Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Martha Nehemia Gwau

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. MARTHA N. GWAU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushuru sana kwa nafasi hii uliyonipa na mimi ya kuchangia katika Wizara hii muhimu sana ya Maliasili na Utalii.

Mheshimiwa Naibu Spika, kipekee naomba nipongeze Wizara, nimpongeze Mheshimiwa Waziri, Mheshimiwa Naibu Waziri lakini na wataalam wote katika Wizara hii kwa ajili ya jitahada zao wanazochukua kuhakikisha kwamba suala zima la utalii nchini kwetu linapewa kipaumbele, lakini pia kwa namna moja au nyingine wanajitahidi kutangaza na kuvutia watalii kuja wengi Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, tuna vivutio vingi sana Tanzania ambavyo tumebarikiwa na Mungu, tuna Serengeti, Ngorongoro, Mlima Kilimanjaro na vingine vingi ambavyo siwezi kuvitaja kwa sababu ya muda, lakini tunavyo vivutio vingi ambavyo tumepewa na Mungu ila ni swali la kujiuliza ni kwa nini hatuna watalii wengi kama nchi nyingine pamoja na kuwa tuna vivutio vingi tulivyonavyo. Kwa hiyo, mimi nikaja na mambo mawili/matatu ambayo najua au nahisi yanasababisha tusipate watalii wengi, lakini pia yanasababisha hatujajitangaza vya kutosha.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kipekee naomba nichukue nafasi hii kwa unyenyekevu mkubwa nimpongeze Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa video yake ile ya Royal Tour ambayo kwa kweli imeenda kuwa ni suluhisho katika Wizara hii ya utalii, lakini pia katika uchumi wa nchi yetu. Najua Mheshimiwa Rais alivua Urais akavaa uzalendo, uzalendo ndiyo uliotawala hatimaye akaamua kuwa kipaumbele na kutangaza utalii wa nchi yetu. Kwa hiyo, kwa unyenyekevu mkubwa naomba nimpongeze sana na naomba nimwambie kwamba hii mifano ni ya kuigwa kwa sisi wengine na kwa watumishi wote. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi inaeleza ifikapo mwaka 2025 tuwe na watalii milioni tano lakini mpaka sasa tuna takribani watalii 1,500,000 na tuna miaka mitatu kufikia Ilani yetu ya uchaguzi. Kwa hiyo, mimi naamini kwamba tukiweka njia Madhubuti na tukiwa na mikakati maalum tutafikia hii idadi ya watu milioni tano kama ilivyoandikwa kwenye ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Royal Tour ya mama imeleta mafanikio makubwa sana nchini kwetu na itaendelea kuleta, mojawapo ni kutangaza vivutio vilivyopo, lakini pia kuwasadia wawekezaji, kusaidia pato la Serikali, lakini kusaidia jamii kwa ujumla kama vile ajira nakadhalika. Kwa hiyo, jukumu langu kumpongeza mama lakini pia ni jukumu letu kumuunga mkono na sisi kuja vitu mbadala ambavyo vitasaidia kuunga juhudi zake mkono. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, fursa za uwekezaji pia zimefunguliwa kutokana na Royal Tour, ni kweli usiopingika wawekezaji watakuwa wameona fursa zilizopo Tanzania na angle gani waje wawekeze kwa kutumia Royal Tour ya Mama. Kwa hiyo kwa hayo tu machache mama aliyotufungulia sasa ni jukumu letu la kubeba ule uzalendo wa mama na sisi kama Wabunge kuishauri Serikali, lakini pia na Wizara kuchukua yale maono ya mama na kuyaweka kwenye uhalisia ili tuweze kusonga mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nitajikita kwenye ushauri kwa Serikali kwa mambo mawili; ushauri wa kwanza ni njia za kisasa za utangazaji wa utalii, lakini wa pili utakuwa ni chombo cha ku-regulate standards na watoa huduma kwa ujumla. (Makofi)

