Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nishukuru na mimi kunipa nafasi hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nipongeze sana Wizara hii, watendaji wote na Waziri na Naibu Waziri, wamefanya kazi nzuri na bajeti hii ina muelekeo mzuri; wapate fedha, sisi tunasubiri maendeleo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mtu mmoja alikuwa anachangia jana hapa, anasema daraja la Kigamboni halina faida, hivi kweli halina faida daraja la Kigamboni, kweli? Ila amesema amekwenda mara nane, mara ngapi, anakwenda na kurudi, si ndio faida yenyewe. Kama daraja halipo angekwendaje? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Awamu ya Tano ni kwa ajili ya watu wa chini. Na watu wa chini kule, hivi tunakwenda kuwaambia leo mambo hayo watu wa Kigamboni kweli? Eeh, wanatembea kwa mguu, si ndio wana faidi daraja hili. Songa mbele Waziri, usirudi nyuma. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, watu wanazungumzia habari ya kuuza zile nyumba. Nyumba ziliuzwa Waziri Mkuu alikuwa Mheshimiwa Sumaye. Mheshimiwa Sumaye ndiye aliesimamia mambo hayo, ndiye alieuza zile nyumba, lakini na nyumba zile na nyumba…
MHE. DEO K. SANGA: …mnanijua, wee!
Mheshimiwa Mwenyekiti, na nyumba zile…
Mheshimiwa Mwenyekiti, na nyumba zile walionunua ni Watanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ni Mheshimiwa Sumaye, si athibitishe!
Mheshimiwa Mwenyekiti, walinunua nyumba zile ni Watanzania, ndio walionunua zile nyumba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuombe Waziri mwenye dhamana, pale mjini…
MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuombe sana Waziri katika bajeti aone namna ya kutafuta fedha hata kilometa moja na nusu Makambako Mjini. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe, katika kupandisha daraja barabara za Halmashauri kwenda TANROADS, kuna barabara ya kutoka Makambako - Kifumbe, kutoka Usetule kwenda Kitandililo, tafadhali sana. Lakini vinginevyo Rais wa Awamu ya Tano…
MWENYEKITI: Ahsante! Ahsante sana.