Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. ABEID M. IGHONDO: Mheshimiwa Spika, naomba kutoa mchango wangu wa maandishi katika Wizara hii muhimu ya Maliasili na Utalii.
Mheshimiwa Spika, nawapongeza mawaziri wa wizara hii kwa kazi nzuri wanayoifanya na zaidi nampongeza Mheshimiwa Rais kwa kuwa mstari wa mbele kuitangaza nchi yetu na vivutio tulivyonavyo hususan kupitia Royal Tour.

Mheshimiwa Spika, katika jimbo langu kuna msitu wa Mgori ambao unamilikiwa na wananchi kupitia Serikali za Vijiji na Halmashauri ya Wilaya ya Singida, hata hivyo wananchi hawa wapo tayari kuukabidhi msitu huu kwa Wizara ili uwe ni msitu wa Hifadhi ya Taifa ambapo hatua kadhaa zimeshanyika kukamilisha mchakato huo.

Ningependa wakati Waziri anafanya majumuisho aniambie ni hatua gani iliyofikiwa maana ni muda sasa tangu jambo hili limeanza kufanyiwa kazi. Ningependa kuona jambo hili linafikia mwisho ili msitu huu uweze kulinufaisha Taifa letu na pia wananchi wetu waweze kunufaika ipasavyo.

Mheshimiwa Spika, vilevile ningependa kuishauri Wizara kuvitangaza vivutio vyetu ipasavyo na kuiboresha safari Channel TV inayotumika kutangaza vivutio vyetu. Ninashauri wawepo watangazaji bobezi katika channel hiyo, pia Balozi zetu zitumike ipasavyo kutangaza vivutio vyetu na kuhamasisha watalii wengi kuja nchini ili nchi yetu ipate watalii wengi.

Mheshimiwa Spika, namalizia kwa kusisitiza Mheshimiwa Waziri anipatie mrejesho kuhusu umiliki wa msitu wa Mgori mchakato wa Serikali kuuchukua mmefikia wapi? Kwa nini unachukua muda mrefu namna hii?

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja na naomba kuwasilisha.