Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi na hongera kwa Waziri, Profesa Mbarawa na Naibu Waziri wake na timu nzima ya Wizara. Mmeanza vizuri, endeleeni kwa kasi hiyo hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nina mambo machache kuhusu barabara ya Kidahwe - Kasulu kilometa 50, fedha shilingi bilioni 19.3. Kutoka Kidahwe hadi Kasulu Mjini ni kilometa 60; je, ina maana kilometa 10 zinazobakia zitajengwa lini? Ni vizuri barabara yote ya Kidahwe - Kasulu, kilometa 60, zikajengwa pamoja bila kuacha kiporo au kipande hicho; tafadhali Wizara angalieni jambo hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Kasulu – Kibondo – Kabingo na Kasulu – Manyovu, Mheshimiwa Waziri umesema itakuwa financed na ADB kama sehemu ya mkakati wa Sekretarieti ya EAC. Ni vizuri tukajua time frame ya ujenzi wa barabara hii, ni barabara ndefu, kilometa 2,258; tafadhali Wizara pamoja na Wizara ya Fedha muipe kipaumbele barabara hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kupandisha hadhi barabara za Mkoa wa Kigoma. Mheshimiwa Waziri, Mkoa wa Kigoma ni kati ya mikoa yenye mtandao mdogo kabisa wa barabara za mikoa (Regional Roads). Tafadhali, pandisha au toa idhini ya kupandishwa barabara zifuatazo kuwa barabara za mkoa:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Kasulu – Kabanga – Msambara – Mwaufa – Mganza hadi Herujuu; barabara ya Nkundutsi – Malamba – Muhunga – Herujuu; barabara ya Buhigwe – Muyama – Kasumo – Mwanga – Mganza – Herujuu. Barabara hizi zina sifa na kitakuwa kichocheo za kukuza uchumi na zina sifa zote stahili kupandishwa hadhi kuwa Regional Roads.