Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi ya kuchangia, lakini hata hivyo niende moja kwa moja kujikita kwenye hoja za msingi.
Kwanza kabisa nataka nimshauri Waziri kwamba sasa hivi tuna makampuni makubwa mawili yanayotoa huduma za ndege Tanzania, FastJet pamoja na Precision. Waheshimiwa wengine walichangia wakikueleza kwamba wale watu wameamua kuwa wezi moja kwa moja; mimi nina mfano moja kwa moja wa Precision Air, ndiyo ndege peke inayokwenda Mtwara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na uwanja wa Mtwara kutokukarabatiwa kwa miaka mingi, lakini Precision Air wamekubali kwenda pale na kutoa huduma kwa ajili ya watu wa Mtwara. Adha ya kwanza tunayoipata Precision Air, reporting time Dar es Salaam ni saa 10.00 usiku kama vile unakwenda nchi za nje. Lakini hata hivyo, kule Mtwara tunatakiwa turipoti saa 11.00 asubuhi kila siku katika siku zote 365 katika mwaka. Sasa kwa sisi tunaotokea mbali na Mtwara Mjini tunalazimika kutoka majumbani kwetu saa 9.00 usiku, wengine saa 8.00 usiku kama akina Mheshimiwa Mkuchika na wengine wanaotokea Newala. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme wazi pia kwamba, hawa watu nauli zao zimekuwa kubwa sana hazifanani na hali halisi na uchumi wa watu wa Mtwara. Precision Air tiketi ya kwenda na kurudi Mtwara sasa hivi imefikia shilingi 850,000, hakuna jinsi ya kuweza kubadilisha. Lakini hawa FastJet unapokwenda Arusha au Moshi ukiwa unaelekea huko, ukitaka kubadilisha safari yako tiketi uliyokata Dar es Salaam kwa shilingi 200,000 unaambiwa kule uongezee shilingi 200,000 ili waweze kukupangia tarehe nyingine uweze kusafiri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba Waziri mambo hayo ayaangalie kwa jicho la karibu sana kwa sababu tunatamani kupata huduma hizi za ndege kwenda majumbani kwetu, lakini kwa bahati mbaya kabisa gharama hizi zimekuwa kubwa sana. Ni bora kwenda Afrika ya Kusini au sehemu nyingine kuliko kusafiri kwenda Mtwara kwa sasa hivi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nirudi kwenye masuala ya barabara; tumeona hapa vizuri kabisa mmetenga, utaanza kufanyika upembuzi yakinifu kwa ajili ya barabara ya Nanganga - Ruangwa - Nachingwea ambako ni nyumbani kwa Waziri Mkuu, ni jambo nzuri kufikiria haya mambo. Lakini sisi tulisema kwamba, hizi barabara ni ring roads, utakapomfikisha Waziri Mkuu katika barabara nzuri kabisa nyumbani kwake, akitaka kutoka pale kuelekea Nachingwea atakwenda vizuri, lakini atashindwa kufika Masasi ambako nako ni central business, anatakiwa akafanye shughuli zake nyingine kule.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona pia katika barabara ya kutokea Mtwara kwenda Newala kurudi mpaka Masasi, zimetengwa sasa hivi pesa kwa ajili ya kufanya kazi katika kilometa 50 tu. Tunasema wazi kwamba hizi hazitoshi, kwa sababu barabara ile toka nchi hii haijapata uhuru iko vile na mliahidi kwamba, mtaweka pale ndani wakandarasi wasiopungua wanne kwa kuwapa vipande vidogo vidogo, ili iweze kukamilika kwa wakati. Hatujaona Serikali hii inafanya jambo hili na sisi tunasema tunaomba mara moja tupewe taarifa hii. Lakini pia barabara ya Lukuledi kwenda Nachingwea hatujaona sehemu yoyote serious inayoonesha kwamba kuna pesa zozote zimetengwa pale kufanya chochote ikiwemo fidia kwa ajili ya watu wa Lukuledi na maeneo mengine.
MWENYEKITI: Ahsante.