Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Suleiman Haroub Suleiman

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. SULEIMAN HAROUB SULEIMAN: Mheshimiwa Spika, awali ya yote kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujaalia afya njema na amani.

Mheshimiwa Spika, naomba kuchukua fursa hii adhimu kumpongeza Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa uongozi wake uliotukuka kheri na baraka ziwe kwake.

Mheshimiwa Spika, aidha natoa pongezi kwa Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na watendaji wote wa Wizara hii wakiongozwa na Dkt. Francis.
Mheshimiwa Spika, binafsi ni Mjumbe wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii, nimejionea na kupata taarifa za utekelezaji wa Wizara katika kipindi cha Kamati hivyo basi nina ushauri tu kwa maslahi ya Taifa letu.

Kwanza, Wizara hii sio Wizara inayoshughulikia masuala ya Muungano wa Tanzania, lakini ushirikiano kati ya baadhi ya taasisi za SMZ na SMT zitasaidia kuengeza idadi ya watalii wa ndani na wakimataifa. Mfano, Mamlaka ya Hifadhi na Urithi wa Mji Mkongwe Zanzibar, Idara ya Mambo ya Kale, Idara ya Utamaduni na Sanaa, Mamlaka ya Mazingira na kadhalika, hivyo basi nashauri Wizara ya Maliasili na Utalii ishirikiane na Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale ya Zanzibar kwa lengo la kuongeza idadi na namba ya watalii.

Mheshimiwa Spika, pili, Wizara kuongeza kasi ya utangazaji wa vivutio sambamba na kubuni activities tofauti katika vivutio vyetu. Mfano, kuweka michezo ndani ya maeneo wanayozuru/sehemu za utalii. Hii itasaidia wageni kushawishika kuja mara kwa mara nchini.
Tatu, kuboresha miundombinu katika maeneo yanayotumika kwa wageni kutembelea, mfano barabara; nne kuboresha huduma ya mawasiliano katika hifadhi zetu. Kukosa mawasiliano ni changamoto kwa watalii kwani zipo sehemu bado mawasiliano ya simu hakuna.
Tano, kufikisha huduma za kifedha kwa baadhi ya maeneo yanayotumika kwa kazi za kitalii. Mfano ATM, WAKALA na kadhalika ili mtalii aweze kutumia akiwa ndani ya hifadhi kununua huduma tofauti na hii zaidi inawalenga watalii wa ndani; sita, kumaliza miradi yenye kuongeza idadi ya watalii lakini pia yenye kuongeza fursa za ujio wa watalii nchini, mfano, meli kwa ajili ya utalii wa majini, malango katika hifadhi zetu, Mradi wa REGROW, Mradi wa Nyuki na kadhalika.

Saba, kuitumia filamu ya Royal Tour katika matamasha ya kimataifa. kwani filamu ya royal tour imeitangaza sana nchi yetu; nane, Wizara kutumia historia na uasilia wa maeneo yanayotumika kwa shughuli za kitalii. mfano; Mikindani (biashara ya Utumwa), machifu na historia zao (Chifu Mkwawa Nyika wa Iringa) na kadhalika; tisa kuipa nguvu Idara ya Malikale na Makumbusho na kumi, kuboresha mahusiano mema na Mataifa tofauti.

Mheshimiwa Spika, kumi na moja, Wizara ifikirie kuweka kumbukumbu ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuipa nguvu ya kifedha na maarifa Wizara hii na wananchi wa Tanzania kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, hitimisho, nampongeza sana Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutusaidia na kuisaidia sekta ya utalii kifedha kwa kuamini kuwa sekta hii ina mchango mkubwa sana kuinua uchumi wa Tanzania. Ninawatakia kila la kheri katika kutimiza majukumu mliokabidhiwa na Mheshimiwa Rais. Mimi Mjumbe wa Kamati naunga mkono hoja asilimia mia. Ahsante sana.