Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Amina Daud Hassan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. AMINA DAUD HASSAN: Mheshimiwa Spika, naomba kuchangia makadirio na mapato na matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

Mheshimiwa Spika, nampongeza Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya kwa Taifa letu kwa kutuletea utalii kupitia Royal Tour. Pia nampongeza Waziri na Naibu wake pamoja na watendaji wake wote kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Mheshimiwa Spika, tuzidi kuitangaza Tanzania kupitia watalii wanaokuja Zanzibar wanaokwenda Jozani kuna wanyama adimu kama kima punju vilevile kuna utalii wa kuzamia mbizi upo Paje na utalii wa culture na mila na desturi na utamaduni wetu. Mfano mapishi, ustaarabu wa mapokezi mazuri ya wageni pia tuishukuru Serikali kwa watalii wanakwenda kutembelea mikoa ya Tanzania Bara wanamalizia kuja Zanzibar ili kuweza kuona vivutio vizuri ambavyo vinapatikana Zanzibar kama hoteli iliyopo baharini Pemba, na hoteli mbalimbali kubwa.
Mheshimiwa Spika, ushirikishwaji wa private sector, tunamshukuru Bakhresa kwa kuleta meli zake ili kuweza kuwapatia na kuwasafirisha watalii kwa urahisi na kuweza kufika Tanzania Bara kwenda kuona Mlima Kilimanjaro, Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na kadhalika na kwenda visiwani bila ya shida yoyote.

Mheshimiwa Spika, natoa wito na kuishauri Serikali iweze kuiongezea bajeti Wizara hii ili iweze kuongeza miundombinu rafiki kwa watalii wetu ambao wanatarajiwa kuja kwa wingi sana. Kwa mfano, barabara, kuongeza hoteli ya nyota tano, kuongeza usafiri wa anga na baharini ili kuweza kumudu ongezeko la utalii, na hata watalii wanapokuja kwetu waone raha kama wapo nyumbani kwao, lakini vilevile nchi yetu itaimarika na kuongezeka kwa pato la Taifa.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.