Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. YUSTINA A. RAHHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushuru sana na mimi kupata fursa hii ya kuchangia bajeti ya Wizara ya Mifugo. Nami vilevile nitoe pongezi kubwa kwa Rais wetu Mama Samia Suluhu kuweza kuweka bajeti kubwa katika Wizara hizi za kisekta za uzalishaji kwa kuwatia moyo Watanzania kujikwamua na umaskini ambao umekuwa kikwazo kikubwa kwa wafugaji na wakulima. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna fursa kubwa sana katika sekta hii ya mifugo kuweza kuleta mabadiliko makubwa ya kiuchumi, kuweza kutusogeza katika uchumi wa kati, kwa sababu kwanza ukiona Tanzania tumezungukwa na Maziwa Makuu ambapo tungeweza kufanya uvuvi katika Maziwa Makuu na tungeweza kupata tija samaki tukaweza pengine kuwauza nje na ikachangia katika Pato la Taifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kusikitisha ni kwamba sekta hii bado haijafanya vizuri, kwamba mchango wake kwa Pato la Taifa bado ni chini ya asilimia 10, bado inachangia kati ya asilimia Saba mpaka Nane, sasa hebu ona jinsi tulivyo nyuma lakini tukiwa proud tu kwamba Tanzania sisi ni wa pili kuwa na mifugo mingi, sasa pia hatujaweza kutumia fursa hiyo kujikwamua kiuchumi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Tanzania ni wa pili katika kuwa na mifugo mingi Afrika lakini Tanzania hii pia ni ya pili katika kuwa na udumavu wa mifugo, sasa hii ina-reflect nini? Ina-reflect tu kwamba ulaji au upatikanaji wa mazao ya mifugo bado upo chini na ubora wake upo chini, ndiyo maana hata bado tunaingiza mazao haya ya mifugo kama nyama tunaingiza kutoka nje, maziwa, Samaki sasa tuone kwamba tunapaswa kufanya nini, bado ukienda hoteli za kitalii, ukienda supermarket, utakuta kwamba mazao ya mifugo bado tunaingiza kutoka nje. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika hotuba ya Waziri ameweza kuona ni kwanini tuna kipato kidogo kutokana na mazao ya mifugo, amesema mojawapo ni kuwa na kosafu za mifugo yetu, tuna asilimia 90 ya mifugo ni mifugo yetu ya asili ambayo kosafu ndiyo sababu pengine ya kuwa na tija ndogo, vilevile magonjwa ya mifugo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli bado hatujawa na sheria, kwa mfano tunamajosho huko sheria ya kuogesha mifugo bado hatujaweza kuisimamia na ndiyo maana majosho sehemu nyingine pia yapo hayatumiki ni bahati tu kwamba mifugo ya kienyeji ina ustahimilivu mkubwa, lakini inang’atwa na kupe, inatembea na kupe, inakuwa na minyoo, ndiyo maana mifugo yetu haina ubora. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ni la malisho pamoja na maji. Naipongeza Wizara kwa intervention inazofanya katika matatizo haya. Kwa mfano, Wizara imetenga karibu bilioni 3.9 katika kubadilisha kosafu za mifugo kwa kufanya uhimilishaji. Sasa uhimilishaji huu namuomba tu Waziri kama kweli ana nia njema, kazi hii ambayo itafanywa na Maafisa Ugani huko kwenye Halmashauri kwa wafugaji, kwa kuwa amenunua pikipiki za Maafisa Ugani wa Mifugo basi angewapatia kabisa mitungi ya kubeba liquid nitrogen ili huko kwenye makundi haya ya mifugo ya asili waweze kufanya uhimilishaji ambao kwa vyovyote vile ni ngumu kufanya uhamilishaji kwa sababu mifugo hii ya asili inachungwa pamoja, mitamba pamoja na madume. Pengine basi angeweza kusambaza hata madume labda madume bora ya mbegu kuweza kufanya uhimilishaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile nakisemea kituo cha NAIC kinachozalisha hizi artificial insemination tunachokituo kimoja kiko Arusha na hali yake si nzuri, uwezo wa kuzalisha mbegu za kutosha za kusambaza Tanzania nzima