Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Martin Alexander Mtonda Msuha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. MARTIN M. MSUHA: Mhshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchukua nafasi hii kuungana na wenzangu kuwapongeza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano na Naibu wake kwa hotuba nzuri iliyosheheni mipango mizuri juu ya utekelezaji wa shughuli za Wizara hiyo kwa mwaka tajwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sekta ya ujenzi; kutokana na mvua nyingi zilizonyesha msimu uliopita, barabara nyingi za Jimbo la Mbinga Vijijini zimeharibika vibaya sana kiasi cha kuathiri shughuli za usafirishaji na uchukuzi ndani ya jimbo. Njia nyingi zilifunga mawasiliano kama barabara zifuatazo; Mbinga - Mkumbi - Lugari, Mbinga - Linda - Litowo, Linda - Muhongozi, Kigonsera - Matiri - Kilindi, Lipumba - Kihangimahuka, Muhongozi - Paradiso. Nimuombe sasa Mheshimiwa Waziri aweze kutoa waraka au agizo kwa Meneja wa TANROADS Mkoa, aweze kuchukua hatua za haraka ili matengenezo ya barabara hizo yaweze kufanyika mara moja ikiwa ni pamoja na ujenzi wa madaraja kama lile la Mapera, Mto Lukanzauti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara iangalie uwezekano wa kuingiza kwenye mpango wake wa mwaka ujao kipande cha barabara ya kutoka Mbinga Mjini hadi Longa kwa kiwango cha lami ili kuunganisha na mradi wa ujenzi wa barabara ya kutoka Longa hadi Litowo unaojengwa kwa ufadhili wa European Union kwani itakuwa ni kituko kuacha kipande hicho kuendelea kuwa cha vumbi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu uchukuzi; katika sekta hii naiomba Serikali iangalie yafuatayo; ununuzi wa meli mpya katika Ziwa Nyasa na upanuzi wa Bandari ya Mbamba Bay.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mawasiliano; napenda kuipongeza Serikali kwa dhati kwa hatua iliyofikiwa katika sekta ya mawasiliano hususani mtandao wa simu za mkononi. Hata hivyo, naomba waombwe tena Kampuni ya Halotel ili iweze kufikisha mawasiliano ya simu za mkononi kwenye maeneo yafuatayo; Kingoli, Kata ya Litumbandyosi, Mihango Kata ya Kigonsera, Lukiti - Linda, Litembo - Litembo, Mahilo - Kitura, Kindimba Chini - Muungano, Sara - Muhongozi, Kilindi - Matiri, Barabara - Matiri, Kikuli - Mikalanga, Makonga - Miukalanga, Matuta - Kipapa, Mbuta - Kamabarage, Mhimbazi - Amani Makolo, Lipumba - Kihangimahuka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha na kuunga mkono hoja.