Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Mimi nina mambo machache tu. Nitaunga mkono bajeti ya Mheshimiwa Waziri akinipa majibu juu ya mambo yafuatayo:-
Jambo la kwanza ahadi ya Mheshimiwa Rais Kikwete aliyeitoa mwaka 2005 na baadaye mwaka 2010 katika Jimbo la Nzega na bahati nzuri Meneja wa TANROADS, Mkoa wa Tabora yupo, juu ya ujenzi wa lami kilomita 10 ndani ya Mji wa Nzega, ahadi hii ilikuwa ya Rais Kikwete. Mwaka 2014, Rais Kikwete alifika Nzega akiwa na Rais wa sasa wakati huo Waziri wa Ujenzi aliiongelea barabara hii. Baadaye Rais Magufuli akiwa mgombea aliongelea suala la ahadi hii. Kwa hiyo, naomba majibu kwa Mheshimiwa Waziri juu ya suala hili nijue nini kinafanyika ili niweze kumuunga mkono na yeye anafahamu namheshimu sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, Mheshimiwa Rais aliahidi madaraja mawili katika Jimbo la Nzega na ni kwa sababu Halmashauri kupitia TAMISEMI hawana uwezo wa kuyajenga madaraja haya, daraja la Nhobora na daraja la Butandula pamoja na barabara zake. Hli ni jambo lingine ambalo napenda kupata majibu.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la tatu, nataka niseme kidogo kuhusu Bandari ya Bagamoyo. Mimi naiunga mkono kama strategic investment kwa nchi na study zinaonekana kwamba by 2030-2035, six percent ya mzigo wa dunia wa kibiashara unaopita katika bahari utapita kwenye bahari ya Hindi. Tathmini za kisayansi zinaonesha hakuna bandari itakayokuwa salama duniani kwa gharika mbalimbali kama Bandari ya Bagamoyo. (Makofi)
Mheshimwia Naibu Spika, lakini tatizo langu ni moja kama nchi tunalipa fidia, kama nchi tunachimba kuongeza kina cha bandari hii, what is the stake ya kwetu, share yetu kama Taifa kwenye mradi wa Bandari ya Bagamoyo ni asilimia ngapi? Kwa sababu the biggest part ya expenses tunafanya sisi kama nchi, kupokea wharfage tu haitutoshi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la nne, Rais Kikwete aliahidi Wilaya ya Nzega wakati anamnadi Mheshimiwa Dkt. Kigwangalla na Mheshimiwa Selemani Zedi, ujenzi wa barabara ya kutoka Tabora kupita Mambali kufika Itobo kwenda Kahama. Nitaomba majibu kutoka kwa Mheshimiwa Waziri nini kinafanyika. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hizi nilizozitaja ni barabara muhimu sana kwa wakazi wa Mkoa wa Tabora. Vilevile madaraja haya, daraja la Nhobora ni daraja la uhai kwa wananchi wa Jimbo la Nzega kwa sababu hili daraja mto wake ndiyo unaenda ku-connect kule ambako Mheshimiwa Rais Magufuli akiwa Waziri wa Ujenzi alijenga daraja kwa kutumia local engineers Wilaya ya Igunga. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho nilitaka niwaambie Waheshimiwa Wabunge tuna haki ya kukosoa na nataka niwashauri Waheshimiwa Mawaziri, kwa karne hii tumepata the most honest President. Rais Magufuli is honest, ni mkweli, kama hataki jambo atasema, hana siasa. Niwaombe Waheshimiwa Mawaziri mmepata kiongozi wa kufanya naye kazi ambaye ni most result oriented, msaidieni kumshauri, msiogope. Sisi huku mtaani tunasema mna nidhamu ya uoga, tunawaomba kama kweli ipo basi msiifanye hii. Kwa sababu huyu mtu deep in his heart anachokisema ndicho anachokiamini na hata kama kuna makosa amewahi kufanya au anafanya basi tujue deep in his heart hana malicious interest na nchi hii. Mheshimiwa Magufuli ana-represent the true picture ya common Tanzanian na anayajua maisha ya Watanzania, kwa hiyo, tumsaidie kuweza kufikisha nchi hii anakotaka. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.