Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia. Kwanza naanza kumshukuru mwenyenzi mungu ambaye amenijalia afya njema kwa siku ya leo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nianze kumwambia Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, kwamba sitaunga mkono hotuba hii mpaka hapa atakaponipa majibu yaliyo sahihi. Kwa nini nasema hivyo, leo mimi ni Mbunge katika Jimbo la Nyang‟hwale nina umri wa miaka sita katika nafasi hii ya Ubunge.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2010 Mheshimiwa Rais aliyepita wa Awamu ya Nne alikuja kuomba kura kwenye Jimbo hilo la Nyang‟hwale, akatuahidi kutujengea barabara kwa kiwango cha lami kutoka Kahama kupita Wilaya ya Msalala, Nyang‟olongo, Bukwimba, Nyang‟hwale, Busolwa, Busisi na Sengerema kwa Mheshimiwa Wiliam Ngeleja. Mwaka 2012 Mheshimiwa Rais alikuja kwa mara ya pili akiwa ameongozana na Waziri Mheshimiwa Jumanne Maghembe, Rais wa sasa, Mheshimiwa Majaliwa na Mheshimiwa Stephen Masele.
Mheshimiwa Mwenyekiti, alikuja akafanya mkutano wa hadhara pale, akatuahidi tena neno lile lile, kwamba nitawajengea barabara ya kiwango cha lami kutoka Kahama - Nyang‟hwale kuunganisha Sengerema. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2015 mgombea Urais, Makamu wa Kwanza wa Rais, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan naye alikuja akasema maneno yale yale. Tulimuomba na akasema barabara hii itajengwa kwa kiwngo cha lami. Mwaka 2015 Rais wa Awamu ya Tano Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli niliomba na kukumbusha na akasema mimi nilikuwa Waziri wa Ujenzi kipindi kile, sasa nikiwa Rais barabara hii itajengwa kwa kiwango cha lami.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi waliamini na wakatoa kura nyingi sana kwa Mheshimiwa Rais na mimi mwenyewe Mbunge. Leo nina sababu gani ya kuunga mkono hoja hii, viongozi wangu Wakuu wa Kitaifa wametoa ahadi na ahadi hii haimo ndani ya hiki kitabu, naunga mkono nini? Ninaomba Mheshimiwa Waziri, utakapokuja kuhitimisha hapo, bila kutoa majibu sahihi leo sikubali kuunga mkono na nitashika shilingi, itakuwa ni mara yangu ya kwanza leo. Huyo anayesema hawezi sijui yeye ndiye aliyenileta Bungeni? Mimi nasema sitounga mkono hoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna lami ambayo tuliahidiwa, ujenzi wa barabara ya lami kutoka Geita kuja Nyang‟hwale yenye urefu wa kilometa 80, tangu mwaka 2013 tumeweza kujengewa kilometa sita. Kwenye kitabu hiki leo nimesoma nimepangiwa kilometa 2.78, kilometa 80 zitajengwa baada ya miaka mingapi? Nina haja gani ya kuunga mkono hoja hii? Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri ninaomba leo uniambie.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia niende kwenye upande wa mawasiliano. Jimbo langu lina Kata 15, lakini ni Kata sita tu ndizo zenye mawasiliano. Kata tisa ambazo ni Bukwimba, Kafita, Nyugwa, Kakola, Nyamtukuza, Nyabulanda, Shabaka, Nyijundu, Kaboha hazina mawasiliano ya simu. Lakini cha ajabu kwenye kitabu chenu hiki mmesema hivi; Busolwa kuna Mnara lakini haujawashwa, kuna kama Kata sita ziko hapa pembeni mmeonesha kwamba haujawashwa. Hebu niambiwe sababu gani kwa nini minara hiyo haijawashwa na iko tayari leo zaidi ya miaka miwili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa wananchi wa Jimbo la Nyang‟hwale wanamsikiliza leo Mbunge wao, hawamuoni kwenye tv lakini wanamsikiliza kwenye redio kwamba leo Mbunge wetu…
MWENYEKITI: Mheshimiwa ahsante, muda wako umekwisha ahsante.