Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Naibu Spika, katika ukurasa wa 49 na ukurasa wa 88 wa hotuba ya Mheshimiwa Waziri amezungumzia suala la migogoro ya wafugaji na watumiaji wengine wa ardhi. Nipongeze Wizara kwa kutatua migogoro hii ambapo Mkoa wa Lindi imetatuliwa migogoro kumi. Aidha, kwa mpango wa mwaka 2022/2023, Wizara itaendelea kutatua migogoro husika.

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wangu ni kuwa Wizara ijikite kwenye kuzuia migogoro zaidi kuliko kusubiri itokee ndipo watatue. Ni vema Wizara ikafanya tathimini ya mifugo hitajika kila Mkoa au Wilaya na hatimaye kuweka mikakati ya kudhibiti kuongezeka kwa mifugo katika maeneo husika.