Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Prosper Joseph Mbena

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. PROSPER J. MBENA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na mimi niungane na waliompongeza Mheshimiwa Waziri kwa hotuba yake nzuri. Nianze kwa kusema naunga mkono hoja. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara ya kutoka Kisaki kuja Morogoro, Bigwa kilometa 151, ni barabara ambayo ipo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM. Ni barabara ambayo Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne ameahidi wananchi wa Morogoro Vijijini, ni barabara ambayo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu hii ya Tano ameahidi wananchi kwamba barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami na ni barabara ambayo ilipitishwa kwa ajili ya mpango wa MCC, lakini hata bila MCC kupita bado Serikali iliipa umuhimu kwamba ingeanza na kipande cha kilometa 78 cha kutoka Bigwa hadi Mvuha kwa kiwango cha lami.
Mheshimiwa Mwenyekiti, inasikitisha kwamba barabara hiyo haipo humu kwenye kitabu cha hotuba ya Waziri, hiyo haikubaliki, itatuletea ugomvi usiokuwa wa lazima na wananchi wa Morogoro Vijijini na niwe mkweli kabisa mimi nitakuwa upande wao, tunaihitaji barabara hii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, madaraja yaliyomo katika njia hiyo; lipo daraja la Ruvu, lipo daraja la Mvuha na lipo daraja la Dutumi. madaraja ya Mvuha na Dutumi yanatitia, yanadidimia chini madaraja yale. TANROADS wana habari, wameagizwa washughulikie, lakini mpaka ninavyosema hivi hakuna kinachofanyika na hayamo kwenye mpango huu, inasikitisha. Lakini napenda nimkumbushe Waziri kwamba hilo litaleta ugomvi usiokuwa na lazima.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mafuriko yaliyotokea hivi karibuni sehemu ya Mvuha yamesababishwa kwa sehemu kubwa na matatizo ya madaraja haya kwa sababu yanaenda chini, mvua inayesha, mafuriko yanajaa juu, watu hawawezi kupita, hakuna ukingo, yanaleta ajali kwa watu na magari yanayopita, Mheshimiwa Waziri tusaidie.
MWENYEKITI: Ahsante.