Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, nawapongeza Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mheshimiwa Mohammed Mchengerwa (Mb) pamoja na Naibu wake Mheshimiwa Paulina Gekul (Mb). Nawapongeza pia Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu, watumishi wote wa Wizara na wanasanaa na michezo wote.

Mheshimiwa Spika, nawapongeza timu ya wanawake Twiga Stars na kwa namna ya pekee nampongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa ya kujitoa kuhamasisha utalii na michezo ikiwemo kuwafadhili vijana wa Twiga Stars pamoja na kuwapatia viwanja kwa ajili ya maisha yao ya mbele. Napongeza pia kwa kuwaenzi waasisi wetu kupitia sherehe na makongamano mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, maombi yangu; kwanza Wilaya ya Nyasa katika kuimarisha michezo tumeamua kuanza kujenga uwanja wa michezo. Tunaomba support yenu ya hali na mali ikiwemo kusaidiwa nyasi za bandia na michango ya fedha kutoka kwa wadau mbalimbali na pili, tunaomba pia mtutembelee Nyasa ili kutuhamasisha.

Mheshimiwa Spika, nawasilisha.