Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Magdalena Hamis Sakaya

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Kaliua

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwa nini Serikali inaruhusu Shirika la ndege la FastJet hutoa huduma kwa kuwaibia wateja/abiria kwa kiasi kikubwa hivyo? Ndani ya ndege, maji nusu lita wanauza shilingi 3,000 wakati wanachukua kiwandani kwa bei ya jumla, nusu lita shilingi 300.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukikata tiketi ya go and return, ukipata dharura ukashindwa kusafiri tarehe ya tiketi hata ukiwapa taarifa saa 24 kabla ya safari, hela yako inakufa na tiketi imekufa. Begi hata kama lina nguo za mtoto, likizidi kilo moja unalipishwa kuanzia shilingi 100,000 mpaka shilingi 200,000; huu ni wizi mtupu wakati Serikali ipo na inaona. Tunaomba majibu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mawasiliano ya simu; katika Wilaya ya Kaliua kuna maeneo ambayo hakuna minara ya simu na hivyo, wananchi hupata shida kubwa ya mawasiliano. Kata ya Igwisi, kijiji cha Upele na vitongoji vyake vyote, kata ya Tugimlole mpaka kijiji cha Igombe. Kata ya Ulambi, Sigaga mpaka vijiji vya Usinga na Kotonko. Kata ya Igagala mpaka vijiji vya Wachawasome na vitongoji vya Kona Nne, Ukumbanija, Ufulaga. Kata ya Ugunga mpaka vijiji vya Mpilipili na vitongoji vya Kanyanya. Maeneo yote ya Kaliua kuanzia pale mjini mtandao wa Tigo ni wa shida sana.