Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Godbless Jonathan Lema

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arusha Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. GODBLESS J. LEMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Naomba kabisa nianze bila kusahau na suala ambalo tulikutananalo Arusha na Mheshimiwa Waziri naomba anisikilize sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tulikwenda Arusha na Kamati ya Viwanda na Biashara na tulivyofika TANELEC, mahali ambako tunatengeneza transformer, walikuwa na malalamiko ya msingi sana. TANESCO ni shareholder wa TANELEC, yaani kwenye Board ya Directors ya TANELEC, Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO ni mjumbe. Cha kushangaza sana ni kwamba, Kenya wananunua transfoma Tanzania, Msumbiji wananunua transfoma Tanzania, mpaka Malawi, lakini Tanzania ambao ndiyo wanaotengeneza transformer na TANESCO ambao ndiyo inafanya biashara ya umeme, inanunua transfoma kwa Manji, kutoka India kwa bei mara mbili ya zinazouzwa TANELEC!
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri, haya mambo ni mambo ya ajabu kweli, kwamba partner, mwenzi wa TANELEC ambaye ni TANESCO kwenye Board anaingia Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO, wanakwenda kufanya maamuzi ya manunuzi ya transfoma, wanaacha kununua transfoma Tanzania, wanakwenda kumpa order Manji kuagiza transfoma ya dola 4,000 au 5,000 wakati pale zinatengenezwa transfoma. Sisi na Wajumbe wote wa Kamati tulihuzunika sana na tulimpelekea Waziri wa Viwanda na Biashara tukamwomba akuone! Hili jambo Mheshimiwa, siyo tu ni jipu, hii ni cancer ambayo matibabu yake kwa kweli, lazima yafanywe very serious.
Mheshimiwa Mwenyekiti, madini ya Tanzanite; ninachokielewa na ninachokiona, Mheshimiwa Waziri ni Mtaalam wa Miamba, lakini ukweli ni kwamba, lazima tutafakari kwenye Wizara ya Nishati na Madini tunahitaji Mtaalam wa Miamba ama Mtaalam wa Biashara ya Madini. Tukiweza kulipambanua hilo vizuri tunaweza tukaisaidia sana Wizara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninavyoongea sasa hivi Madini ya Tanzanite yameanguka kwa takribani asilimia 60 mpaka 70! Jiwe lililokuwa likiuzwa shilingi milioni moja mwaka jana mwezi wa 11, leo jiwe hilo linauzwa shilingi 300,000 mpaka shilingi 400,000 hakuna market! Sababu ni moja, kuna confusion kubwa imekuwa created kati ya madini ya tanzanite, ambayo ni cut na madini ya tanzanite ambayo ni rough. Kwa hiyo, nimwombe sana Waziri, waende wakafanye tathmini ya kutosha; watu wote waliokuwa wakinunua madini Arusha wakisafirisha kwenda nje, wote wame-shift position wamekwenda Mombasa, wamekwenda Kenya. Kimsingi ni kwamba, hawataweza kuzuia madini ya tanzanite yasiende kwa njia za panya kufika Nairobi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kitakachoonekana, Nairobi ndiyo watakuwa wana-seal mzigo. Mzigo utaondokea Kenya, kwa hiyo tanzanite yote duniani itaonekana inaondokea Kenya kwenda kwenye Mataifa ambako inanunuliwa kwa sababu, haikufanyika feasibility study vizuri ya kuweza ku-burn hii tanzanite ambayo leo inazuiwa kwenda rough.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba Mheshimiwa Waziri wataalam wako wanapokuja kufanya utafiti wa biashara ya madini wasije tu watu waliosomea miamba inavyotoa madini, waje watu ambao wako business oriented. Leo tunavyoongea Arusha watu wameondoka na kwa sababu ya hii kasi ya Serikali hii watu wanaondoka wanahamisha investment. Biashara kubwa inafanyika Mombasa na jiwe la Tanzanite ukipita nalo kwenye kengele hapo, gemstone haipigi kelele. Kwa hiyo, mawe yataondoka yote Arusha, yatakwenda Mombasa, yatakwenda Nairobi, wata-seal mzigo Nairobi, watakwenda Thailand, watakwenda Marekani, itatokea kama ilivyotokea miaka ya nyuma, Kenya ilipewa zawadi ya ndege kwa kuuza madini mengi ya Tanzanite wakati Tanzania haijawahi kupewa zawadi hata ya baiskeli. