Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Asya Mwadini Mohammed

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. ASYA MWADINI MOHAMMED: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuweza kunipa nafasi nami niweze kuchangia hotuba hii ya Wizara ya Maliasili na Utalii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukisoma Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa Awamu ya Tatu, unasema kwamba ifikapo 2025/2026 tunatarajia kupata wageni wapatao milioni tano.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa tuna wageni takribani bilioni 1.5 kwa hiyo milioni moja na nusu maana yake tunatarajia kuwa na target ya wageni wageni 3,500 idadi hii siyo kubwa na wala siyo ndogo kama tutafanyakazi vizuri katika sekta hii ya utalii tuna uwezo wa kuifikia hata ifike mwaka huu ama ni mwakani.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimekuwa mdau mkubwa sana katika sekta hii ya utalii na nimekuwa nikichangia mara nyingi kuhusiana na utafutaji wa masoko ya kiutalii. Niipongeze kabisa kwa moyo wangu wa dhati programu maalum ambayo imeanzishwa ya Royal Tour ambayo imekuja kwa maslahi mapana ya kutangaza utalii wetu, lakini vilevile nje tu na kutangaza kwa ajili ya kuleta wageni nchini imeamua na kujikita zaidi kuonesha mambo mengi ambayo yanapatikana kiuchumi ndani ya Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia ile movie ya Royal Tour utakuta kuna masuala mazima ya bandari, bahari, madini na vitu vingine kwa hiyo wawekezaji wanapaswa waje na watakuja kutokana na ile filamu ambayo wameiona na vitu ambavyo vimo ndani ya filamu. Lakini ni kweli tumepanga na filamu ni nzuri na ina jambo jema lakini kama Wizara nilitaka tu nijue wao wana mpango gani na wamejiandaa vipi katika utekelezaji wa programu hii? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu nazungumza haya nilikuwa nafanya mawasiliano na watu wa tour operators wa Zanzibar na wamesema wameipokea vizuri na filamu imeanza kuleta impact mpaka juzi wakati naongea wanasema kama asilimia ya hoteli 50 tayari zimekuwa booked. Lakini tunavyokwenda kutafuta wawekezaji tunahitaji kuleta wageni ndani ya Taifa letu ni lazima tuangalie miundombinu ambayo imetuzunguka. Je, ni rafiki na hawa wageni ambao wanakuja? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sekta hii ya utalii ni mtambuka na haitegemei tu kwamba waweze kufanyakazi peke yao lakini kuna wadau mbalimbali ni lazima wawashirikishe ili waweze kuwa wanatatua changamoto mbalimbali. Umekuwa shahidi kwenye Bunge lako zinapokuja changamoto za maji, umeme, miundombinu ya barabara Wabunge wengi huwa wanasimama kuzijadili hoja hizi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo tunaona kwenye maeneo haya bado yanahitaji kufanyiwa kazi ya ziada kama tumeamua kuleta wawekezaji Wizara hizi ni lazima zishirikiane na Wizara ya Maliasili waweze kusaidiana kwa pamoja ili waweze kuleta maendeleo mapana na tuweze kuingiza pato. Barabara nyingi za kwenda kwenye hifadhi na vivutio vingine zimechakaa na ni mbovu, lakini halikadhalika kuna maeneo hata umeme hakuna yaani kunatumia solar na vitu vingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, hili jambo maana yake tulipotangaza tunatarajia kupokea na kama tunapokea lazima tuwe tumejiandaa, nje na hayo nisikitike pia kwa mfano changamoto ya watu wa Uhamiaji kuhusiana na kuwapokea wageni wetu maana yake tunasema reception ndiyo ina matter. Sasa mgeni ndiyo maana kuna Mbunge hapa amechangia amesema wageni wakija huwa hawarudi, lakini mapokezi ambayo yanaanza mwanzo huwa hayana picha nzuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano ukienda kwenye destination ya Zanzibar nachukulia mfano nyumbani, pale bandarini ukifika wageni ambao wanatoka safari pamoja na abiria wanachanganywa pamoja na wakifika pale Uhamiaji labda unaweza ukawakuta askari wapo wawili au watatu na kuna kundi la wageni na wanapofika pale yaani wageni wamening’inia kama madagaa yametandikwa kwenye mkeka yanataka kuanikwa. (Makofi)

Kwa hiyo, yaani askari anamuita mgeni njoo, wewe ni raia wa wapi, mpaka amsikie mgani anazungumza yaani nimeshuhudia mwenyewe, kiukweli nimesikitika sana. Sasa leo tuna wageni wachache tunakwenda kutangaza filamu na tumeanza kuitangaza kuna wageni watakuja kundi, makundi kwa makundi na nchi tofauti kama tunahitaji kweli kukuza utalii wetu lazima maeneo haya yakafanyiwe kazi za kimkakati. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, labda nishauri kwenye hii programu ya Royal Tour, kwanza kabisa kwa sababu Royal Tour imezungumza itakuja na phase ya pili na phase ya tatu, phase ya pili wajitahidi sana kushirikisha sekta binafsi ambao ndiyo wadau wakubwa wanaofanyakazi katika masuala mazima ya utalii. Lakini la pili washirikishe wazawa kama ni royal basi hata tuje na jina ambalo tunaweza tukasema local tour ambao wazawa wajue umuhimu wa kushiriki kwenye utalii na isifike hatua tukawa siku zote tunawategemea wageni kutoka nje ya nchi ndiyo ambao waweze kutuingizia pato. Sasa tuwaingize na wazawa ili tuweze kutengeneza picha na tafsiri pana ya kuweza kukuza utalii wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini suala lingine ni la uwekezaji, tuendelee kuhamasisha wawekezaji Mheshimiwa Waziri aliposimama hapa kwenye hotuba yake alisema kuna wawekezaji 30 tayari wameanza kutembelea Tanzania, kwa hiyo, kuna haja kuweka mazingira rafiki, tuache kuwawekea vikwazo ambavyo havina tija ili tuweze kuwasaidia waweze kuwekeza katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile hii filamu ya Royal Tour imeandaliwa na wenzetu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo lakini kwa kuwa kuna Bodi ya Utalii ambayo kila siku kazi yao kukaa chini kutengeneza mipango mikakati ya kuweza kutangaza Tanzania hii ni kama hawajakabidhiwa. Niiombe Wizara ya sanaa wawakabidhi Wizara ya Maliasili kupitia Bodi ya Utalii ili waweze kwenda kufanyakazi vizuri na iweze kuwa ni nyenzo kama nyenzo zao nyingine waweze kuwa wanaitumia katika kazi zao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niende kwenye hifadhi zetu za Taifa, ndani ya Taifa letu tuna hifadhi 22 ambazo kwa sasa ambazo zimetangazwa, lakini ufanisi siyo wa kuridhisha na hifadhi ambazo zinafanya vizuri yaani zinaweza zikawa labda ni tano mpaka labda kuelekea 10, tano na siku zote ndiyo tunaisikia Serengeti ndiyo inafanya vizuri na imekuwa migogoro mingi, kila siku ziamkapo watu wanalalamika tembo, tembo, tembo, mazao yanapotea askari wanapigana na raia, raia wanapigana na askari hili jambo halileti afya na wala siyo sifa kwa Taifa na tuna uwezo wa kuliondoa kama tutashirikiana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nchi zozote duniani zilizoendelea wamewakaribisha vizuri wawekezaji wa sekta binafsi na hizi hifadhi 22 kwa Serikali bado ni mzigo mkubwa kwa hiyo kuna haja kabisa...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)

MHE. ASYA MWADINI MOHAMMED: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi.