Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara kuendelea kukamilisha zoezi la usanifu wa kina wa barabara ya Oldeani Junction - Matala - Mwanuzi - Kolandoto. Barabara hii ndiyo barabara ya kuunga Mkoa wa Arusha na Mkoa wa Simiyu hadi Mwanza. Hii barabara ni fupi sana na ujenzi wake hautasumbua maana inapita katika maeneo mepesi kufikika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii inapita katika maeneo yenye vitunguu, mpunga, mahindi na pia eneo muhimu sana kwa ufugaji. Barabara hii ni rafiki wa mazingira na ndiyo maana inaitwa Serengeti Southern By pass.
Naomba Serikali itafute fedha za ujenzi haraka sana ili kutimiza sera ya kuunga mikoa, lakini pia ahadi ya viongozi wa juu wa Awamu ya Nne na ya Tano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia barabara ya Karatu - Mbulu - Haydom - Matala iliyoingia mwaka huu kwenye hatua ya upembuzi yakinifu na baadaye usanifu wa kina. Ni imani yangu kuwa baada tu ya maongezi hayo kazi ya ujenzi itaanza mara moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tunaomba barabara ya Manyara - Kitete - Losetele ipandishwe hadhi kutoka barabara ya Halmashauri kwenda kuwa barabara ya Mkoa; barabara hii inaunganisha Wilaya ya Karatu na Wilaya ya Monduli. Ni barabara inayopitisha mazao mengi kuelekea soko lililoko Arusha. Nashukuru.