Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Emmanuel Lekishon Shangai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI: Mheshimiwa Spika, naomba kutoa mchango wa maandishi kufuatia kuwasilishwa kwa bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

Mheshimiwa Spika, ifuatayo ni mchango kwa Wizara hii; kwanza ili kuboresha utalii na kuvutia watalii wengi nchini Wizara haina budi kushirikiana na Wizara nyingine kwa ajili ya kuboresha miundombinu mbalimbali ya barabara hasa barabara ya kutoka Loduare mpaka Nabi Gate kwani ni barabara muhimu sana kwa watalii wanaotembelea Hifadhi ya Ngorongoro na Serengeti na barabara ya lami kutoka Mto wa Mbu mpaka Loliondo kwani nayo ni muhimu kwa watalii kufika Oldonyo Lengai.

Mheshimiwa Spika, Wizara ipitie na kufanyia kazi maoni ya wananchi wa Tarafa ya Ngorongoro, Sale na Loliondo kwani ndiyo mwarobaini wa changamoto za muda mrefu za maeneo hayo. Ni muhimu sana Serikali ione kuwa eneo la pori tengefu la Loliondo ni ardhi ya vijiji, hivyo vijiji husika ziruhusiwe kutumia ardhi yao bila usumbufu na wananchi waondokane na mgogoro wa ardhi iliyodumu kwa miaka 31 sasa, kimsingi mgogoro huu umewarudisha wananchi nyuma kiuchumi na wengine kupoteza maisha pamoja na mali zao.

Mheshimiwa Spika, Wizara itafakari upya namna ya kufanya kazi na Baraza la Wafugaji ili kurejesha mahusiano na wananchi wanaoishi kwenye eneo la Hifadhi ya Ngorongoro, pamoja na kutekeleza jukumu lake la kuwapatia wananchi wenyeji maendeleo kama ilivyo kwenye sheria ilyoanzisha eneo hilo bila kuwawekea vikwazo vya kimaendeleo kama ilivyo sasa.

Pia Wizara itekeleze MoU iliyoingiwa kati ya Wizara, Baraza la Wafugaji, NCAA na Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro na kuwaajiri watumishi wa Baraza la Wafugaji.

Mheshimiwa Spika, mwisho ni kuhusu kuboresha huduma za waongoza watalii na quality za magazine.