Suala la kwanza, sasa hivi dunia iko kiganjani watu wanaita hivyo, kwa hiyo ni jukumu la Wizara au ni jukumu letu sisi sote ni kuhakikisha ni njia gani tunatangaza utalii na njia gani zinawafikia walengwa hasa tunaotaka kuwatangazia.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara imekuwa ikijitahidi kwa namna mbalimbali kwenda labda kwenye makongamano mbalimbali, lakini labda kutoa brochures tofauti tofauti, ila kwa dunia ya sasa hivi lazima tujiulize je, ni kweli hizi njia zinafanya kazi? Kwa sababu ni wangapi wanaosoma hizo brochures na hata kama Wizara wakienda kwenye maonesho wana banda la Tanzania labda vivutio vya Tanzania; je, ni kweli hilo banda linatembelewa na watu wengi? Kwa hiyo, utakuta hawapati idadi ya watu wa kutosha, lakini tukienda digital marketing inawafikia watu kwa haraka na kwa muda mfupi pasipo kutumia gharama kubwa sana kama sasa kusafiri sehemu mbalimbali.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimefanya utafiti mdogo sana kwenye nchi jirani za Afrika, lakini na nchi za wenzetu zilizoendelea. Nimeona juzi juzi tu hapa siyo muda mrefu Kenya imeingia Mkataba na mtandao wa TikTok, TikTok ni mtandao wa vijana siyo vijana na watu wengi wanatumia kwa ajili ya ku-post vitu mbalimbali. Wametengeneza short videos ambazo zinaonesha utalii wao na hii yote ni njia ya ku-recover kutoka kwenye COVID-19 ambapo sekta yetu ya utalii iliyumba sana. Kwa hiyo, kama sekta iliyumba lazima tujifikirie ni namna gani mbadala za haraka haraka ambazo zitasababisha sisi tujitangaze kwa urahisi lakini tupate matokeo kwa muda mfupi.

Mheshimiwa Naibu Spika, digital marketing is the way forward kwa sababu hiyo ndiyo inakupa majibu ya haraka haraka. Hata kuna document moja ya World Bank wameandika digital platform na demand kwenye business ya utalii, hivi ni muhimu kwa sababu siku hizi watu wakiamka asubuhi anashika simu ya mkononi kwanza tofauti na zamani ilivyokuwa. Kwa hiyo, tukitumia digital platform ya kuwatangazia vivutio, tuwatangazie tunatoa vitu gani Tanzania wataweza kuja kuona kwa kutumia simu ya mikononi bila ya kuwa tumeenda kutangaza, tumeenda nchi hii na nchi hii. Kwa hiyo, mimi nashauri tujikite sana kwenye digital economy. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia kuna nchi jirani ambazo huwa wanafanya vizuri kwenye utalii kama Morocco, wao walikuja na mkakati maalum baada ya COVID wakaja na mkakati maalum wa utangazaji wa utalii unaitwa Aji and We Are Open. Huo mkakati ulikuwa unalenga kuleta watalii tena baada ya COVID kuwapa awareness kwamba sasa tumefungua utalii wetu karibuni. Kwa hiyo, na sisi Tanzania tuje na different programu mbalimbali japo tunayo hii moja ya mama yetu mpendwa ya Royal Tour, lakini tuongeze na zingine kuonyesha kwamba sasa tumeshafungua utalii na sasa tuko tayari kupokea wageni waje kwa wingi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kingine cha pili katika hiyo hiyo digital marketing tuna watu mbalimbali mashuhuri ambao wanafuatwa na watu mbalimbali na kwa wingi mkubwa wa mamilioni na wengine wana ma-followers wengi. Tukiainisha target market yetu kama tunataka nchi ya Urusi, tunataka wa Marekani, tunataka wa London, tunataka watu wapi, ni kiasi cha kutafuta mtu mashuhuri wa hiyo sehemu akaja kutangaza utalii. Aki-post kwenye platform zake sisi tunapata watalii, nakuhakikisha msanii aki-post au mtu mashuhuri hata ukiwa na viewers watu milioni tano, milioni 10 huwezi ukakosa watu milioni moja wa kuja kutembelea Tanzania. Kwa hiyo, ni wazo langu na rai yangu kwamba Serikali mtachukua hilo suala kwa ukubwa wake kama nchi za wenzetu walivyofanya na mpaka sasa namba yao ya utalii imeanza kuwa kubwa na kurejesha kutoka kwenye ile hali ilivyokuwa ya COVID-19.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala langu la pili lilikuwa ni chombo cha ku-regulate standards za watoa huduma wetu na niungane na mchangiaji aliyepita, shida nyingi Tanzania kwanza zile punctuality, standards za watoa huduma wetu bado haziridhishi. Tunakuwa tunawatoa huduma ambao moja whether hawana mafunzo ya kutosha, mbili hawana uzoefu wa kutosha au walimu wao wanaowafundisha hawana enough skills za kuwapa hawa wanafunzi waka-compete au wakawa competent kwenye maeneo yao ya kazi.

Sasa mimi nikiangalia mfano wanasheria wana chombo chao kile Law School lakini wa leseni zao, watu wa NBAA wanatoa CPA; je, kama sisi tumeamua kujikita kwenye utalii na kama utalii huu ni muhimu kwa nini utisije na chombo chetu cha ku-regulate hawa watoa huduma, simaanishi hoteli hiyo tayari ipo. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Ahsante Mheshimiwa Martha kwa mchango wako.

MHE. MARTHA N. GWAU: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru, naunga mkono hoja. (Makofi)