Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa za Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa za Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia, cha kwanza nimshukuru Mheshimiwa Rais kwa utulivu wa nchi yetu, lakini pia kwa kutupa nafasi ya kujadili masuala yanayohusu nchi yetu kwa uwazi na bila woga. Sasa kazi iliyobaki ni sisi Wabunge kuwasimamia wananchi ambao wametutuma kuja hapa kusema haki na kuwasemea katika mambo yale ambayo ni maovu.

Mheshimiwa Spika, hii document ya CAG iko wazi, ni public document kwa hiyo kila mtu anaiona. Hata hapa mtu akisema ataonekana kwamba labda huyu akisema hivi amesema vibaya tutakuwa tunajidanganya tu, kwa sababu hii document iko wazi na hata mataifa mengine wameshaisoma. Kwa hiyo, ni kazi yetu sisi Wabunge kuwasemea wananchi ambao wametutuma kuja hapa kusema yale ambayo yanawafaa. Maana yake itakuwa ngumu sana kutosema ambapo unaangalia kila kurasa tatu za majedwali, kila majedwali kumi, matano, manne, matano, sita, saba Halmashauri ya Bunda imo.

Mheshimiwa Spika, kila ukizungumza wizi wa vifaa vya tiba Halmashauri ya Bunda imo, kila ukiuliza sijui hela za POS hazikuja Halmashauri ya Bunda imo. Wakati fulani inaniwia vigumu sana kusema hii ripoti kila wakati inaangalia Bunda na Bunda ndiyo jimbo langu na Halmashauri ndiyo Halmashauri yangu, mnaohusika mmeiona hiyo.

Mheshimiwa Spika, nilikuwa najiuliza maswali mengi na Bunge lililopita tulisema hivi haya maazimio tunayoweka humu ndani yanaenda wapi, yaani nani anayatekeleze? Sasa nikajiuliza wewe Spika na Bunge lako katika Katiba Ibara ya 143 umepewa mamlaka, Ibara ya 96(1) imelipa mamlaka Bunge hili kuunda Kamati mbalimbali na tumeweka PAC, tumeweka LAAC na tumeweka PIC.

Mheshimiwa Spika, sasa najiuliza tuunde Kamati nyingine ambayo itakuwa inafuatilia maazimio ya Ripoti ya CAG. Najiuliza tarehe 2 Novemba, 2022 tulizungumza juu ya KADCO na tukaamua katika azimio kwamba sasa Serikali iende ikachukue uwanja wa KIA yaani Kampuni ya KADCO itoke uwanja wa KIA ikabidhiwe Serikali kwa Mamlaka ya Ndege Tanzania.

Mheshimiwa Spika, azimio tumeweka na mbaya zaidi nimesoma hapa mpaka Baraza la Mawaziri wameweka wamezungumza hili jambo, mpaka leo tunazungumza hamna kitu. Sasa hayo maazimio tunampa nani, yaani hii kelele tunampigia nani kwa mfano, maana yake mimi naona wezi wote tunaowazungumza humu ndani wengi wameteuliwa na Mawaziri, wengi wameteuliwa na Rais na wengi tunao sisi Chama Cha Mapinduzi ambao ndiyo waamuzi.

Mheshimiwa Spika, yaani Rais wa Chama Cha Mapinduzi, Mawaziri wa Chama Cha Mapinduzi, wezi wanaiba, chama kinawataka wawafukuze wezi hawawatoi. Maazimio ya Bunge tunataka, maazimio ya Bunge hili, mwizi na mtetea mwizi wote waende lock up wote mazianyati, tumechoka sasa, tunamtetea nani? Kwa mfano, sasa lile azimio limesema, ninajiuliza hiyo KADCO ni mtu au ni nani, yaani KADCO ni chombo fulani au nini sasa?

Mheshimiwa Spika, kama azimio la Bunge limesema, Mawaziri wamesema na jambo halitekelezeki na siyo kwamba hiyo KADCO inaleta faida, imetengeneza hasara karibu ya shilingi bilioni sijui tano. Hivi ni nini sasa tunasema, tunazungumza kufanya nini? Mheshimiwa nafikiri kwamba tuunde Kamati nyingine ambayo itashughulika na jambo hilo ili itusaidie.

