Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Ally Seif Ungando

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. ALLY S. UNGANDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nami kuchangia kwa maandishi katika mada hii ya miundombinu kwani ni muhimu sana katika Jimbo langu la Kibiti.
Katika Jimbo langu la Kibiti kuna changamoto kubwa katika miundombinu, hasa maeneo ya Delta hakuna mawasiliano kabisa; Mfisini, Kiomboni, Sanenga, Salale, Mbwera, Mbuchi, Kingongo, Mberambe, Msala, Mchinga, Maparoni, Mbuchi, Pombwe, Kechuru; katika maeneo haya mazingira si rafiki kwa mawasiliano na barabara zao pamoja na magati ya maeneo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ujenzi wa gati la Nyamisati, napenda kuishauri Serikali yangu sikivu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kuanza haraka sana ujenzi wa gati la Nyamisati, kwani gati hili ni muhimu sana, litahudumia Wilaya mbili za Mafia na Kibiti kwa kuhudumia wananchi wengi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Bungu – Nyamisati; barabara hii nayo ni muhimu sana kwani inatumiwa na wananchi wa Mafia na wa Kibiti, tena barabara hii ijengwe kwa lami. Kibiti – Ruaruke – Nyamisati; barabara hii nayo iboreshwe kwa kiwango cha changarawe kwani ina mchango mkubwa wa kukuza uchumi wa wakulima. Kufungua barabara mpya kutoka Kipoka – Maparoni – Msala, jamani hii ni barabara muhimu sana kufunguliwa kwani italeta mchango mkubwa sana wa uzalishaji mali katika uchumi wetu wa Taifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kibiti – Makima – Kisarawe – Chole. Hii nayo ni barabara muhimu ya Chole Kati kuja Dar es Salaam. Kinyanya – Magogo – Matatu – Msoro, nayo ni barabara ya muhimu sana kwa kuja katika Makao Makuu ya Kata ya Mtawanya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la minara; nashauri Serikali yangu sikivu ipelekwe maeneo husika ili nayo iwafaidishe wananchi wa sehemu husika kwa kuboresha huduma za jamii kama kujenga shule, zahanati, kuchimba visima, barabara na kadhalika. Katika Jimbo langu la Kibiti kuna maeneo mengi ambayo hayana mawasiliano, kama maeneo ya delta na nchi kavu kama Mng‟aru, Kimbugi, Miwaga, Ngulakula, Rungungu, Mangwi, Nyamwimbe, Ruaruke.
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Kibiti – Mchukwi; barabara hii ni muhimu sana kwenda Hospitali ya Mission ya Mchukwi. Barabara hii iwekewe lami kwani hospitali hii inawahudumia watu wengi sana kutoka ndani na nje ya Wilaya yangu ya Kibiti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo ni muhimu sana, upewe kipaumbele katika bajeti hii. Bandari hii ikiisha itachangia mchango mkubwa katika Pato letu la Taifa, kupunguza msongamano wa foleni katika Jiji la Dar es Salaam na vijana wetu kuajiriwa kupitia bandari hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mapambano dhidi ya UKIMWI; kila mmoja anawajibika kuhakikisha anapambana na suala zima la UKIMWI. Wahakikishe kutoa elimu wakati wa ujenzi wa barabara ili watu wapime kwa hiari na watambulike kisha wapewe elimu ya ushauri nasaha.