Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Spika, Asante sana kwa kunipatia fursa hii ya mimi kuwa mchangiaji wa kwanza katika hotuba ya Wizara ya Nishati na Madini.
Mheshimiwa Spika, jambo la kwanza niwashukuru sana wananchi wangu wa Jimbo la Momba na niwashukuru sana vilevile Mahakama Kuu kwa kuhalalisha Ubunge wangu siku ya tarehe 16, baada ya Mgombea wa Chama cha Mapinduzi kunikatia rufaa. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa hayo yote. Sasa niwambie wananchi kwamba tumerudi kwa ajili ya kazi moja tu kuhakikisha Momba inaendelea mbele. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nimesoma Hotuba ya Waziri kidogo ilichelewa, lakini nimepitia Hotuba ya Kamati pamoja na Hotuba ya Kambi ya Upinzani. Kwa mara ya kwanza katika Bunge hili niseme kabisa kwamba Kamati ya Nishati na Madini imejitahidi sana kutoa taarifa inayoelezea matatizo yaliyopo kwenye Sekta nzima ya Nishati pamoja na Madini, niwapongeza sana Kamati ya Nishati na Madini. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, tumekuwa tukizungumza kila mara na Serikali ya Awamu ya Tano imekuja na kaulimbiu ikisema itakapoingia madarakani itapitia mikataba yote na makampuni yote yanayochimba na kuzalisha madini ndani ya nchi yetu, lakini mpaka sasa, hatujasikia mapitio ya mkataba kwenye kampuni yoyote. Hatujasikia na ni kauli ambayo ilitoka kwa Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli. Sasa kwa nini tunaliulizia hili jambo kwa sababu sekta ya madini ndiyo sekta ambayo sisi kama Taifa tumeibiwa sana! (Makofi)
Mheshimiwa Spika, makampuni haya tangu yameanza kuzalisha madini hayajawahi kupata faida na haya yamekuwa yakizungumzwa ndani ya Bunge tangu Mabunge yaliyopita. Bunge la Tisa, la Kumi mpaka hili la Kumi na Moja tunajadili mambo yaleyale na mifano midogo tunayo. Tuna mfano wa Mgodi unaozalisha Almasi wa Williamson Diamond pale Shinyanga, umeanza kuzalisha mwaka 1940, leo tunapojadili ni miaka 76, lakini mpaka leo hawajawahi kupata faida, hawajasitisha uchimbaji wa madini na ukiangalia kwenye malipo yao ya kodi ndani ya hili Taifa hakuna chochote kinachofanyika. Haya ndiyo tunayosema, kile kilichoahidiwa na Serikali ya Awamu ya Tano cha kupitia mikataba, ndiyo kilitakiwa kifanyike sasa, kwa sababu haiwezekeni watu miaka 76 hawapati faida, lakini hawaondoki, wako pale pale.
Mheshimiwa Spika, sasa haya ndiyo maswali ambayo tulikuwa tunahitaji kupata majibu kutoka kwenye Wizara ya Nishati na Madini ambayo iko chini ya Mheshimiwa Waziri Sospeter Muhongo. Kwa hiyo tunahitaji hayo majibu. Tunahitaji majibu juu ya kampuni ya ACACIA ambayo hata Kamati imeeleza, Mahakama ya Usuluhishi imewaambia walipe kodi ya mapato karibu bilioni 89 ambazo walikuwa wamezikwepa kwa kipindi cha miaka minne, lakini mpaka leo kampuni hiyo hiyo inashindwa kulipa na Serikali haijasema, haijatoa kauli na haijachukua hatua yoyote. Sasa haya ndiyo mambo tunayosema, huwezi kuita hapa kazi tu, wakati unashindwa kusimamia makampuni ya namna hii. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, haya tunataka kazi iendane na kukamata hawa watu, walipe hizo bilioni 89 ambazo zimeamuriwa na Mahakama ya Usuluhishi kuhakikisha kwamba Taifa letu linapata hiyo faida. Kwa hiyo, nategemea Mheshimiwa Waziri Sospeter Muhongo atatupatia majibu kwenye majumuisho yake hizi bilioni 89 zilizoamriwa kulipwa kwenye Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa nini mpaka sasa hivi, Serikali inashindwa kuzipata fedha hizi?
