Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Juma Usonge Hamad

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chaani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. JUMA USONGE HAMAD: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana na mimi kunipatia fursa hii ya kuweza kusimama na kuweza kutoa mchango wangu kwenye Wizara hii ya Maliasili na Utalii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kipekee kwanza nikupongeze sana kwa umalidadi wako wa kusimama kwenye kiti, lakini pia nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri, dada yangu kwa kazi nzuri ambayo wanayoifanya lakini pia kwa kuaminiwa na Mheshimiwa Rais kuongoza Wizara hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia kipekee nimpongeze sana Mheshimiwa Rais Mama yetu Mama Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa ambayo anaifanya hususan kwenye filamu ambayo tayari ameizundua hivi karibuni ya Royal Tour ambayo imetuletea matokeo makubwa sana ambayo na faida kubwa sana kutuletea wageni katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, leo sisi ambao tayari tunatokea upande wa pili wa Zanzibar jana napiga simu naambiwa kuna wimbi kubwa na wageni ambao wanaingia Zanzibar, kumbe faida kubwa ambayo inapatikana kupitia Royal Tour haipo tu kwa Tanzania Bara bali ipo mpaka Zanzibar, kwa kweli tunampongeza sana mama. Hii imetengeneza fursa kubwa sana vijana wetu kule ambao tunaita beach boy pamoja na waongozaji wa kitalii kufurahia matunda ya nchi yao, lakini pia matunda haya yanatokana na mama yao Mama Samia Suluhu Hassan, kwa hilo nampongeza sana Mama Samia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini mbali na hilo sasa nijikite kwenye mchango wangu, mbali na sekta hii ya kiutalii ambayo ina umuhimu mkubwa sana kukuza uchumi wetu na maendeleo ya wananchi wetu moja kwa moja, lakini yapo maeneo ambayo bado hatujaangalia kiujumla. Ingawa Tanzania tumebarikiwa katika maeneo yasiyopungua zaidi ya saba ambayo ndio tumejikita zaidi kuleta watalii nchi kwetu likiwemo eneo la hifadhi ya wanyamapori, lakini kuna eneo la maporomoko ya maji, kuna eneo la milima, kuna maeneo ya misitu, mazingira na maliasili, kuna utamaduni, utalii wa mali ya kale, lakini pia kuna utalii wa fukwe. (Makofi)

Mimi nataka niishauri zaidi Wizara hii mbali na kuangalia na wanyamapori lakini kwenye eneo la fukwe bado hatujawekeza zaidi. Tathmini inaonesha nchini kwetu Tanzania tuna hekari zisizopungua 1,428 kandokando ya bahari pamoja na maziwa makuu, lakini bado hatujaangalia kwenye eneo hilo. Ukweli usiopingika watalii wengi ambao tayari wanakuja kutembelea nchini kwetu Tanzania pamoja na Afrika kiujumla wanapendelea zaidi kuangalia katika maeneo ya fukwe. Leo hii mgeni anapata likizo kwenye mwaka wa miezi 12 anapata likizo ya mwezi mmoja mtalii yule ukimuuliza anakwambia maeneo ambayo nitapendelea zaidi kwenda kutembelea ni eneo la fukwe na eneo la hifadhi ya wanyamapori. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye maeneo hayo tunafanya vizuri hususani kwenye eneo la wanyamapori, lakini kwenye eneo la fukwe hasa bado hatujawekeza zaidi. Rai yangu kwa Serikali tuangalie namna gani tunaweka mpango mkakati either wa muda wa miaka mitano, either miaka kumi kwenye eneo hili la fukwe tunawekeza zaidi, inawezekana eneo la fukwe maeneo yale yanaonekana very expensive kwa wawekezaji kununua, lakini ninaishauri Serikali tuanzishe mfumo wa PPP (Private Public Partnership) hiii itatusaidia sana kama Serikali, akija mwekezaji kama Serikali inatoa asilimia 50 na asilimia 50 anatoa mwekezaji. Hii itasaidia kujenga mahotel makubwa pembezoni mwa fukwe, lakini sio fukwe tu za bahari tunayo maziwa makuu, mito na maeneo mengine mbalimbali hii itavutia sana kuleta wawekezaji na ndiyo tathmini ambayo inaonesha duniani kote huko watalii wengi ambao wanakuja wanaangali huko katika maeneo ya fukwe. Kwa hiyo, naamni tukifanya hivyo vizuri zaidi tunaenda kuongeza idadi kubwa sana ya watalii katika nchi yetu kila mwaka zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini mbali na hilo pia kuna eneo lingine ambalo kwenye suala la chakula bado hatujawekeza vizuri zaidi. Watalii wengi ambao tayari wanakuja nchini tunawalazimisha kuwalisha vyakula ambavyo havieleweki. Lakini miongoni mwa vitu ambavyo watalii wengi wanaokuja nchini kwetu wanavutiwa na chakula wengi wao na ndiyo maana ukifanya tathmini watalii wengi, mtalii akija mwaka huu mwakani ni nadra sana kurudi. Lakini bado hatujaangalia maeneo gani ambayo tayari tunaweza tukamvutia ili aweze kurudi miaka na miaka ni eneo la chakula tu peke yake. Na ndiyo maana ukiangalia kule kwetu Zanzibar kuna eneo la Forodhani ambalo ni eneo ambalo limeshamiri kwenye vyakula tunaita local food ambavyo vinatokana na bahari. Lakini bado hatujaangalia kwenye eneo hilo.

