Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Balozi Dkt. Pindi Chana, Mbunge na Waziri wa Maliasili na Utalii pamoja na Naibu wake Mheshimiwa Mary Masanja, Mbunge. Vilevile nimpongeze Dkt. Francis - Katibu Mkuu pamoja na Naibu Katibu Mkuu Ndugu Mkome.

Mheshimiwa Spika, kwa namna ya pekee nampongeza Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan - Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuhamasisha na kuutangaza utalii wetu. Nasi Wilaya ya Nyasa tunamuunga mkono.

Mheshimiwa Spika, maombi, kwanza kumaliza mgogoro wa Lipalamba na wanakijiji wa Kijiji cha Mseto; kusaidia kutengeneza barabara zinazopita kwenye hifadhi ya Lipalamba ambazo zinahitaji kifusi kutoka mbali; tunaomba shilingi 5,000,000 kwa ajili ya kukamilisha zahanati ya kijiji cha Mipotopoto kinachopakana na Hifadhi ya Lipalamba na huo mkakati wa utalii kwenye maziwa makuu ikiwemo Nyasa umetajwa kwa kifupi sana. Naomba ufafanuzi ni kitu gani kitafanyika?

Mheshimiwa Spika, niliomba kujenga hosteli ndogo kwenye hifadhi hiyo ili kuanzisha utalii wa eneo hilo. Hadi leo sikujibiwa; je, Wizara yenu haina utamaduni wa kujibu barua?

Mheshimiwa Spika, nawasilisha.