Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa fursa ya kuchangia kupitia njia hii ya mchango wa maandishi kwenye Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, mchango wangu utajikita kwenye maeneo mawili yanayoambatana pamoja na utalii wa tiba (medical tourism) na utalii wa kibiashara (business tourism).

Mheshimiwa Spika, maeneo haya mawili ya sekta ya utalii yanategemea sana jitihada kutoka kwenye sekta nyingine kama vile sekta za afya, sekta ya ujenzi, sekta ya ulinzi, na sekta ya biashara. Hivyo Wizara ni lazima iwe na mashirikiano na Wizara za Ujenzi, Afya, Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Mambo ya Nje, Ulinzi na Mambo ya Ndani. Lengo ni kuona jinsi gani mipaka inatumika kama fursa, badala ya kuichukulia kama zao la laana na uadui.

Mheshimiwa Spika, Serikali imeweka miundombinu ya Hospitali za Rufaa za Mikoa na Kanda kuwezesha utekelezaji wa utalii wa tiba (medical tourism), lakini pia nchi yetu ina mipaka, mkakati inayozalisha majirani ambao ni soko kubwa kuwezesha utekelezaji wa utalii wa biashara (business tourism). Mipaka inaleta wateja wa maeneo hayo mawili ya utalii wa tiba na utalii wa biashara.

Mheshimiwa Spika, nchi kama vile Malawi, Mauritius, Mozambique, Comoro, Seychelles, Zambia, Congo, Rwanda, Burundi, Somalia, Uganda, Sudan, Somalia na Kenya ni muhimu katika utekelezaji wa utalii wa biashara.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.