bado ni mdogo, pengine Waziri ningeshauri tu kwamba kama kuna uwezekano wa kufanya extension, kwa mfano mifugo iliiyopo Dodoma kutegemea NAIC iliyopo Arusha peke yake bado haiwezi kutosheleza, mifugo iliyopo Shinyanga, Mwanza utegemee NAIC peke yake na kwa sababu umewekeza kidogo huko NAIC uhimilishaji gharama yake ni kubwa. Kwa mfano, kwa sasa hivi ukimpandisha ng’ombe mmoja unampandisha kwa elfu ishirini pengine hata asiwe na mimba urudie. Kwa hiyo, na gharama hizi zipunguzwe ili wafugaji wengi waweze kutumia hizi artificial insemination. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, namna nyingine ambayo umeona ni kubadilisha kosafu ni kuzalisha mitamba kwenye mashamba ya Sao Hill pamoja na NARCO na kwingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba hii mitamba sasa isambazwe huko vijijini kwa akina mama, tunaweza tukawashauri akina mama zetu ile asilimia kumi ya mkopo anaopata mapato ya ndani kutoka Halmashauri wanaweza wakawekeza huku wakajenga mabanda mazuri ili sasa Wizara mitamba hiyo isambaze kwa akina mama.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna asasi isiyo ya Kiserikali kama Heifer International imefanikiwa sana katika kusambaza mitamba kwa namna kwamba ukipeleka mitamba hiyo hata mitano katika kijijini kimoja itasambaa na kijiji kizima itajaa kwa maana ya kukopesha mtambo, utampa mama akizaa anampandisha yule ndama na akishampandisha anampa jirani yake. Kwa hiyo, mifugo hii itazunguka na kwa ajili hiyo akina mama watapunguza umaskini. Kwa hiyo, hilo moja naomba tu isambazwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, intervention nyingine uliyofanya ni katika kuzalisha malisho ya mifugo. Ni kweli wazo hili ni zuri lakini uzalishaji huu kwa maeneo ambayo hakuna miundombinu ya umwagiliaji, malisho haya yatazalishwa kama mazao mengine wakati wa masika kwa maana hiyo wakati wa masika malisho yatakuwa mengi, tukirudi kwenye kiangazi changamoto ya malisho itakuwa palepale. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa sambamba na kusambaza hii ambapo umetenga karibu Bilioni 1.2 umesema utaweka na mashamba darasa kwenye Serikali za Mitaa, mimi nishauri tu kwamba usambazaji wa mbegu za malisho ziendane na kuwawezesha wafugaji kuweza kuhifadhi sasa malisho ya mifugo ili ije iwasaidie kipindi cha kiangazi, wakatengeneza ma-bell ya hay wasile kile kipindi cha kiangazi iwasaidie, vinginevyo tutafika kiangazi bado kutakuwa na changamoto ya malisho. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kipindi cha kiangazi ng’ombe mpaka wanakorogewa uji na wengi wanakufa, kwa hiyo hii ni hatari sana lazima tupeleke teknolojia kuhifadhi malisho kwa wafugaji wetu tukitaka tuwasaidie. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo mchango wangu mwingine ni kwenye vituo vya kukusanya maziwa. Kiukweli maziwa kipindi cha masika maziwa ni mengi sana na kwa sababu maziwa ni mengi kina mama au watu waliopo vijijini wanashindwa kuyapeleka kwenye masoko hii ni kwasababu pengine mifugo yetu ya asili hii anakamua labda nusu au mpaka lita mbili sasa hizo chache hawezi kwenda kilometa chache kufuata soko la maziwa. Tungeweza kuweka hivi vituo bado hizi zingekuwa payroll za akina mama kama ameweza kupeleka hata lita mbilimbili kwa wiki ana hakika tu kabisa kwamba anazo pesa za kuweza hata kununua supplement, hata dawa za mifugo kama Serikali inashindwa pengine kupeleka vituo vingi vya kukusanya maziwa hata inaweza ikashawishi ushirika ulioko kijijini hata SACCOS lakini hii ni muhimu sana, asilimia karibu 66 au theluthi ya maziwa tunayotumia humu ndani yanatoka kwa mifugo. (Makofi)