Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Ikiwa ni mara yangu ya kwanza kuchangia, siyo tu katika Bunge hili la Kumi na Moja, lakini katika Bunge kwa ujumla wake. Nipende kuchukua nafasi hii kwanza kumshukuru Mungu kwa uzima na afya zetu wote humu ndani maana uzima na zetu zinatoka kwake. Pia nipende kuwashukuru wananchi wa Jimbo la Mafinga Mjini na niwahakikishie kwamba, nitakuwa mtumishi wao bila kujali itikadi zao, nitawatumikia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kwa kuwa sikupata fursa kuchangia katika Hotuba ya Mheshimiwa Rais nipende pia kumshukuru na kumpongeza na pia kuwapongeza Mawaziri na Serikali kwa ujumla kwa jinsi ambavyo wameanza kazi kwa kasi inayotia moyo wananchi. Nafahamu kutakuwepo na kukatishwa tamaa kwingi lakini niwatie moyo, tusonge mbele, katika lolote jema unalolifanya mtu lazima hapakosekani mtu wa kukukatisha tamaa. Sisi tuchape kazi tuwatumikie Watanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema maneno hayo ya utangulizi na mimi nijikite katika suala zima la Mapendekezo ya Mpango. Kwanza kabisa nikubaliane na nimuunge mkono Profesa Muhongo kwa sababu bila nishati ya umeme hata hii ndoto ya viwanda hatutaweza kuifanikisha. Pia nimuombe Profesa, kwa ujuzi na utaalam wake twende mbele zaidi kwa sababu kwa kuwa na gesi haitoshi tu kuwa na umeme, kama ulivyokuwa umesema megawatt 10,000 kwa malengo, sawa itatusaidia, lakini hebu kwa kutumia utaalam wako na wataalam mbalimbali wa masuala ya jiolojia tu-extend namna gani tutanufaika na gesi. Kwa mfano, kitaalam gesi ni kitu ambacho kinahitajika sana duniani. Tunaweza kusafirisha gesi siyo kwa kujenga bomba lakini kwa kufanya liquidfaction na tuka-export gesi kwa nchi jiraji kama vile China na India ambazo kutokana na geographical location yetu tunaweza kusafirisha gesi kwa kutumia meli kubwa.
Kwa hiyo, nikuombe Profesa kwa utalaam wako tu-extend ili kusudi gesi hii, tunapokwenda katika uchumi wa kati tuweze kunufaika zaidi kama ambavyo nchi kama Russia zinavyoweza kunufaika na gesi, siyo kwa kutumia tu katika kuzalisha ndani lakini pia kwa kuza nje.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pilli, nipende kuzungumzia sekta ya utalii. Hata katika taarifa ya utekelezaji wa Mpango ambao umepita Sekta ya Utalii imethibitika kwamba ilikua kwa kasi na mchango wake katika pato la taifa ulikuwa ni mkubwa sana. Niombe tu, katika mpango kwa kuwa hii ni sekta ambayo ilionesha wazi imekua kwa kasi hebu tuendelee kuipa nguvu. Pia tutanue wigo wake. Tunaweza kutanua sekta ya utalii kwa kuitangaza kupitia michezo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wenzetu nchi jirani wanatangaza sana utalii kupitia michezo hasa mchezo wa riadha. Hebu tujaribu pia kuona namna gani tunaweza kuwekeza. Nafahamu geographically, kama ambavyo nchi jirani kuna wanariadha wanatoka maeneo fulani fulani, na sisi pia tuna maeneo hayo ambayo tungeweza kutengeneza wanariadha wa kutosha ambao wangetumika siyo tu kwa kuongeza kipato lakini pia kuitangaza nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimemwona Mheshimiwa Massay juzi alikuwepo kwenye riadha pale kutoka huko Hanang Mbulu. Tunaweza kutenganeza wanariadha wazuri ikawa siyo tu source of income kwa nchi lakini kwa kuitangaza nchi. Kupitia michezo tumeona tumeona mchezaji Mbwana Samata pamoja na kuwa baadhi ya vyombo vya habari vilipotosha na kuonyesha kama anatoka DRC au anatoka Botswana na kadhalika, lakini ni sehemu ambayo inatosha kabisa kutangaza utalii na hivyo kukuza utalii na mwishowe kukuza pato la Taifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia, nizungumzie suala la miundombinu. Ni kweli kabisa naona Waheshimiwa Wabunge wengi wakisimama wanazungumza kuhusu reli ya kati ni vizuri, lakini pia tusiisahau reli ya TAZARA. Sisi watu tunaotoka Nyanda za Juu Kusini tunalima vizuri mazao ya nafaka. Reli hii ingeweza kutosha kabisa kusafirisha siyo tu mazao ya chakula kama mpunga na mahindi, lakini hata mazao mengine ya biashara na hasa zao la mbao kutoka huko Nyanda za Juu Kusini. