Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipatia fursa hii. Kwanza kwa niaba ya wanawake wote Tanzania, Afrika na dunia nichukue fursa hii kumpongeza sana Fatma Samba Diouf kwa kuwa Katibu Mkuu wa FIFA kwa hiyo, nampongeza sana. Hii ni hatua kubwa sana kwa Waheshimiwa wanawake duniani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa haraka tu naomba niseme mambo machache; la kwanza kuhusiana na ferry ya Dar es Salaam. Mwaka jana Mheshimiwa Waziri alituambia kwamba ile ferry ilinunuliwa kwa shilingi bilioni 7.9. Nilikuwa naomba kujua leo hii ferry hiyo iko wapi? Kwa sababu, taarifa nilizonazo hiyo ferry sasa hivi haipo kazini! Nilikuwa naomba kujua iko wapi? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili ni suala la bajeti. Nilikuwa naomba Waziri anapokuja kutoa maelezo hapo anapo-windup atuambie inawezekanaje, tulipitisha bajeti ya Wizara hii nyeti sana kwa nchi yetu kwa shilingi bilioni 191 fedha za ndani kutoka Mfuko Mkuu, lakini mpaka Aprili 30, wametumia shilingi bilioni 607 zaidi ya asilimia 68 Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa naomba maelezo ya kina inawezekanaje Wizara hii ipate fedha hizo na imezipataje wakati tuna matatizo makubwa kwenye Wizara nyingi ambazo hata asilimia 50 hawajafika? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine nililokuwa naomba kulichangia ni suala zima za nyumba za Serikali, limeongelewa sana. Nilikuwa naomba kujua, lile Azimio la mwaka 2008 kutoka kwenye maelezo binafsi ya Mheshimiwa Kimario mpaka leo limefikia wapi? Na je, mna mpango gani wa kuendeleza nyumba hizo au kuzirejesha, ili tujue wahusika? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa naomba nizungumzie barabara ya Kinondoni, kutoka Mwenge mpaka Morocco. Nimefuatilia vitabu vya bajeti kuanzia mwaka 2013 mpaka leo, fedha ambazo zimeshatolewa ni shilingi bilioni 126, lakini barabara ile bado. Sasa nilikuwa naomba ilikuwa ni kuanzia Morocco mpaka Tegeta, lakini kwa awamu mbili; nilitaka kujua hizi fedha zimefika wapi kwa sababu mpaka majuzi hapa tulisikia Mheshimiwa Rais akisema kwamba anatoa zile fedha zilizokuwa za sherehe za Uhuru kwenda kujenga hii barabara.
Sasa nilikuwa nataka tu kupata maelezo, hizi fedha ambazo zimeshatolewa kuanzia mwaka 2013 mpaka leo ziko wapi? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho…
MWENYEKITI: Ahsante.