Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa za Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Prof. Kitila Alexander Mkumbo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ubungo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa za Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

WAZIRI WA MIPANGO NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Spika, na mimi nishukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia hoja tatu. Nitakuwa na mambo manne, la kwanza ni muktadha, muktadha ni kwamba humu ndani Bungeni tuna Waheshimiwa Wabunge sisi wote lakini pia kuna Serikali na kila mtu apewe nafasi ya kufanya kazi yake. Kazi ya msingi ya Mheshimiwa Mbunge ni kuhoji Serikali. Kazi ya sisi tuliopo huku ni jukumu letu la msingi kujibu hoja za Wabunge. (Makofi)

Kwa hiyo, tunaposimama kujibu hoja za Wabunge isionekane kwamba tunatetea majambazi, haiwezekani, Serikali ya CCM ilishafunga Mawaziri. Kwa hiyo, suala la kupeleka majambazi na wezi mahakamani halijaanza leo lipo. Wapo Mawaziri, wapo Makatibu Wakuu walishafikishwa mahakamani, muhimu ni kwamba sheria lazima zizingatiwe. Kwa hiyo, nataka kuweka vizuri hili kwamba tunapofanya shughuli yetu ya msingi ya kujibu baadhi ya hoja za Waheshimiwa Wabunge isionekane kwamba tunafanya makosa kama ambavyo Waheshimiwa Wabunge mnahoji kama jukumu lenu na sisi tuna haki ya kujibu hoja za Waheshimiwa Wabunge. Kwa hiyo, tupewe nafasi hiyo. (Makofi)

Katika Taarifa ya CAG mambo ya msingi tunakubaliana na kwa kweli hamna Waziri hapa anayebishia Ripoti ya CAG, lakini kuna hoja ambazo Waheshimiwa Wabunge wamezisema mimi kama Waziri wa Serikali ninawajibika kuzijibu. Kwa mfano, mtu anasema naomba ninukuu; “na leo nasisitiza kuwa tumepigwa zaidi trilioni 280.”

Mimi kama Waziri wa Mipango ninayefahamu kwamba pato la Taifa lote nchi hii ni shilingi trilioni 141, nitaacha vipi kujibu hoja hii? Yaani kutoka Kagera mpaka Pemba, ukikusanya fedha zote za Watanzania ni shilingi trilioni 141. Mtu anasema zimepigwa trilioni 280 how? Logic inakataa. Kwenye argument kuna kitu kinaitwa fallacy, kwamba premise and conclusion lazima zioane pale zikigongana ina kuwa inconsistency inakuwa ni mkanganyiko huo ni mkanganyiko wa hoja ninawajibika kuizijibu. (Makofi)

Mtu anakuambia, Mheshimiwa Mbunge anasema nchi inakufa hiyo kwenye CAG report haipo…

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, Taarifa.

SPIKA: Mheshimiwa Jesca Msambatavangu, Mheshimiwa Profesa Kitila, kuna taarifa.

TAARIFA

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, ahsante, nilikuwa naomba kwa kuwa wamesema wanajibu hoja nilikuwa naomba pia anajibu hoja kama Serikali anachangia whatever. Hizi anazosema trilioni mia na, zimehusiha na hizi za wizi ambazo CAG amezigundua na ambazo hatujazigundua, hizo trilioni. (Kicheko/ Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Profesa Kitila Mkumbo unaipokea taarifa hiyo?

WAZIRI WA MIPANGO NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Spika, ameuliza swali siyo taarifa, kwa hiyo, sihitaji kushughulika nayo hiyo.

Kwa hiyo, nilikuwa natoa mfano, nimetoa mifano miwili tu; mfano wa pili nyinyi wote mliopo Waheshimiwa Wabunge na sisi, ni nchi yetu. Sisi ni viongozi, mMtu anakuambia nchi inakufa hiyo katika political science unaongelea…

SPIKA: Mheshimiwa Profesa Mkumbo, kuna taarifa nyingine kutoka kwa Mheshimiwa Mpina.

TAARIFA

MHE. LUHAGA J. MPINA: Mheshimiwa Spika, anajieleza vizuri kwamba amefanya financial analysis kwamba trilioni 280 haziwezi kupigwa. Sasa yeye katika financial analysis yake anajua zimepigwa ngapi? (Kicheko/Makofi)

SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, naona taarifa zenu zinatoka kwa sura ya maswali ambayo Mheshimiwa Waziri kwa kweli halazimiki kujibu, kwa sababu ili Serikali iweze kujibu maswali ni katika kipindi cha maswali na majibu. Mheshimiwa Waziri.