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu umeme na mazingira. Tanzania kuna takataka nyingi sana. Amesema Mheshimiwa Japhary kwamba takataka siyo disadvantage, takataka ni umeme. Lakini leo nchi hii tuna claim kuwa na takataka nyingi mijini badala ya kuzi-transform takataka hizi kuwa umeme. Wameongea wenzangu hapa kuhusu biogas, kama Wizara ya Nishati na Madini ingekuwa serious na biogas leo misitu inavyokatwa nchi hii inakatwa kwa sababu hakuna njia mbadala ya nishati ya kupitia tofauti na kuni, lakini ukiangalia maeneo yote ya Usukumani kuna ng‟ombe wengi, kuna vinyesi vingi vya ng‟ombe ambavyo hivi vingeweza kuwa transformed kuwa umeme, vingeweza kuzuia sana uharibifu wa mazingira mkubwa sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo suala la biogas siyo suala la umeme peke yake na kupikia chakula. Ukitaka kuokoa Taifa hili na uharibifu mkubwa wa mazingira, Mheshimiwa Waziri ni shahidi ukiwa kwenye ndege unakwenda Dar es Salaam hapa katikati Morogoro kote kumeanza kuisha. Mawaziri na Wabunge tunanunua mikaa barabarani. Ukiongelea future ya Taifa bila kugusa mazingira ni kujidanganya sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana suala la biogas, mimi ni shahidi nyumbani kwetu ninakotoka kijijini kwa mama yangu tumemfungia biogas ana ng‟ombe wawili, tuna miaka mitatu hajawahi kutumia kuni, tuna miaka mitatu hajawahi kutumia umeme wala hajawagi kununua gesi ya madukani. Kwa hiyo, suala la biogas siyo suala tu la nishati mbadala, lakini nishati ambayo inaweza ikazuia uharibifu mkubwa wa mazingira. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, TANESCO wanapobadilisha nyaya utafikiri wametumwa na ibilisi kuja kukata miti. Hakuna watu wanakata miti hovyo kama TANESCO. Kila wanapobadilisha waya wanakata miti, mti mmoja kukua unachukua zaidi ya miaka mitano mpaka 15 halafu TANESCO wanakuja kubadilisha waya imetumika muda mrefu wanakata mti wote. Kupanda mti mwingine mpaka ufike kwenye maeneo ulikofika ni miaka mingine kumi, tunaendelea kutengeneza jangwa. Waya za siku hizi nimeziona, ni waya ambazo zina plastic, ziko covered na plastic. Unajiuliza kuna sababu gani ya TANESCO kukata miti hovyo badala ya ku-prune miti na kuacha waya zipite kawaida na miti iendelee kuwa mapambo ya miji yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakuomba sana Mheshimiwa Waziri, TANESCO waambiwe kabisa wakitaka kufanya pruning ya miti yoyote wawe na link kwanza na Halmashuri husika ili tukubaliane na Mipango Miji hii miti inakatwaje, kwa sababu watu wanafanya jitihada. Mheshimiwa Mbowe amepanda miti kutoka KIA mpaka Hospitali ya Machame mpaka Moshi Mjini, juzi TANESCO walikuwa wanabadilisha waya, wanahamisha nguzo mimi nikawakuta wamekata. Nikasimama, nikampigia Mbunge simu, nikamwambia Mbunge miti uliyopanda, amenwyeshea mwenyewe kila kitu mwenyewe, miti imefika mita tatu, mita tano juu TANESCO wanakata miti na waya zinazopita pale ni waya ambazo zina plastic cover. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe sana Mheshimiwa Waziri kwamba TANESCO wanavyofanya kazi ya kuweka waya mijini na Mheshimiwa Maghembe analijua hilo tukiwa kwenye kikao cha RCC waliliongea hili. Waangalie kabisa kwamba mazingira ni muhimu kuliko kitu chochote katika nchi hii. Hakuna kitu cha msingi kama mazingira. Kwa hiyo TANESCO watusaidie, wa-communicate na Halmashuri, tukubaliane namna gani ya ku-prune miti na waya zipite bila kuharibu mazingira. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri anafahamu, Waziri Mkuu alikwenda bandarini, alivyofika bandarini akakuta ile flow meter imefunguliwa akauliza, alipouliza Waziri Mkuu akawa na hasira kwa sababu anaipenda nchi yake akakamua jipu. Lakini yule mama alisema nimetumiwa message na Waziri, sasa Mheshimiwa Waziri kwa sababu wewe tulikutolea maazimio mwaka jana na bado leo tuko na wewe, ina maana ni huruma yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, basi kama ni Mheshimiwa Waziri alimtuma yule mama aongee tu na Waziri Mkuu yule mama mumrudishe kazini kwa sababu kwa vyovyote vile yule mama kama aliambiwa na bosi wake fungua hiyo flow meter, halafu mama akasema nimeambiwa na bosi wangu, Waziri Mkuu akatumbua jipi bila ganzi. Mheshimiwa Waziri Mkuu mimi nakuheshimu sana, kwa kweli hebu mfikirieni yule mama kama ambavyo sisi ama wenzako huko ambavyo wamekufikiria wewe Mheshimiwa Waziri. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, mwaka jana tulimfungua na mashati hapa lakini mwaka huu tumekuona umekuja na tunashindwa kuongea vibaya dhidi yako kwa sababu wote waliokuja……
MWENYEKITI: Ahsante.