Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa huo muda wa dakika tano, nafikiri itanitosha kwa vile ya kwangu ni machache sana.
Napenda kuanzia kwa kumpongeza kwanza Waziri na Naibu wake na timu nzima ya Wizara hii kwa hotuba yao nzuri. Pia napenda kusisitiza katika mipango yao wangejaribu kuangalia mawasiliano ni muhimu sana katika uchumi wa nchi yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, ameongelea kuhusu mobile money banking kwenye hotuba yake ya kwamba Tanzania inaongoza duniani kwa kuwa na mzunguko wa karibu shilingi trilioni 4.5 za mobile money. Tujaribu kuangalia, je, hizo pesa zote ambazo ziko kwenye mzunguko wa shilingi trilioni 4.5 kwa mwezi zina umuhimu gani kwa Taifa letu hasa kwenye uchumi wetu? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini cha kuangalia zaidi ni namna gani zinasimamiwa? Ninaangalia haya makampuni mengi ambayo yanaendesha hii biashara hata mahesabu yao yanaonesha kuwa yanapata hasara. Sasa hii pesa ambayo ni 20% ya pesa zote za amana za nchi hii zinasimamiwa na makampuni ambayo yanapata hasara na hizi ni pesa za wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, namuomba Waziri pamoja na mwenzake Waziri wa Fedha waangalie mifumo ya benki sasa hivi imebadilika kutoka kule kwenye traditional banking kuja kwenye hizi benki za kileo ambazo zaidi zinatumia teknolojia. Tujiangalie ni kwa nini sisi Tanzania tuongeze hapa, are we in control, sidhani! Inaweza kuwa ni bomu hili, kwa hiyo tujiangalie sana kwa hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ambalo napenda kuchangia ni uwanja wetu wa Songwe, miaka 14 uwanja haujakamilika na Mbeya ni geographical strategic kwa nchi yetu. Nchi zote zinazotuzunguka ni nchi kubwa za SADC na abiria wengi wanatoka huko, hivyo tukimalizia huo uwanja utatusaidia kukuza uchumi wa nchi. Kule tuna mazao mengi ikiwemo maua na mbogamboga na wenzetu wote wa Nyanda za Juu Kusini wanategemea sana huu uwanja. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini lingine ni TAZARA, watu wengi hapa hawajaongelea umuhimu wa TAZARA, kwa nini tujenge vitu vipya badala ya kuimarisha vitu tulivyonavyo? Investment ya TAZARA ni kubwa sana. Unaongelea bandari bila ya kuongelea TAZARA utakuwa unapoteza muda wako. TAZARA ndiyo tunaitegemea lakini haina menejimenti imara, muundo wake ni mbovu na wa kizamani tuuangalie. Naomba sana pamoja na kuboresha TAZARA angalia vilevile kujenga Bandari Kavu Mbeya kwenye kijiji cha Inyara itasaidia nchi zote zinazotuzunguka. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lingine la mwisho ni suala la barabara zinazounganisha mikoa. Tuna barabara yetu ya Isyonje – Kikondo -Makete na Njombe, ni ahadi ya Rais, aliahidi akiwa Igoma na akaahidi tena akiwa Kikondo kuwa hii barabara itakamilika kwenye bajeti ya mwaka huu sasa mmeiweka wapi? Haya ndiyo maeneo yenye uchumi mkubwa wa nchi hii. Kwa nini hatu-invest kwenye vitu ambavyo vitazalisha na kuleta uchumi mkubwa kwenye nchi hii? Tunahangaika na vitu vingine ambavyo unaweza kusema labda ni vitu vya anasa hata kama ni muhimu lakini ni anasa zaidi lakini vitu ambavyo ni kwa ajili ya kujenga uchumi wa nchi hii hatuviangalii. Naomba hiyo barabara iwemo kwenye bajeti ya mwaka huu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimalizie hapo, naunga mkono hoja, ahsante.