Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naendelea kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa uwasilishaji mzuri wa mpango wa makadirio ya mapato na matumizi ya fedha kwa mwaka wa fedha 2016/2017.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nina hoja chache za kuandika au kutoa ushauri kwa maandishi, ili zifanyiwe kazi na Wizara kama ifuatavyo:-
(i) Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna tetesi kuwa moja ya sababu inayosababisha kukawia au kucheleweshwa kwa uunganishaji upya wa mashirika mawili ya reli ya kati yaani TRL na RAHCO, ni tetesi au madai kuwa kuna baadhi ya watendaji ndani ya Wizara ambao wana maslahi ya binafsi ya kibiashara kupitia miradi inayosimamiwa na RAHCO. Naomba Mheshimiwa Waziri uchunguze hili.
(ii) Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali ifanye juhudi kubwa katika kuzifufua upya na kuziimarisha karakana za TRL za Morogoro na Tabora ili ufanisi wa kiufundi na kuimarisha vichwa na mabehewa ya treni uweze kuwa wa uhakika.
(iii) Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Mfuko wa Maendeleo wa Mawasiliano kwa Wote hadi Aprili, 2016, Jimbo la Tabora Mjini lenye jumla ya kata 29, kata za Kalunde katika vitongoji vya Ulundwa na Ilamba, kata ya Ifucha, vitongoji vya Miziwaziwa, Usuhilo na Ugurudu, kata ya Ntalikwa, kitongoji cha Shimo la Udongo, kata ya Uyui, kitongoji cha Imala Mihayo na Kakulungu na kata ya Ndevelwa, vijiji vya Ibasa na Izenga, hakuna kabisa mawasiliano ya simu. Ninaomba Wizara iwakumbuke wananchi hawa katika uwekaji wa minara ya simu ili nao waweze kupata mawasiliano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.