Mheshimiwa Spika, sasa nilikuwa nasikia Wabunge wanazungumza wizi wizi, wizi, nimesoma ripoti hii nimegundua kumbe wizi siyo peke yake tu, yaani hapa tunapokwenda kunadalili ya mauaji ya Watanzania wasio na hatia. Hivi kama vituo vya afya na zahanati 16 na kama hospitali za mkoa na hospitali za rufaa 17 zinakuwa na madawa yaliyoisha muda wake zaidi ya miezi mitatu mpaka miaka kumi ikiwemo Benjamin Mkapa ambapo tunatibia Wabunge.

Mheshimiwa Spika, dawa zimeisha muda wake zenye thamani ya shilingi bilioni 3.5 zimeisha muda wake, sasa hapa tunasema nini, tunazungumza kupata nini? Yaani leo Tanzania ambayo tuna wasomi, tuna mifumo ambayo inaangalia expire date iko wapi kwneye dawa, leo tuna dawa, vituo vya afya, zahanati, bohari kuu zimeisha muda wake na zipo. CAG anasema miezi mitatu mpaka miaka kumi, zipo.

Mheshimiwa Spika, hiyo ni dalili moja wapo ya kwamba huko tunakokwenda tutaua Watanzania wasio na hatia na wataalam tunao. Mimi nafikiri kwamba nalo hilo tuliangalie maazimio haya tunampa nani? Lazima tukubali sasa kwamba Bunge lijalo kama kuna Ripoti ya CAG tupate kwanza maazimio yetu tuliyoyaweka Bunge hili kama yametekelezwa, kama hayakutekelezwa hakuna haja ya kujadili, tunajadili nini sasa. Nafikiri kwamba tuangalie kwamba inakuwaje.

Mheshimiwa Spika, nimeangalia kitu kinaitwa GPSA, taasisi mbalimbali zimeagiza magari shilingi bilioni 35 point, mpaka ripoti hii inatengenezwa hayajaja, labda sasa sijui kama tutajibiwa au itakuwa muda mwingine. Shilingi bilioni 35 magari yameagizwa hayaji, watu wanadai magari, hayaji, hela zimetolewa. Sasa tunamwambia nani? Tuunde Kamati ya kufuatilia maazimio hayo ili tuweze kuwa na uhakika wa jambo hili.

Mheshimiwa Spika, kuna mikataba yaani tunaajiri wakandarasi, tunatengeneza mikataba, tuna wanasheria na tuna kila kitu, riba shilingi bilioni 418; yaani tunalipa watu hewa, mtu umemtengenezea mikataba riba shilingi bilioni 418, ukigawa kwa shilingi 500 kituo cha afya ni vituo karibu 387. Tunagawa, yaani unawapa watu bure tu, shilingi bilioni 418. Watoto wanakaa chini, hali ni mbaya zahanati hazijafikia, tunagawa. Kwa hiyo, nafikiri kwamba tuunde kamati ya ufuatiliaji wa jamnbo hili.
Mheshimiwa Spika, lakini la mwisho, Wabunge wamesema mambo mengi hapa ukisema ni kumalizia tu, mambo mengi yamezungumzwa humu ndani. Amezungumza mtu mmoja hapa jana Mbunge na Wabunge wengi wamesema hili Bunge letu sasa linatazamwa, lina Spika wa Mabunge ya Dunia. Kwa hiyo, sasa lazima tuangalie na nimekusikia kwenye kauli yako wakati unahitimisha baada ya kupata zilke kura nyingi ukasema kwambva IPU fedha zao mali yao itakaa salama. Naomba sasa usalama wa Watanzania wa mali za umma ukae salama kwenye Bunge hili waanzie hapa. Nikuombe waanzie hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa hivi Mkurugenzi hivi tukizungumza hapa tunamzungumza Rais, hivi Rais amemteua Mkuu wa Mkoa amemteua Mkurugenzi kwenda kuiba?

MJUMBE FULANI: Hapana.

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, Rais amemteua Mkurugenzi kwenda kuiba? Tunamsaidia Rais wezi wote walioiba huko dani tuwatoe. Siku moja niliwahi kusema hapa na narudia…(Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Getere malizia sekunde 30 muda wako umeshaisha.

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, niliwahi kusema hapa, nikibahatika kupata Uwaziri au Unaibu Waziri baada ya siku tano mtakuwa mmenifukuza, kwa sababu ziara yoyote nitakayoenda kila nitakaemkuta ameharibu ni lock up, lock up, lock up, nikirudi mtasema nimekiuka demokrasia, mtanifukuza kazi, ahsante sana. (Makofi)