Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Spika, maeneo ya utalii katika Wilaya ya Newala nikianza na utalii; Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii naomba mtume tume ya wataalamu waje Jimbo la Newala Vijijini kuona maeneo mazuri ya utalii yaliyopo Jimbo la Newala Vijijini katika Kata ya Chilangala ambako kuna maporomoko mazuri sana ya utalii katika Mlima Miyuyu.

Aidha kwenye Jimbo la Newala Mjini lipo Shimo la Mungu eneo zuri kabisa la utalii. Tunaomba mje muwekeze katika Wilaya ya Newala kwenye masuala ya utalii.

Pia Wilaya ya Newala kuna kivutio kizuri sana cha utalii wa utamaduni wa Kimakonde kuanzia ngoma na vyakula. Katika Jimbo la Newala Vijijini katika Kata ya Mchemo huwa kuna maadhimisho ya siku ya utamaduni wa Kimakonde, tunaomba Wizara yako ituwezeshe kuimarisha sherehe hizo, pia mje mjionee siku hiyo maalum. Kama Wana-Newala tupo tayari kushirikiana nanyi katika kila hatua.

Mheshimiwa Spika, changamoto kati ya TFS na wananchi wa Kata ya Chilangala; naomba kuuwasilisha kwenu mgogoro unaofukuta kati ya wananchi wa Kata ya Chilangala na TFS ambapo mwezi Aprili mwananchi mmoja amefariki katika harakati zitokanazo na mgogoro wao kutotatuliwa hali iyoleta kadhia hiyo.