Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, kwanza nawapongeza Wizara kwa maandalizi ya hotuba nzuri ya bajeti, Mawaziri wa Wizara hii wana bahati ya kuwa na watendaji wenye weledi, namfahamu Katibu Mkuu Dkt. Abbas toka tukiwa naye kwenye media, akiwa newsroom ya Business Times-Majira, kadhalika Ndugu Yakubu ambaye pia amekaa newsroom za kimataifa, Ndugu Singo Mkurugenzi wa Michezo ni mtu open minded, kwa hiyo Wizara ina kila sababu ya kuacha alama (legacy).

Mheshimiwa Spika, nawapongeza TFF kwa kuwezesha na kufanikisha ushiriki wa timu zetu za Taifa zote kuanzia za vijana, wanawake na wakubwa. Tunajua ni mzigo mkubwa sana, lakini wanajitahidi sana,

Ushauri wangu kwanza ni kuhusu kufungia fungia, nashauri pamoja na kuwa ni kanuni ambazo vilabu vimejitungia kwa kushiriki katika kuzitunga, TFF wasaidieni ili tuwe na adhabu mbadala, kumfungia mtu miaka mitano ndugu zangu put yourself in such a position!

Mheshimiwa Spika, tulipitisha sheria kwamba 5% ya zawadi ya mshindi iende kuimarisha michezo, nashauri fedha hii kwa kuanza tuutupie jicho mchezo wa riadha.

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye mchango wangu wa kuzungumza, tuepuke kuingilia uchaguzi wa TWF na hapa kwa nia njema nawashauri TFF, waacheni wanawake wachaguane kwa huru na haki, hakuna asiyejua kuwa TFF kwa ujanja ujanja walivuruga uchaguzi wa TWF, matokeo yake mpaka sasa TWF haina mwakilishi katika Kamati ya Utendaji ya TFF, hili suala tukilitizama katika jicho la jinsia, linaleta tafsri ambayo sio nzuri. Wizara kama kiongozi na msimamizi mkuu naishauri suala hili liishe, hakuna jambo ambalo linasemwa lisiwafikie familia ya michezo. Baadhi ya viongozi wa TFF kauli zao katika suala hili sio jema, tujitafakari.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.