, kata ya Kilanjehanje na kata ya Kitole.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna tatizo pia la kuunganishiwa umeme katika vijiji ambavyo tayari vimeshapata umeme. Watu wa REA bado wanasumbua, vijiji vimepata umeme lakini kuunganisha umeme majumbani inachukua muda wakati mwingine ni zaidi ya miezi sita toka mwananchi alipie umeme, umeme anakuwa bado hajaunganishiwa. Kwa hiyo, naomba pia Mheshimiwa Waziri hilo pia uliangalie.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni kuwa jana kupitia vyombo vya habari tuliona Mheshimiwa Rais akizungumza na Mabalozi lakini pia alizungumza na Katibu wa SADC akieleza nia ya Serikali ya kujenga kiwanda cha mbolea pale Kilwa Masoko.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua nafasi hii kumpongeza, kukupongeza wewe Mheshimiwa Waziri,nimefurahi sana katika hilo na hata kwenye hotuba yako ukurasa wa 37 umeeleza kwamba zimetengwa pesa shilingi bilioni 4.41 kwa ajili ya utengenezaji wa kiwanda hicho, tunashukuru sana. Lakini naomba pia suala hilo liendane sambamba na upanuzi wa…
MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa, muda wako umekwisha…
MHE. VEDASTO E. NGOMBALE: Ahsante!