Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi ili na mimi niweze kuchangia hoja ya Wizara hii ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. Nitaanza kuchangia kwa kuzungumzia hoja ya Bandari ya Mtwara na kama walivyosema wenzangu waliopita kwenye masuala ya Kitaifa, basi itikadi tuweke pembeni. Umuhimu wa bandari ya Mtwara umeelezewa vizuri sana na hotuba ya Kambi ya Upinzani ukurasa wa 26; zimetajwa sababu 12, lakini na wewe Mheshimiwa Waziri, ukurasa wa 84 umeelezea umuhimu wa Bandari ya Mtwara. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwa masikitiko makubwa naomba ninukuu kauli za utatanishi ambazo zipo kwenye hotuba hii. Naomba kunukuu, ukurasa wa 84 unasema kwamba, “Bunge lako lilitaarifiwa juu ya kukamilika kwa majadiliano baina ya Mamlaka ya Bandari na mkandarasi wa mradi wa kupanua Bandari ya Mtwara kwa kujenga ghati mpya nne kwa utaratibu wa sanifu, jenga na gharamia,” mwisho wa kunukuu. Lakini hapo chini kuna sentensi ambayo ni ya utatanishi inasema; “napenda kuliarifu tena Bunge lako tukufu kuwa, majadiliano hayo sasa hayakufanikiwa”; kule juu tuliambiwa yamekamilika, sasa tunaambiwa kwamba hayakufanikiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunajikaanga sisi wenyewe, uwekezaji tukiwekeza kwenye Bandari ya Mtwara, hatuisaidii Mtwara tu tunaisaidia Tanzania, sasa hivi wakati wa msimu wa korosho meli ya Dangote ikiingia Bandari ya Mtwara, basi korosho haziwezi kusafirishwa kwa sababu Bandari ya Mtwara inakuwa haina uwezo wa kuudumia meli nyingi. Na tuliaminishwa kwamba, ghati nne zinajengwa na tarehe 26 Februari, 2016 Mheshimiwa Waziri Mkuu alitembelea bandari hii akaulizia kwamba, mkandarasi anaendelaje? Maana nasikia kwamba anazungushwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, alijibiwa kwamba anaendelea vizuri na hakuna tatizo, lakini leo hii tunaambiwa kwamba majadiliano hayakufanikiwa.
Mimi niungane na waliosema kwamba TPA kuna matatizo, Mamlaka ya Bandari kuna matatizo. Kwa hiyo, naomba Waziri utakapokuja kufanya majumuisho utuambie nini kilijiri, nini kilitokea, kwa sababu, kampuni hii ni kampuni kubwa, ni kampuni ya Hyundai ya Japan, haiwezi kuacha mradi huu kwa sababu nyepesi tu ambayo imetajwa hapa. Maana sababu yenyewe imeelezwa kwamba mkandarasi kwa sasa hawezi kugharamia mradi badala yake aikutanishe mamlaka na benki itakayotoa mkopo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kampuni ya Hyundai haiwezi kufanya jambo hili inawezekana kuna uzembe ulifanyika na mtu fulani. Kwa hiyo, naomba Waziri utakapokuja utuambie nini kilijiri mpaka mradi huu mkubwa ukaahirishwa tena kwa dakika za mwisho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi niungane na wenzangu kuzungumzia kwamba, uwekezaji kwa Kanda ya Kusini haufanywi kwa kiasi kinachotakiwa; nimezungumzia Bandari ya Mtwara, lakini unapozungumzia eneo maalum la uwekezaji tunazungumzia Mtwara na Lindi, lakini hata Bandari ya Lindi…
MWENYEKITI: Ahsante.