Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa na Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha uliuoishia tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa za Mamlaka za Seriakli za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishi tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezajiwa wa Mitaji ya Umma kuhusu uwekezaji wa mitaji ya umma kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa na Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha uliuoishia tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa za Mamlaka za Seriakli za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishi tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezajiwa wa Mitaji ya Umma kuhusu uwekezaji wa mitaji ya umma kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nami niongeze machache ambayo Kamati yetu imeweza kuyaona wakati tukipitia hizi ripoti. Nitaanza kwa kuvuta kumbukumbu ya taswira ya Mheshimiwa Rais, siku napokea Ripoti ya CAG nitaenda kunukuu maneno aliyoyasema na kila mmoja aliyasikia na vyombo vyote vya habari viliandika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitaanza kusoma, anasema; “Invoice imekuja tunatakiwa kulipa dola milioni 88 unaliza mkataba ulisemaje, hii imetokea wapi? Unaambiwa vifaa vimepanda. Nauliza Mkataba wenu ulisemaje? Mtu anapopokea bila kuuliza, anailetea Serikali ilipe, stupid!”

Mheshimiwa Mwenyekiti, aliendelea kati ya maneno mengine aliyoyasema; “Miradi mingine ambayo tunaifanya inakuwa ni mikubwa ambayo matazamio yake yanajulikana.” Akauliza maneno na akasema; “oneni uchungu na fedha za Serikali, na hivyo vinafanyika kwa sababu kuna watu wanafaidika.” Akaenda mbele zaidi akasema; “Kuna sehemu tumezubaa, pengine kwenye primitive measures, hatuchukui hatua.” Mwisho wa kunukuu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeanza na hayo maneno kwa sababu siku hiyo Mheshimiwa Rais, anawasilisha hotuba niliangalia vizuri na nilimwangalia. Nikaona picha ya mama akionyesha machungu ambavyo anatambua ukubwa, utajiri wa rasilimali zilizopo kwenye nchi lakini zinapigwa na watu wachache. Kamati yetu ya PAC kama ilivyopitia LAAC, tumechukua masaa ya kutosha kukaa, kujadili zile ripoti na baadaye tunajiuliza tuweke nini, tuache nini, kwa sababu ni madudu bandika bandua. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya waliyoyataja wenzetu ni baadhi tu, lakini changamoto yetu kubwa haijawahi kuwa kwenye mifumo, haijawahi kuwa kwenye utaratibu, imekuwa kwenye kitu kimoja ambacho nimekitaja na kukiandika mara tatu, nikasema kutekeleza, kutekeleza kutekeleza. Utaratibu umeandikwa na umeainishwa vizuri, utaratibu wa kuingia, kuhama, kuheshimu na kutimiza matakwa ya Mikataba, tumekuwa hatufanyi hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, utaratibu umeainisha nini cha kufanya, lakini Watendaji wetu wameacha kufanya yote tunayoyasema. Msemaji mmoja hapa ametueleza kilichotokea katika MSD nitatoa mfano na nitaueleza vizuri. Mtendaji na baadhi ya waliohusika kwenye MSD waliingia kwenye Mkataba na Kampuni moja ya kutoka Misri, ameitaja mwenzangu inaitwa Alhandasia ya kunua vifaa tiba. Ikatanguliza fedha zaidi ya bilioni 3.4 ika-deposit kwenye akaunti, akaunti inajulikana ambayo naweza nikakutajia hapa, ambayo jina la Akaunti inaitwa ASM e-trade, akaunti namba iko hapo 0045609416002 iko kwenye Benki ya Egypt Gulf.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya ku-deposit hizo fedha akijua moja ana-deposit hizo fedha bila ya kuona, ameshinda kandarasi, anapaswa kuonyesha at list uwezo wa ku-perform hizi contract, hajafanya hicho kitu, lakini pia hajafanya utafiti kuja kama ana-exist au ha-exist kwa maana hapati assurance ya benki, lakini ame-deposit zaidi ya bilioni tatu kwenye akaunti ya mtu. Wakasubiri zaidi ya miezi mitatu madawa hayaletwi. Wakaanza kui-consult hiyo kampuni inapatikana wapi, wakamtumia taarifa balozi wetu Misri, akatafuta hiyo kampuni haikujulikana kampuni iko wapi. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hiyo kampuni kwa fedha ambayo wali-deposit ambayo ni bilioni 3.4, tulipaswa kupata aina 75 za madawa tofauti tofauti. Baada ya mkataba kushindikana ikabidi wa-recall kampuni nyingine na hiyo kampuni wakaiambia sasa tusaidie kuchukua hata yale madawa ambayo alipaswa kuleta huyu Alhandasia, tukuongezee kwenye Mkataba uweze ku-delivery akakubali kufanya hivyo. Sasa wakampa mkataba wa bilioni 10, lakini katika ku-delivery akaonyesha katika zile product ambazo alipaswa ku-delivery 75 katika hizo ame-delivery product 29 tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa unaweza ukaona nini changamoto ambayo ameieleza mwenzangu. Tulifanya nini, tulifanya due diligence kujihakikishia kwamba hiyo kampuni ina-exist, tulikuwa na assurance performance ya contract na wale watu, hayo ndiyo yanafanyika katika kila item ambayo naigusa hapa. Changamoto ya hii nchi siyo fedha wala siyo uchumi, changamoto ni watendaji ambao wameamua kwa makusudi mazima bila kufuata kanuni na taratibu. Mheshimiwa Rais, akasema tumewanyamazia pengine tuchukue primitive measures, tuweze kuwawajibisha na nataka niulize hapa ni wangapi wamewajibishwa kwa kuisababishia Serikali hasara ya mabilioni ya fedha yanayoongelewa leo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumekuwa tukiona kwenye vyombo vya Habari, mtu ameiba zaidi ya bilioni kadhaa, trilioni kadhaa, lakini faini anayokuja kutozwa ni milioni kadhaa na umeshakuwa mtindo wa kawaida tu, iba bilioni utaenda kulipa faini ya milioni, hauwezi kuwa ndiyo mtindo wa maisha na tukaenda, hatutofika kokote kwa mtindo huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama hiyo haitoshi wakagundua chaka lingine na Mheshimiwa Mwenyekiti wa LAAC, ameieleza vizuri, kuna chaka linaitwa TAKUKURU. Sasa siwezi kueleza chochote kwa sababu sijui, lakini kwa mazingira yanayoonekana TAKUKURU ndiyo namna pekee ya watu kuficha madudu yao kwa sababu wanajua tutakagua kwa zaidi ya miaka 10, 15 na baadaye ushahidi utakosa na faili litafungwa na business as usually. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo hiyo tu, miradi mingine ambayo imekuwa kwa Watumishi wa Umma ambayo wameisababishia Serikali hasara ni kuhamishwa katika hiyo idara hata haya tunayoyaongelea leo kwenye MSD wamehamishwa kutoka MSD wakapelekwa kwenye idara nyingine, hivi hilo lengo ni nini? kupeleka hasara kwenye maeneo mengine au kuendeleza kutuliza kila sekta. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais, anazunguka kila sehemu kutafuta fedha, anahangaika na tozo kila maeneo, lakini kinachofanyika leo ni nini? Ni mifuko yote inavuja asubuhi, mchana na jioni, hatuwezi kwenda namna hiyo. Hivyo naungana na Hotuba ya Kamati zote tatu, pamoja na Kamati yangu hususani juu ya pendekezo la MSD, moja TAKUKURU kukamilisha uchunguzi, lakini pia ni lazima kuwepo na action za kimaadili kama kuna watu wamefanya makosa kwenye Serikali…

WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Waziri.

TAARIFA

WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana mchangiaji lakini naomba nimpe taarifa kwamba, wahusika waliohusika na ubadhirifu au uvunjaji wa taratibu za manunuzi chini ya MSD wameondolewa kabisa MSD Tarehe 22 Aprili, 2022. Mheshimiwa Rais aliteua Mkurugenzi mpya na sasa hivi mambo yanaendelea vizuri taratibu zilizobaki ni za kiuchunguzi wa TAKUKURU na vyombo vingine vya uchunguzi. Hatua zimeshachukuliwa tangu Aprili, 2022.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Anatropia unaipokea hiyo taarifa?

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Bahati mbaya sana kwenye Kamati ambayo Mheshimiwa Spika alinipanga tunaongelea value for money.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukimwondoa katika nafasi yake ume-save shilingi ngapi, nadhani hoja ziwe baada ya ule ubadhirifu alivyovifanya tumeweza kuangalia alikuwa ana kiwango gani ambacho tumekiweka wakati kesi zikishughulikiwa, fedha za walipa kodi ziweze kuwa zimeokolewa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nadhani hiyo iwe spirit kwa sababu lengo ni kusaidia Taifa na lengo la Mheshimiwa Rais ni kuhakikisha anapata fedha za kuendesha nchi. Pia watu wanauliza alipelekwa wapi, karudishwa Jeshini kuendelea kufanya kazi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee pia suala la KADCO najua muda wangu utakuwa mchache lakini nilikumbushe Bunge lako tarehe 2 Novemba hapa mwaka jana iliongelea suala la KADCO pamoja na kutoa maazimio ambayo maazimio ya KADCO ni pamoja na KADCO kuwa chini ya Mamlaka ya TAA lakini hilo suala mpaka leo halijaweza kufanyiwa kazi, lakini hiyo haitoshi Baraza la Mawaziri lililokaa katika Kikao Namba 15 cha mwaka 2009 liliwahi kutoa maazimio ya kiwanja cha ndege cha Kilimanjaro kuwa chini ya TAA lakini mpaka leo tunavyoongea miaka 14 baadae hakuna chochote kilichofanyika. Call yetu tunayoitoa ni lazima KADCO sasa iende kwa mujibu wa utaratibu unavyosema kwamba viwanja vya Serikali vitaendeshwa chini ya mamlaka ambazo zimeanzishwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba niishie hapo kwa hayo machache. Ninaunga mkono maazimio yote yaliyotolewa na Kamati yetu Tukufu. Nakushukuru sana (Makofi)