Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017 MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nikushukuru kwa kunipa fursa hii adhimu. Pia niwashukuru wananchi wa Jimbo la Mchinga, Mkoa wa Lindi, kwa kuniamini na kunichagua kwa kura nyingi kuwa Mbunge wao. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kueleza huzuni kubwa niliyonayo kwamba Diwani wa Kata ya Kimwani, Jimbo la Muleba Kusini kupitia Chama cha Wananchi CUF jana ameuawa akiwa nyumbani kwake kwa kukatwakatwa mapanga. Tunashukuru Jeshi la Polisi tayari limekwishamkamata mgombea wa CCM ambaye alishindwa na tunaamini haki itatendeka. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatengeneza mipango ya kwenda kutatua changamoto za wananchi, lakini wenzetu mliopo madarakani hamkubali kushindwa. This is very shameful to our country. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati naanza kuchangia mapendekezo haya, niyakumbuke maneno ya Profesa mmoja Mchumi wa Uingereza lakini kwa bahati mbaya anafundisha mpira. Wiki iliyopita timu yake ilicheza na timu nyingine na kwa bahati timu yake ndiyo nilikuwa naishabikia. Baada ya matokeo timu yake ikawa imefungwa, anahojiwa na Waandishi wa Habari anasema, we had good attitude and fantastic spirit despite the result. Anasema attitude ni nzuri, spirit ni fantastic lakini matokeo ni mabovu, wamefungwa. Ndiyo hili ninaloliona siku zote Tanzania tunapanga mipango mizuri, mipango ambayo inapoletwa ndani ya Bunge inapata sifa kubwa kwamba ni mipango mizuri na inatoa dalili ya matumaini kwa Tanzania lakini matokeo siku zote yamekuwa ni mabovu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa napenda kuishauri Serikali ya Awamu ya Tano, Serikali ya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, asije mwisho wa siku akalalamika kama alivyolalamika kocha wangu mimi kwamba good attitude and fantastic spirit despite the result na ili yasimkute haya aangalie anatumia mfumo gani kuwapata Watendaji Serikalini na wasaidizi wake. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi karibuni tumesikia ametumbua majipu kwa Mabalozi. Hatuwezi kustaajabu kuona Mabalozi wetu wanafanya kazi chini ya kiwango, wanachukuliwa makada wa CCM walioangushwa kwenye Ubunge, wananchi wamewakataa, ndiyo wanakwenda kuwa Mabalozi, utatumbua tu. Napenda Mheshimiwa Magufuli asije akashindwa, aangalie mfumo wake wa kuwapata wasaidizi na watendaji wake ili mipango mizuri hii tunayoipanga iweze kuwa na tija kwa Taifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, natokea Lindi, tuna changamoto kubwa Lindi ya misitu yetu kuvamiwa, sijui niwaite majangili wa misitu au niwaite watu gani. Mkoa wa Lindi ulikuwa ni miongoni mwa mikoa yenye hifadhi kubwa ya misitu, Hifadhi ya Selous iko kule lakini tuna hifadhi kubwa ya misitu ambayo wananchi na Serikali kwa nia nzuri kabisa tuliamua kui-conserve kwa manufaa ya Taifa hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa bahati mbaya sisi Mkoa wetu wa Lindi unapatikana katika hali ya kitropiki ambapo mvua zetu tunategemea misitu na bahari. Waziri wa Muungano anayeshughulikia misitu naomba asikilize hili, kuna uvunaji wa kupita kiwango wa misitu ambao unawahusisha vigogo wa Serikali. Ndiyo maana mimi kama Mbunge na Wabunge wenzangu tumekuwa tukilalamika, tumekuwa tukiwaeleza Wakuu wa Wilaya, tumekuwa tukimueleza Mkurugenzi, kila siku misitu iliyohifadhiwa na Serikali inaisha na ukikamata mbao unakuta zimegongwa, tunapata shida. Hatuwezi kutengeneza mipango ya maendeleo wakati rasilimali na maliasili hii tunaiacha ipotee hivihivi tu. Hawa watu hawalipi kodi na hata wakilipa kodi wanafanya over harvesting (wanavuna zaidi).
