Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa hotuba yake nzuri iliyogusa karibu sehemu nyingi, hasa katika ujenzi wa miundombinu ya barabara. Hata hivyo, nitapenda kupata ufafanuzi katika maeneo muhimu mawili kuhusu miundombinu ya barabara katika Jimbo langu la Muhambwe lililoko Wilaya ya Kibondo, Mkoa wa Kigoma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri katika hotuba yake ametaja kuwa kuna pesa imetengwa kwa ajili ya ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami (Nyakanazi – Kibondo, kilometa 50, shilingi 17,400,000); angalia katika kitabu ukurasa wa 227.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa kupata ufafanuzi ili kuondoa mkanganyiko pale Waziri anaposema Nyakazi - Kibondo, kilometa 50.
Wananchi hawaelewi kwani kipande hicho kinaishia Kabingo ambayo iko Wilaya ya Kakonko, Nyakanazi - Kibondo ni kilometa 91. Vilevile naomba commitment ya Waziri kuhusu hiyo pesa inayotegemewa kutoka ADB itapatikana lini na ujenzi utaanza lini kwa kipande kutoka Kabingo - Kakonko - Kibondo - Kasulu - Manyovu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri kwenye mapendekezo ya RCC iliyofanyika Februari, 2016 tulipendekeza baadhi ya barabara katika Majimbo ya Muhambwe, Kibondo, zipandishwe hadhi kutoka Wilaya kwenda Mkoa (Kitahama - Mabamba) na kutoka Mkoa kwenda Taifa (Kifura – Kichananga – Mabamba) kutokana na umuhimu kiuchumi na kiusalama kwa nchi yetu. Sijaona kwenye hotuba hii, naomba ziingiwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kutenga pesa kwa ajili ya barabara ya Kibondo – Mabamba, (Page 255(281). Kwenye hotuba ilisema itajengwa kwa kiwango cha lami (kilometa 45), nimeona imetengewa shilingi milioni 80; tafadhali angalia suala hili kwani nyumba zinaendelea kuwekewa alama za “X”.