Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia Wizara hii ya Mifugo na Uvuvi, kwanza nimshukuru waziri mwenyewe na Naibu Waziri wake na watendaji wake wote wanaofanya kazi wanafanya kazi vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kwamba Mashimba wewe ni ndugu yangu na unafanya kazi na unatembea kila mahali tunakuona unafanya kazi na Ulega lakini kiukweli wizara ambayo siielewe ni hii hapa. Siielewi kwa sababu gani najiuliza hivi sisi watanzania kwa nini tunakariri maneno tumekariri maneno kwa nini? Zero grazing kwa nini tunakariri? Wafugaji wanaangaika kila nchi kila mahali wanaangaika tuna pori mapori ya NARCO ambayo yana uwezo wa kuchukua ng’ombe 61,000 waliopo sasa hivi ni 19 zero grazing kwa nini tunaangaika wenzetu hawana maeneo? Nchi yetu bado nzima ukienda singida ukienda maeneo ya mapori yapo ya kutosha tuna Hifadhi za Taifa ziko 22 zinazofanya kazi na kutoa hela ni tano tu 17 zimelala.

Mheshimiwa Naibu Spika, tuna game reserve uwa najiuliza hivi maana ya game reserve ni ni hivi neno reserve maana yake nini? Maana yake sijui ukipata shida usaidiwe ziko 27 zinafanya kazi 5 tu, tuna open area tuna maeneo ya wazi mengi tu tuna misitu, wafugaji wanauwa ng’ombe eti Wizara ya Mifugo na Uvuvi kazi ya kufanya ni kupeleka hereni yani wananchi wale wanateseke wewe wanaenda tena na hereni wananchi wanateseka uwapi malambo, hivi hii wizara ikoje? Hivi tukifanya zero grazing watanzani hivi minada ya watanzania si ndio study tour yao hivi leo mbuzi unaweza kwenda mnadani ukanunua mbuzi mmoja laki moja utaweza?

Mheshimiwa Naibu Spika, hivi mbona Wabunge wote kila mnada mnaenda na watu wanaishi pale kwa starehe kwa nini tusitafute solution ya wafugaji tukawapa maeneo. Sikubaliani leo kwamba pori fulani tuwape wafugaji tukiwapa pori tuwapangie vitalu, na walipe kodi leo ukienda Misenyi ng’ombe wale walioko NARCO misenyi ile inahitaji ng’ombe 15 wako ng’ombe 900 kila mahali mashamba ya Serikali yapo hayana ng’ombe wafugaji wanateseka kila mahali na ng’ombe tunakula nyama tunakunywa maziwa kuashia koo imeisha ipo tu why.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikuombe waziri najua unafanya kazi na wenzako sasa mkae kwa kweli hii bajeti tutawapitishia lakini bajeti ijayo mtatuambia hivi kazi kweli humu ndani ikoje? Hivi kuna nini kwa nini watu wanateseka? Amezungumza Mbunge mmoja hapa ukianza kuzungumza habari ya mfugaji umezungumza mwananchi, watu wanateseka mali zao zinaisha, nenda umasaini ng’ombe zinaisha kila mahali nenda Mara juzi nimekwenda pale Mto Mara mtu wangu amenywesha ng’ombe mkasema mavi yamekuja ng’ombe wahame, mavi yanauwa samaki.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa jamani ehe! tukubaliane kwamba hawa wafugaji mnataka tuweje? Tuna nchi yetu ina mifugo mingi, tunakula nyama mnadani, tunatosheka na nyama, halafu tunafilisi watu tuteseke, kwanini tuteseke? Kwa nini wananchi wateseke na nchi yao ipo? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jamani nendeni Hispania, mimi nimekwenda Hispania pale, wana eneo kama Mkoa mzima, wanazo block za kutosha, wana ng’ombe wa kutosha. Hiyo haitoshi, Mheshimiwa Waziri Mashimba hebu nikuulize swali, hivi leo una ng’ombe wapo hapo NACRO – Kongwa, hivi ukichukua madume kwa sababu dume moja linazalisha majike 25, hivi ukichukua madume yale ukawagawa hata kwenye Kata madume 40 ni ng’ombe 1,000 tukaanza kubadilisha ufugaji wetu kwa kutumia madume yetu, hivi shida iko wapi? Shida ni nini?(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, zamani Mwalimu Nyerere alipeleka ng’ombe kila mahali kila kijijji, leo hakuna kitu, mnaacha wafugaji wanaisha lakini mnadani mmekaa na vitabu mnakusanya ushuru, mnakusanya wapi? Mnada wa kwenda Kenya badala ya kwenda Tarime mpakani alivyozungumza Mbunge hapa mnaweka kirumi, maana yake ndiyo nini kirumi mimi sielewi sasa, yaani mnapokwenda kuweka mpakani kirumi ukienda Misenyi tunapambana na Uganda kwa malisho, mnasema Uganda wanakuja kulisha huku ndani, hivi pori limejaa na majani yapo, kwa nini watu wasilishe, shida nini? Mkae mpange! Wizara hii nami naanza kuitilia mashaka, hivi kweli mnapigania ng’ombe au mnampigania nani? mnapigania samaki au mnampigania nani? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa mimi naomba mkae…

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Getere hebu subiri kidogo hapo, Mheshimiwa Lucy uko salama hapo? Upo salama, kama upo salama kaa pembeni, maana yake! Haya Mheshimiwa Getere endelea. (Kicheko)

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipunguza, maana yake jazba ni kubwa sana kwa sababu mimi kuna vitu naviangalia miaka nenda rudi, miaka nenda rudi, watu wanahama wanafilisika, mtu alikuwa na ng’ombe 1,000 zinakuwa mia mbili, zinakuwa mia, zinakuwa sifuri, kila mwaka watu wanahama, ardhi ipo imejaa Tanzania, hamuweki!

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mashimba sasa nikuulize swali, juzi nilikuja ofisini kwako na Diwani na Kata ya Salama na Kata ya Kiloleli mkatuambia mnatupa majosho yale mawili, Kiloleli na Salama Kati, mkatuonesha bajeti je, hizo fedha ziko wapi? Mpaka leo hatuzioni, eti Wizara ya Kilimo fedha zake Milioni 18 za kwenda kuchimba majosho mpaka sitolewe kwenye Wizara! Eti yenyewe haitoi Wizara, yaani humo ndani kuna matatizo humo ndani! Hii Wizara muitengeneze, ninawaomba Watendaji wenu muwatengeneze ninyi ni viongozi wazuri, nawashukuru sana muendelee kufanya kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)