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri wa Maliasili ulichukue hilo, very serious. Tuna shida misitu Lindi inaisha, inapotea, mmeleta ng‟ombe wengi wasiokuwa na idadi lakini hiyo ni nafuu, tumeweza kuwa-accommodate, hatuna migogoro ya wafugaji na wakulima, shida yetu kuna majangili wa kukata misitu hovyo. Kuna msitu mkubwa wa hifadhi katika Jimbo la Mchinga, Msitu wa Nkangala unavunwa, Mkurugenzi anajua, Mkuu wa Wilaya anajua, Mkuu wa Mkoa anajua, naomba mchukue tahadhari katika hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala la uvuvi, mimi nashangaa kwelikweli. Jimbo la Mchinga ama Mkoa wa Lindi umepakana na Bahari ya Hindi, inafikia wakati samaki wanazeeka na kufa wakaja tu kuokotwa ufukweni hivi, maana yake kwamba ile bahari watu hawajavua na wavuvi hawajawezeshwa. Staajabu yenyewe kubwa iliyopo maeneo yote ambayo bahari imepitia ndiyo kuna watu maskini kwelikweli. Bahari badala ya kuwa ni faraja au kitega uchumi muhimu imegeuka kuwa laana kwani walio karibu na bahari wote ni maskini. This is very shameful.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati wenzetu wanatumia bahari tu uchumi wao umekuwa mkubwa sisi watu tuliokuwa karibu na bahari ndiyo maskini. Kwa bahati mbaya mnapopanga hii mipango, pangeni na namna ya kuwasaidia wavuvi, msipowasaidia ndiyo wanatumia zana haramu za uvuvi. Watu wanapiga mabomu, wanatumia makokoro na kadhalika, hatuwasaidii, tunabakia kulalamika tu kwamba achene uvuvi haramu, hawataacha kwa sababau hawana alternative.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri suala hili mlichukue, wakati mnakwenda kutengeneza huo mpango ambao mtau-submit tena, wekeni nguvu kwenye suala la uvuvi. Nilishukuru kweli, kwenye hotuba ya Mheshimiwa Rais, ukurasa wa 23 aliweka msisitizo kwa suala la uvuvi, alisema kwamba viwanda, uvuvi na kilimo ni ajenda yake. Naomba tuone kwa vitendo wakati mtakapo-submit Mpango wa Miaka Mitano au wa mwaka mmoja, tuone mmewekeza nguvu kubwa katika suala la uvuvi. (Makofi)
Mheshimiwa mwenyekiti, suala la viwanda, Mkoa wa Lindi na Mtwara imejaliwa. Imekuwa nyuma kimaisha kwa muda mrefu, uchumi wetu umekuwa wa chini sana lakini Mwenyezi Mungu ametuletea neema ya gesi ambayo ni utajiri na ni umeme pia. Tunashukuru Mheshimiwa Profesa Sospeter Muhongo pamoja na REA wamejitahidi vijiji vingi hivi sasa vinapata umeme Lindi na Mtwara. Mie nashukuru Jimboni kwangu zaidi ya 80 % ya vijiji vimepata miradi ya REA. Naomba tu Mheshimiwa Muhongo unimalizie vile vijiji kumi na tano vilivyobakia ili Jimbo zima liwe linawaka umeme. Haitakuwa upendeleo maana umeme unatoka kwetu, gesi ipo kwetu, tukiwa na umeme namna hii ni jambo la kheri na ndiyo wananchi watapunguza kelele ya gesi ibaki na mambo kama hayo. Tumelalamika, watu wakapigwa, tukaelimishwa tukaelewa, bomba limejengwa, sasa hivi tunalilinda, tuwekeeni umeme katika kila kijiji ili tuone sasa kumbe manufaa ya gesi ni haya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini suala hili liendane na viwanda. Tuna rasilimali nyingi, tuna maliasili nyingi, Mheshimiwa Profesa Sospeter Muhongo anajua, kuna madini mengi yako Lindi. Jimbo la Mchinga kuna madini mengi ya kutengeneza cement na vitu vingine ninyi wenyewe mnajua. Wasaidieni wachimbaji wadogowadogo waweze kupata mitaji ili wao waweze kuchimba. Tusiwaachie hao watu wanaanzisha viwanda, yeye ndio ameanzisha kiwanda, yeye ndio awe ana-transport minerals, tusifanye hivyo tutashindwa kutoa fursa kwa wananchi maskini hawa. Naomba nishauri hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho, ili mipango yetu yote iende vizuri tunahitaji tuwe na amani. Tunahitaji tuwe na amani ya kweli siyo amani inayozungumzwazungumzwa tu. Tunalalamika kuhusu suala la Zanzibar, Bukoba watu wanauana.
MWENYEKITI: Muda wako umekwisha Mheshimiwa.
MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. (Makofi)