WAZIRI MIPANGO NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Spika, nirudie tena hoja lazima iwe na mantiki, fedha zote za nchi hii kwa taarifa ya mwaka jana ni trilioni 141. Mantiki inakataa kwamba zimeibwa trilioni 280, ni logic ya kawaida. Mantiki inakataa. Ya tatu…(Makofi)

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, hiyo ni taarifa ya ngapi?

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Spika, naomba ya mwisho.

SPIKA: Haya, Mheshimiwa Mtaturu, taarifa.

TAARIFA

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, nimefurahi sana kaka yangu Mheshimiwa Profesa Kitila Mkumbo ni Waziri wa Mipango. Naomba tu nimpe taarifa, kwamba miongoni mwa Taarifa ya CAG mambo yaliyojitokeza makubwa ya upotevu wa fedha ni pamoja na kuzima POS zaidi ya siku 1000. Yeye kama Waziri wa Mipango, tunaomba jibu namna gani Serikali itachukua hatua kwa zile POS zilizozimwa?

SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, hiyo ilikuwa ni taarifa ya mwisho kwa Mheshimiwa Profesa Kitila Mkumbo, malizia mchango wako.

WAZIRI WA MIPANGO NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Spika, mfano wa pili, sisi ni viongozi we must be responsible. Mtu anakuambia nchi inakufa, hiyo kwenye political science maana yake failed state, siyo kweli. Unasemaje nchi inakufa inayojenga reli yenye kilometa 2600 kutoka Dar es Salaam hadi Kalema? Unasemaje nchi inakufa iliyotoa Rais wa IPU duniani how? Nchi ambayo dunia nzima imeiamini ikakubali kutoa Spika, inakufa vipi? Nonsense. (Makofi)

MHE. LUHAGA J. MPINA: Mwongozo wa Spika.

WAZIRI WA MIPANGO NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Spika, ndio nasema pale ambapo hoja haina mantiki kama Waziri wa Serikali ya Rais Samia lazima nijibu.

Mheshimiwa Spika, haya niendelee nichangia kidogo kwenye CAG Report. Ukweli ni kwamba kisaikolojia macho ya binadamu yameumbwa kuona mabaya kuliko mazuri, ni kisaikolojia, lakini ndani ya CAG Report ameonesha yeye mwenyewe kwamba hatua kadhaa zimepigwa kwenye kutekeleza mapendekezo yake naomba ninukuu vipengele vinne muda ukiniruhusu.

Mheshimiwa Spika, kwenye Taarifa ya Ripoti ya Mwaka ya Miradi ya Maendeleo Utendaji wa Kifedha, ukurasa wa pili, CAG anasema; “zaidi ya asilimia 90 ya miradi ilipata hati zinazoridhisha kwa miaka mitano mfululizo kuanzia mwaka 2017/2018. Hii ikiwa ni ishara nzuri kwenye matumizi ya fedha na utendaji wa Serikali.” (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukurasa wa pili, naomba nirejee tena alisema nini kuhusu Mradi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere, kwa sababu hoja imekuja hapa kwamba mradi umechelewa alisema nini. CAG anasema na nanukuu; “Nilibaini makadirio ya muda wakumalisjha mradi usio halisi, kwani mradi ulipangwa kumilika katika kipindi cha miaka mitatu, huku miradi ya ukubwa kama huo iliyojengwa duniani huchukua kati ya miaka minne hadi miaka kumi kukamilika, makadiro ya awali hayakuwa halisi.” (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hii maana yake ni nini, maana yake ni kwamba wataalamu walitoa mapendekezo yao, lakini kuna mtu akatumia maamuzi ya kisiasa akaweka mradi huu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kuchelewa kwa mradi siyo kwa sababu ya fedha…

MHE. LUHAGA J. MPINA: Mheshimiwa Spika, Taarifa.

WAZIRI WA MIPANGO NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Spika, mfano wa tatu CAG…

SPIKA: Mheshimiwa, Sekunde 30, malizia.

WAZIRI WA MIPANGO NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Spika, mfano wa tatu, CAG kwa miaka mitano mfululizo amelalamika juu ya deni la TANESCO na TPDC. CAG akatoa mapendekezo kwamba Serikali iyageuze madeni haya na kuyasafisha vitabu vya mashirika. Serikali ya Mheshimiwa Rais Samia miaka mitano imekubali na imetekeleza na CAG amesema pale. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mfano wa nne CAG alitoa mapendekezo kwamba Serikali ilipe madeni PSSF kiasi cha trilioni mbili kupitia Hati Fungani, Serikali imelipa na CAG amesema. (Makofi)

SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa. Muda wako umekwishwa.

WAZIRI WA MIPANGO NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Spika, umeisha? (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja. (Makofi)