Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kuchangia bajeti ya Wizara ya Mifungo na Uvuvi ya mwaka 2022/2023.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumshukuru Rais wetu mpendwa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kazi zake nzuri anazozifanya katika Taifa letu. Aidha, napenda kuwapongeza Waziri, Naibu Waziri na Makatibu Wakuu na watendaji wote wa Wizara hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Tanzania tuna wavuvi wengi wadogo wadogo lakini bado hali za maisha sio nzuri na kwa vile wameshavua muda mrefu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wangu, ni lazima tuanzishe viwanda vya Samaki ili kuweza kuwatengezea mazingira bora wavuvi wetu na wale wadogo wadogo ambao watavua bahari kuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaiomba Serikali iweke cold room (majokofu) ya kuhifadhia samaki kwa vile tunajikita katika uvuvi wa bahari kuu. Tukiwa na sehemu hizi tunavutia meli nyingi kuja kuvua nchini kwetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaomba Serikali iweke mikakati endelevu ya muda mfupi wa kuimarisha na kuwasaidia wavuvi ili kuwa na uwezo kamili na kuvua kwenye bahari kuu, kwa kufanya hivi kutasaidia ajira katika nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inapaswa kutoa mafunzo kwa wavuvi wetu wadogo ili kuimarisha uvuvi wa bahari kuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia tunaiomba Serikali kuimarisha upatikanaji wa masoko ya kimataifa ya kuuza samaki. Jambo hili ni muhimu na litasaidia kuitangaza zaidi nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.