Mheshimiwa Spika, lakini, kuna mambo mengine ambayo tulikuwa tumeyajadili. Kwenye Mabunge yaliyopita Bunge liliamuru kwamba makampuni ya uzalishaji wa madini yajisajili kwenye soko la hisa la ndani ya nchi, siyo yafanye cross listing. Unajua, watu wanashindwa kuelewa haya makampuni yamejisajili London yamejisajili kwenye masoko ya nje ambako sisi Watanzania wa ndani hatuwezi kupata taarifa juu ya mwenendo wa haya makampuni, huku ndani tunapata tu taarifa za kawaida na kinachotokea nini? Kule wanapata faida, lakini kwenye taarifa za ndani za Taifa letu hakuna faida yoyote inayoonekana juu ya makampuni haya yanayochimba madini katika hili Taifa letu.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo tunahitaji kupewa majibu juu ya maazimio ya Bunge, juu ya kauli ya Rais ambayo ndiyo ahadi kwa Watanzania lini mtapitia mikataba ya makampuni yote yanayozalisha madini nchini. Kwa sababu madini yaliyoko ndani ya nchini yetu yanakwisha wala siyo kwamba yatakaa milele, ni Non Renewable Resources na kila mmoja anajua hiki kitu. Kwa hiyo, sasa hatutaki kupata mashimo kama yalivyo kwenye Resolute kama tunavyoona kule Tulawaka kwamba Taifa limebakiwa tu na mashimo ambayo sisi kama Taifa hatukupata faida ambayo tulikuwa tunatarajia kutoka na mikataba ambayo sisi tulikuwa tumeingia. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, jambo la pili ambalo tungependa kupata ufafanuzi, Rais wakati anazindua mradi wa pili, kule Kinyerezi aliahidi kwamba atahakikisha mkataba wa IPTL wa kulipa capacity charge, yeye katika Serikali yake, huo mkataba anauvunja na hatalipa ameyasema hayo Mheshimiwa Rais. Sasa kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri sijaliona hili kwamba mpaka sasa ni hatua gani mmechukua kuhakikisha haya Makampuni hayaendelei kulipwa capacity charge yawe yanazalisha umeme, yasiwe yanazalisha umeme? Hebu fikiri, milioni 300 za Kitanzania zinapotea kila siku kampuni izalishe umeme ama isizalishe, hii hasara hatuwezi kuendelea kuwa nayo. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, makampuni haya yalikuja kwa lengo moja tu, kuzalisha umeme wa dharura, lakini mpaka sasa hivi siyo kwamba tuna udharura, udharura haupo sana kama kipindi ambacho kilikuwepo. Sasa hivi tuna uhakika na kile tunachokifanya, lakini mpaka leo haya mambo yanaendelea, sasa tunataka tuambie, maana yake tunajua kauli ya Rais ndiyo kauli ya Serikali, ndiyo msimamo wa wananchi, kwamba tunataka kuona makampuni yote yanafungiwa na maazimio yote ya Bunge yanafuatwa na yanapatiwa mkakati wake.
Mheshimiwa Spika, jambo la tatu ambolo ningependa kulizungumzia, Kamati vile vile imelisema na mimi nilitaka niliseme. Kampuni ya Dangote ilikuja kwa lengo zuri kabisa na naamini bado lengo ni zuri. Imekuja kwa lengo la kuzalisha saruji ndani ya nchi yetu, lakini mpaka leo tunapojadili kampuni ile haitatumia gesi ya nchini, haitumii na wala haitatumia gesi kwa sababu mitambo yake ile imetengenezwa kwa ajili ya kutumia makaa ya mawe. Lakini cha ajabu ambalo Watanzania hawajui, makaa ya mawe yale sio yanayotoka Liganga na Mchuchuma kule. Makaa ya mawe yale yatatoka Msumbiji ambako ni karibu kabisa na Mtwara.
Mheshimiwa Spika, sasa unajiuliza haya maswali kila siku kwamba tunazalisha gesi na gesi ipo kwa wingi lakini tunashindwa kwa sababu moja tu, tumeambiwa wameshindwa kukubaliana juu ya bei halisi, kwamba Dangote anataka senti kadhaa tu. Tunaamini sasa gesi ili iwe faida kwa Taifa, gesi hii ndiyo itumike kwenda kwenye Kampuni ya Dangote, Serikali ipate faida kutokana na mauzo ya gesi ili sisi kama wananchi tuweze kujitegemea huko tunakokwenda. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, jambo la nne, miradi ya REA. Waziri hapa amesema kumeongezeka kwa bajeti, nakubaliana, kwamba imetoka karibu bilioni 357 mpaka mnakwenda kwenye 500. Hata hivyo, changamoto ni nini, mwaka jana, mwaka 2015/2016, tulitenga karibu bilioni 357 kwenye Bunge hili hili la bajeti, lakini mpaka sasa hivi tunapojadili kwenye bajeti ile fedha zilizotoka hazijafika hata asilimia 70. Sasa leo unaleta tena 534, of course umeongea vizuri kwamba hapa hakuna cha MCC, its okay, lakini hela hizi zitafika kwa asilimia 100?
Mheshimiwa Spika, Momba kule mlipeleka miradi ya umeme tukaahidi Halmashauri ya Momba itapata umeme wa REA kufikia mwaka jana 2015 Juni, lakini mpaka leo tunapojadili, mwaka mzima, Momba hakuna umeme. Nguzo zipo pale zimesimama, miradi ya REA haiendelei. Sasa hii changamoto tusiwadanganye Watanzania kwa kutaja viwango vya fedha, tunataka utekelezaji unaoendana kwa vitendo, tuambiwe hela inayokwenda kufanya kazi, kwa hiyo hicho ndicho tunachokitaka. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, unaweza kusema hapa REA tumetenga trilioni moja, its okay, trilioni moja itafikiwa mwisho wa mwaka? Je hizo Bilioni 357 za mwaka 2015/2016 zimefika kwa asilimia 100? Mheshimiwa Muhongo kwenye facts za data najua yeye ni mzuri sana, lakini ngoma ipo kwenye utekelezaji, twende tufanye utekelezaji, ndiyo Taifa tunachotaka. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, jambo la mwisho kwenye issue ya vinasaba, tumekuwa tukiijadili kila mwaka. Vinasaba vilikuwa vimeletwa kwa kazi moja tu, lengo ni kupunguza uchakachuaji…
SPIKA: Mheshimiwa…
MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.