Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Spika, napenda kuwashukuru na kuwapongeza Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Mheshimiwa Dkt. Philip Isdor Mpango, Makamu wa Rais wa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Mawaziri na viongozi wote wa Wizara ya Maliasili na Utalii, kwa uongozi wao na utendaji uliotukuka.

Mheshimiwa Spika, napenda pia kutumia fursa hii kukupongeza wewe binafsi, Naibu Spika na uongozi wote wa Bunge kwa uongozi wenu mahiri na wenye ubunifu wa hali ya juu katika kuongoza mhimili wa Bunge.

Mheshimiwa Spika, napenda kumpongeza Waziri wa Maliasili na Utalii, kwa hotuba nzuri iliojaa ubunifu mkubwa na imedhihirisha utayari wa Serikali katika utekelezaji wa ustawi wa jamii na maendelo endelevu, na hii ni mojawapo ya nguzo kuu katika utayari wetu wa ushindani wa kimataifa (national competitiveness). Bajeti hii inaenda sambamba na Dhima ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/22 – 2025/26 ambayo ni Kujenga Uchumi Shindani na Viwanda kwa Maendeleo ya Watu.

Mheshimiwa Spika, pamoja na programu ya kutunza maliasili zetu, Serikali iweke usimamizi wa msitu hasa ya asili ambayo inaendelea kupotea kwa matumizi ya nishati. Katika kupangilia matumizi mazuri ya ardhi, ihusishe Wizara zote zinazosimamia Maliasili, Ardhi, Kilimo, Wizara za Maji na pia Wizara inayosimamia Mazingira. Kwa vile binadamu tunaongezeka ni muhimu kuhakikisha ulinzi kwa kuhifadhi mazingira yetu na kuwepo msukumo zaidi kwenye kuboresha mazingiara.

Mheshimiwa Spika, pamoja na hatua zinazochukuliwa na Serikali kurejesha mahusiano mazuri kati ya TANAPA (Hifadhi ya Kitulo) na wananchi wa Kata za Ilungu, Igoma, Ulenje na Inyala, bado suluhu haijapatikana. Kuna mgogoro wa miaka mingi wa mpaka kati ya TFS na wananchi wa Kijiji cha Mwashoma. Pia kuna mgogoro wa TANAPA (Hifadhi ya Kitulo) na wananchi wa Kijiji cha Kikondo ambao eneo lao lilichukuliwa na TANAPA bila kulipa fidia. Pamoja na changamoto hiyo ya GN za Hifadhi ya Kitulo, pia kuna utata wa mpaka wa Wilaya ya Mbeya na Wilaya ya Makete na inahitajika Wizara ya Ardhi kupitia upya mipaka na kurekebisha. Kutokana na mgogoro huu kuchukua muda mrefu na kusabisha uvunjifu wa amani, kuna ahadi ya mwaka 2015 alitoa Mheshimiwa Hayati Magufuli na kumwelekeza Waziri wa Ardhi na pia Waziri wa Maliasili na Utalii wa wakati huo kupitia upya mipaka, ili wananchi wa Kata za Ilungu na Inyala, hususani Kijiji cha Kikondo na Mwashoma waachiwe maeneo yao.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.