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia katika suala zima la miundombinu, nashauri Mpango pia ujaribu kuelekeza au kutazama miundombinu kuelekea maeneo ambayo tayari ni ya uzalishaji. Kwa mfano, sisi katika Wilaya ya Mufindi barabara ya kutoka kiwanda cha Mgololo unakutana na semi-trailers kila siku, ni uchumi mkubwa kama tutaijenga barabara hii kwa kiwango cha lami maana yake ni kwamba tuta- stimulate uchumi wa watu wa maeneo ya jirani na mikoa ya jirani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wachangiaji wengi wakisimama, na hata mpango unaeleza ambavyo sekta binafsi ni engine ya ukuaji wa uchumi. Pia, hebu tujaribu kujiuliza hii sekta binafsi inafanya kazi na nani? Nakubaliana nanyi kwamba ni engine ya uchumi; lakini engine ambayo huweki oil kwa wakati, engine ambayo huweki maji kwa wakati bila shaka ita-nock. Sasa maji na oil ni Utalii imethibitika kwamba ilikua kwa kasi na mchango wake katika pato la taifa ulikuwa ni mkubwa sana. Niombe tu, katika mpango kwa kuwa hii ni sekta ambayo ilionesha wazi imekua kwa kasi hebu tuendelee kuipa nguvu. Pia tutanue wigo wake. Tunaweza kutanua sekta ya utalii kwa kuitangaza kupitia michezo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wenzetu nchi jirani wanatangaza sana utalii kupitia michezo hasa mchezo wa riadha. Hebu tujaribu pia kuona namna gani tunaweza kuwekeza. Nafahamu geographically, kama ambavyo nchi jirani kuna wanariadha wanatoka maeneo fulani fulani, na sisi pia tuna maeneo hayo ambayo tungeweza kutengeneza wanariadha wa kutosha ambao wangetumika siyo tu kwa kuongeza kipato lakini pia kuitangaza nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimemwona Mheshimiwa Massay juzi alikuwepo kwenye riadha pale kutoka huko Hanang Mbulu. Tunaweza kutenganeza wanariadha wazuri ikawa siyo tu source of income kwa nchi lakini kwa kuitangaza nchi. Kupitia michezo tumeona tumeona mchezaji Mbwana Samata pamoja na kuwa baadhi ya vyombo vya habari vilipotosha na kuonyesha kama anatoka DRC au anatoka Botswana na kadhalika, lakini ni sehemu ambayo inatosha kabisa kutangaza utalii na hivyo kukuza utalii na mwishowe kukuza pato la Taifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia, nizungumzie suala la miundombinu. Ni kweli kabisa naona Waheshimiwa Wabunge wengi wakisimama wanazungumza kuhusu reli ya kati ni vizuri, lakini pia tusiisahau reli ya TAZARA. Sisi watu tunaotoka Nyanda za Juu Kusini tunalima vizuri mazao ya nafaka. Reli hii ingeweza kutosha kabisa kusafirisha siyo tu mazao ya chakula kama mpunga na mahindi, lakini hata mazao mengine ya biashara na hasa zao la mbao kutoka huko Nyanda za Juu Kusini. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia katika suala zima la miundombinu, nashauri Mpango pia ujaribu kuelekeza au kutazama miundombinu kuelekea maeneo ambayo tayari ni ya uzalishaji. Kwa mfano, sisi katika Wilaya ya Mufindi barabara ya kutoka kiwanda cha Mgololo unakutana na semi-trailers kila siku, ni uchumi mkubwa kama tutaijenga barabara hii kwa kiwango cha lami maana yake ni kwamba tuta- stimulate uchumi wa watu wa maeneo ya jirani na mikoa ya jirani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wachangiaji wengi wakisimama, na hata mpango unaeleza ambavyo sekta binafsi ni engine ya ukuaji wa uchumi. Pia, hebu tujaribu kujiuliza hii sekta binafsi inafanya kazi na nani? Nakubaliana nanyi kwamba ni engine ya uchumi; lakini engine ambayo huweki oil kwa wakati, engine ambayo huweki maji kwa wakati bila shaka ita-nock. Sasa maji na oil ni nani? Maji na oil ni Watumishi wa Umma wa nchi hii. Mimi ni-declare interest nilikuwa Mtumishi wa Umma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa Mpango pia ujielekeze kwa Watumishi wa Umma, uwatazame katika maslahi yao, kuanzia mishahara yao, wakati wanapokwenda likizo; utakuta kwamba mwaka huu watapewa nauli mwaka mwingine hapewi nauli, lakini pia hata nauli ya kwenda kazini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nafahamu kwa Dar es salaam kuna Wizara zina gari za kuwapeleka wafanyakazi kazini na kuwarudisha, lakini kuna maeneo mengine mfanyakazi kwa mfano anatoka Kongowe anafanya kazi katikati ya mji, je, tunategemea mfanyakazi huyu atakuwa na moyo wa kuchapa kazi ipasavyo wakati maslahi yake uki-compare na hao wa private sector yako chini kwa kiwango cha kupindukia?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo mimi nishauri; katika mpango hebu tutazame pia Watumishi wa Umma kwa sababu kama tunasema private sector ni engine, basi wao tuwachukulie kama vile ni oil. Ndiyo maana katika ofisi za umma survival ya watu wengi ni kusubiri safari za kikazi kwa sababu ule mshahara hautoshelezi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, nimalizie kwa kusema kwamba, kama ambavyo Profesa Muhongo amesema watahakikisha wanamalizia vipoto vya REA awamu ya kwanza na ya pili. Nashauri kabla ya kutekeleza Mpango unaokuja hebu tukamilishe viporo, kama kuna viporo vya zahanati, kama kuna viporo vya miradi mbalimbali tuvikamilishe, hiyo itatupa nafasi ya kuweza kusonga mbele na kutekeleza ipasavyo mpango unaokuja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie pia kwa kusema, katika kumalizia viporo hivyo niombe hasa katika sekta ya afya. Hebu tuangalie maeneno kulingana na population na namna ambavyo tunahudumia. Naomba kuunga mkono mapendekezo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)