Kwa hiyo, mimi rai yangu nashauri kwamba tuanzishe hata matamatasha kila mwaka kwenye eneo la uwekezaji kwa mfano kama Dar es Salaam, Arusha, kwenye maeneo yote ambapo watalii wanakuja kwa wingi tuwawekee chakula. Chakula ni taste pekee ambayo inamvuta mtalii kuja nchini na kurudi mara kwa mara tofauti na wanyamapori na fukwe. Kwenye wanyamapori anaweza akaja mwaka mmoja, lakini mwakani akasema hakuna kitu kingine chochote, tembo walewale, simba walewale. Lakini kwenye chakula, tukiweka sasa chakula kizuri zaidi, tukiwawekea vyakula ambavyo tayari tumevifanyia taste zote naamini watalii wale watarudi.

Mheshimiwa Naibu Spika, mfano mzuri tuaangalie Mother Africa hapa tunayo nchi yetu ya South Africa wanalo zao la zabibu kwenye utalii sisi Tanzania tuko vizuri zaidi kuliko hata wao. Lakini wanalo zao la zabibu, zabibu ile ina zaidi ya vinywaji sita, saba na kuendelea. Lakini wao wamefanya kama ni tamasha kwa wao, kwa mwaka wanafanya matamasha zaidi ya 30 katika nchi yao na watalii wanakuja kwa ajili ya ku-taste ule mvinyo na ku-taste kwao inakuwa ni free zaidi. Hata mzungu akienda kwao basi ile taste ya mvinyo aliyoipata South Africa mwaka jana anaipata tena na watalii wengi wanarudi Afrika ya Kusini kwa ajili ya mvinyo.

Kwa hiyo, sisi kama Tanzania bado hatujawekeza tunayo naturally, ardhi yetu ni nzuri, hali ya hewa nzuri na matunda pia ambayo tayari tunayozalisha ni mazuri naya na taste nzuri, huwezi kuyapata dunia yoyote ile. Kwa hiyo, bado hatujaangalia kwenye eneo hilo. Kwa hiyo sisi tuangalieni sisi kama Serikali. Tumsaidieni mama, mama ameonesha rai kubwa, lakini mama ameonesha nguvu kubwa kwenye sekta hii ya kiutalii haijawahi kutokea duniani, Rais kama mama amefanya kazi kubwa sana kwenye hii kwa ajili ya kuitangaza Tanzania. Kwa hiyo, lazima tuweke mipango mikakati kuweka mazingira mazuri watalii wakaanza kuja nchini kwetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo machache nakushukuru sana. (Makofi)