Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge kuhusu Wakala wa Kimataifa wa Kimataifa wa Nishati Jadidifu (International Renewable Energy Agency - IRENA) na Azimio la Bunge kuhusu mapendekezo ya kuridhia Mkataba wa Kuanzisha Taasisi ya Dawa ya Afrika wa Mwaka 2019 (Treaty for the Establishment of the African Medicine Agency - AMA)

Hon. Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge kuhusu Wakala wa Kimataifa wa Kimataifa wa Nishati Jadidifu (International Renewable Energy Agency - IRENA) na Azimio la Bunge kuhusu mapendekezo ya kuridhia Mkataba wa Kuanzisha Taasisi ya Dawa ya Afrika wa Mwaka 2019 (Treaty for the Establishment of the African Medicine Agency - AMA)

NAIBU WAZIRI MKUU NA WAZIRI WA NISHATI (MHE. DKT. DOTO M. BITEKO): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nomba nikushukuru tena kwa kunipa nafasi hii ili niweze kuhitimisha hoja hii.

Pili, naomba niwashukuru sana Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, chini ya Mwenyekiti wetu Dkt. David Mathayo kwa umakini wao na uchambuzi mzuri sana walioufanya wakati tumewasilisha mapendekezo ya kuridhiwa kwa mkataba huu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kamati ilifanya kazi kubwa sana na kwa kweli imeturahisishia sana hata sisi Wizara wakati wa kupitia mambo mbalimbali. Kamati ilifanya kazi kubwa ya kuwatafuta na kuwasikiliza wadau, kuona maoni yao, mashaka na wasiwasi walio nao kwenye Azimio hili. Kwa kweli, niwashukuru sana ubunifu wao umetusaidia. Wadau waliofika kwama TPSF na Jumuiya ya Nishati Jadidifu walitoa maoni ambayo kwa kweli yalikuwa yamewekwa kwa umakini mkubwa. Yaliandikwa kabisa na wengine walisema kwa michango yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kifupi, michango ya Waheshimiwa Wabunge wengi waliozungumza kuhusiana na Azimio hili, ni michango iliyounga mkono sisi turidhie na hoja kwamba, tulichelewa ni hayo waliyoyasema kwamba, wasiwasi ni akili na kwamba kawia ufike, bora tumechelewa tuwe na uhakika wa kile tunachoingia. Nataka niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge wote waliotoa michango yao tunawashukuru sana, sana kwa sababu wamefanya kazi hii iwe rahisi na tutakapokuwa tunapitia sera zetu hasa za nishati jadidifu, tutazingatia kwa umakini mkubwa maoni waliyoyatoa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu Waheshimiwa Wabunge wengi wameunga mkono, niseme wote wametuunga mkono kwenye jambo hili. Hivyo, nisingependa kuchukua muda wako kutoa maelezo marefu. Naomba tena nikushukuru wewe na niwashukuru sana Waheshimiwa Wabunge kwa michango yao. Nataka niwahakikishie kwamba, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, aliposema anaifungua nchi ni pamoja na sisi kuingia kwenye Majukwaa ya Kimataifa kama haya, ambapo tunaweza kupata fursa mbalimbali za kujua taarifa mbalimbali hasa kwa sababu dunia ipo kwenye stress ya nishati na nishati jadidifu ndiyo kimbilio la kila mmoja hapa duniani, kwa sababu ya masuala ya kimazingira. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka niwatoe wasiwasi kwamba Mkataba huu hautufungi kwa namna yoyote. Mkataba huu hata gharama ya kulipa ni ndogo, lakini muhimu zaidi tukiona kuna jambo haliendi sawa tuna uwezo wa ku-call off na kuweza kuendelea na maisha mengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba niwasilishe Azimio kwa kusema yafuatayo:-

Kwa kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni miongoni mwa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa;

Na kwa kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni miongoni mwa Nchi Mwanachama wa Taasisi za Ushirikiano wa Kiuchumi Kikanda wa Jumuiya mbalimbali hapa Afrika;

Na kwa kutambua kuwa malengo yaliyomo katika mkataba wa IRENA iliyoanzishwa tangu tarehe 26 Januari, 2009 yana lengo ambalo sisi kama Taifa tunahitaji pia kujiunga;

Na kwa kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inazo rasilimali za nishati jadidifu katika maeneo mbalimbali hapa nchini na yaliyotajwa katika Sera yetu ya Mwaka 2015 na madhumuni yaliyoko kwenye Mkataba huu nimeyaeleza kwa kina kwenye maelezo yangu ya awali pamoja na manufaa tutakayoyapata,

Hivyo basi kwa kuzingatia manufaa ambayo Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itakayoyapata, naliomba Bunge lako lipitishe Azimio hili kuhusu Mapendekezo ya Tanzania kuridhia Mkataba wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati Jadidifu wa Mwaka 2009.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kutoa hoja. (Makofi)