Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Stephen Hillary Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuniona. Mimi nianze kwa kuunga mkono hoja, naomba niunge mkono hoja asilimia mia moja kwa sababu Mheshimiwa Waziri na watendaji wake wa kazi wanafanya kazi vizuri na Mungu awabariki muwe hivyo hivyo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nilikuwa na wazo moja tu, nianze na Mkoa wangu wa Tanga. Wabunge wenzangu wa Mkoa wa Tanga wameongea sana na mimi nataka nirudie, kwani Tanga ni Upinzani? Tanga haikutoa kura nyingi ndani ya Chama cha Mapinduzi? Na kama tumetoa, mbona tunaachwa? Naomba sana Mheshimiwa Waziri wewe ni mtu msikivu, pamoja na Wizara zako zote mbili uchukuzi pamoja na ujenzi, naomba muangalie.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano katika Wilaya ya Korogwe, mwaka 2010 Rais wa Awamu ya Nne aliahidi kutengeneza barabara ya lami kutoka Korogwe kwenda Kwa Shemsi kupitia Bumbuli na kutokea Soni. Leo ukiangalia katika kitabu hiki ukurasa wa 51, haikutengewa hata thumni, maana yake ni nini? Zile sehemu ambazo ni nyeti, ambazo zinategemewa, ambazo zilikuwa ni ahadi, Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano amesema, hazikutengewa hata thumni. Mnatutendea haki kweli?
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili ni suala la Mji wa Mombo. Mji wa Mombo uliahadiwa na Marais wawili na leo narudia kwamba Mji wa Mombo itajengwa kwa kiwango cha lami kilometa 1.5 na ikaahidiwa kwamba, kazi hiyo ifanyike. Mpaka leo hii hakuna chochote ambacho kimeweza kuwekwa. Naomba Serikali yangu tukufu, msikilize kilio cha Wanatanga. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la bandari kavu. Suala la bandari kavu ilikuwa toka Awamu ya Kwanza, ilikuwa kwamba, Korogwe Mjini kutakuwa sehemu ya Old Korogwe, kwamba kutakuwa na eneo la kujenga bandari kavu, lakini kwenye kitabu hiki hakuna. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la reli kutoka Tanga mpaka Arusha, mpaka Musoma ni kitu muhimu sana kwa Watanzania wa Kusini. Watanzania wanategemea kuona safari hii kazi inaendelea, lakini cha kushangaza inayoangaliwa…
Mheshimiwa Mwenyekiti, eeh Kaskazini, sawa sawa, lakini kinachoangaliwa ni reli ya kati peke yake na reli ya TAZARA, kwa nini? Hii reli ya Kaskazini haina maana, haifanyi kazi, hakuna watu, hakuna biashara na hakuna viwanda? Naomba Serikali yetu hii muangalie!
Mheshimiwa Mwenyekiti, bandari ni kitu muhimu sana, lakini leo…
MWENYEKITI: Ahsante.