Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

Hon. Salma Mohamed Mwassa

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

MHE. SALMA M. MWASA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Awali ya yote, napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha kuteuliwa kuwa Mbunge wa Mkoa wa Dar es Salaam. Aidha, napenda kuwapongeza Waheshimiwa Wabunge wote kwa kupewa ridhaa hii na wananchi pamoja na wewe Mheshimiwa Naibu Spika kuweza kuteuliwa kuwa Mbunge.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda nichangie hotuba ya Mheshimiwa Rais katika maeneo yafuatayo. Kwanza, napenda kuchangia katika eneo la elimu. Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli aliahidi kuboresha elimu katika maeneo mengi na kusema kwamba elimu ni bure. Labda kabla hatujafikia kwenye elimu bure, napenda kufafanua yafuatayo. Mheshimiwa Naibu Spika, kuna matatizo mengi juu ya mpango huu wa elimu bure.
Kwanza, miundombinu ni tatizo. Ni wazi idadi ya wanafunzi inaongezeka kwa kuwa elimu ni bure lakini haiendani na miundiombinu iliyopo katika shule zetu. Kwa mfano, katika Wilaya ya Kinondoni kuna jumla ya wanafunzi wa shule za msingi 152,000 na vyumba vya madarasa 1,500 hivyo tunapata wastani wa wanafunzi 98 kusoma darasa moja. Idadi hii ni kubwa sana na haiendani kabisa na udhahiri wa kauli hii kwamba elimu itaboreshwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni wazi kwamba upungufu wa madarasa katika Halmashauri ya Kinondoni ni jambo ambalo litadhoofisha suala hili la elimu. Halmashauri ya Kinondoni inahitaji vyumba vya madarasa 3,018 vilivyopo ni 1,656, pungufu ni 1,362. Inahitaji nyumba za
walimu 452 zilizopo ni 280 pungufu ni 172. Ofisi za walimu ni 222 zilizopo ni 104 pungufu ni 118. Vyoo vya walimu vinahitajika 452 vilivyopo ni 280 pungufu ni 172. Vyoo vya wanafunzi vinahitajika 6,338 vilivyopo ni 1,382 pungufu ni 4,956. Maktaba nazo ni tatizo, zinazohitajika ni 1,446 zilizopo ni 32 tu pungufu ni 114. Kwa hali hii, sasa elimu itakuwa bure kama kutakuwa na
mipango thabiti wa kuongeza miundombinu hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, namshauri Mheshimiwa Rais pamoja na kwamba elimu ni bure lakini aangalie tatizo la miundombinu kwani wanafunzi wengi wanarundikana kwenye darasa moja ambapo haitaleta ufanisi wa kutosha. Tukiangalia kwa mfano jinsia ya kike
inapata shida sana kutokana na upungufu wa vyoo. Tunajua matatizo mengi ya watoto wa kike kwani wanahitaji kutumia vyoo safi. Hivyo basi, tatizo la miundombinu liangaliwe ikiwemo vyoo, madarasa na maktaba.
Mheshimiwa Naibu Spika, nijikite tena kwenye elimu ya sekondari hasa katika Wilaya ya Kinondoni. Kwa mujibu wa taarifa ya makabidhiano ya Serikali ya Awamu ya Tano Wilaya ina matatizo makubwa. Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni ina shule za sekondari 137 tu kati ya
hizo sekondari 48 tu ndizo sekondari za Serikali na 16 ni za mijini na 32 ni za vijijini. Hivyo basi, kuna upungufu wa nyumba za walimu, walimu wengi wanakaa mijini na kufundisha vijijini hali inayosababisha adha kubwa kwa walimu hao kutoka mijini kwenda vijijini na kudhoofisha elimu katika eneo hili la sekondari. Walimu hawa wanaishi kwenye mazingira magumu mno naomba tatizo hili liangaliwe. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hii inadhihirishwa katika taarifa hiyo, kati ya mwaka 2011-2014, wanafunzi waliofanya mtihani walikuwa 34,000 lakini waliofanya vizuri ni 11,000 na waliofeli ni 22,000 ambao ni sawa na asilimia 63. Hivyo eneo hili liangaliwe tena katika kuboresha elimu ya watoto wetu ili tuweze kukidhi mahitaji yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, nawasilisha. (Makofi)