Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Lucy Simon Magereli

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. LUCY S. MAGERELI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa fursa ya kuchangia jioni ya leo katika Wizara ya Ujenzi, Miundombinu na Mawasiliano.
Kabla sijaenda mbele nianze kwanza kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kupata fursa ya kuwepo ndani ya jengo hili, ninamshukuru amejibu ndoto zangu, ingawa ninachokiona haki ya Mungu ninastaajabu. Sikuwahi kufikiri kile chombo kinachoitwa Serikali ambacho tuliamini ni supreme haya ndiyo kinayoyafanya na kwa kweli ninasikitika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijaendelea nimpongeze na nimtaje kwa heshima kabisa kiongozi wangu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mheshimiwa Freeman Aikaeli Mbowe, kamanda, kuwa mpinzani kwa miaka zaidi ya 20 siyo mchezo. Kazi uliyoifanya tumeiona, leo Bunge hili lina watu mahiri sana ndani yake ambao wataisaidia sana Serikali hii na si Bunge hili tu hata Bunge lililopita ndiyo kati ya Mabunge ambayo yaliwaamsha Watanzania wakajua ni nini kinachoendelea kwenye nchi yao na hatimae tuko hapa tulipo na tunafanya tunachokifanya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niende moja kwa moja kwenye suala la daraja la Kigamboni. Nilimsikia Mheshimiwa Tizeba akichangia akisema, eti kwenye bajeti ya Wizara wameweka kivuko kingine cha Kigamboni; sawa sawa kabisa na mkiweke kwa sababu lile daraja mmetengeneza photo point, watu wakapige picha, siyo kwamba mmetengeneza liwasaidie chochote watu wa Kigamboni. Tulikuwa tunahangaika na vivuko vibovu…
…habari ndiyo hiyo, tulieni sasa mpate habari zenu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tulikuwa tunahangaika na vile vivuko vibovu despite the fact kwamba viko tu kilometa sifuri kutoka Ikulu, lakini huduma tuliyokuwa tunapata pale ni mbovu kabisa na leo Serikali ikaja ikatuahidi ya kwamba tunajenga daraja halafu maisha yetu yatabadilika, hayajabadilika chochote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lile daraja linaendelea kuchajiwa, Watanzania wa Kigamboni wanalipia lile daraja, tena eti mnasema mnaweza kumtenganisha Mtanzania wa Kigamboni na baiskeli na pikipiki na bajaji na hiace na gari la mzigo. Hivi mmemtenganishaje huyo Mtanzania wa Kigamboni? Mmempa ahueni gani? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, gharama za kivuko ndizo hizo hizo zilizohamishiwa kwenye gharama za daraja la Kigamboni, Mmempa ahueni gani mama ntilie? Mmempa ahueni gani yule Mtanzania anayesubiri kununua kifaa cha ujenzi akafanyie shughuli zake za ujenzi? Mmempa ahueni gani ikiwa lile guta tu ambalo linachukua bidhaa Buguruni na Kariakoo kupeleka Kigamboni linachajiwa gharama ile ile sawa na iliyokuwa inachajiwa kwenye gharama za kivuko? Hakuna mabadiliko, hakuna ahueni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye kivuko mlituambia mnatuchaji kwa sababu kuna gharama za uendeshaji, well and good. Mmeleta daraja tunachajiwa gharama zile zile, eti mnasema anayekwenda kwa mguu tu ndiye amepata ahueni, amepata ahueni gani? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi niko Dar es Salaam nimekwenda mjini kwa shughuli za kikazi nikapigiwa simu nyumbani, mtoto anaumwa. Nimekwenda asubuhi nimelipa shilingi 2,000, nikarudi Kigamboni kumchukua mtoto nikalipa shilingi 2,000, nikarudi hospitali nikalipa shilingi 2,000, baada ya mtoto kutibiwa nikarudi nyumbani nikalipa shilingi 2,000, ni lazima nirudi kumalizia lile jukumu langu mjini nikalipa shilingi 2,000, jioni nilirejea nyumbani nimelipa shilingi 2,000, umenisaidia nini? And that not only me, Watanzania wengi wa Kigamboni wanapitia katika hatua hiyo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali ifikirie upya kuhusu habari ya tozo za daraja la Kigamboni; mmetumia pesa za Watanzania, lazima ziwarejee.
Lazima pesa za Watanzaia zilizotumika kujenga daraja la Kigamboni, mmejenga Malagarasi, mmejenga la Mkapa, mbona lile hamku-charge? Hawa Watanzania wa Kigamboni na wao wanalipa road licence kama ninyi. Zile gharama za barabara tunazokatwa kwenye lita moja ya mafuta na wao wanalipa, mbona mnawa-double charge?
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tukubaliane ya kwamba mmewaonea sana watu wa Kigamboni, mmewanyanyasa sana, mmewanyonya mno kwa tukio hilo la kuamua kuwa-charge kwenye lile daraja, lakini tukubaliane pia kwamba, hamjawatendea haki hata kidogo. Utabaki kuwa msimamo wangu na Mheshimiwa Waziri naomba ulichukue hilo ulifanyie kazi utupe majibu, hutaki tutakuachia lile daraja sasa upigie picha tuendelee kupita kwenye Kivuko kwa sababu tunachajiwa kitu kile kile, adha yetu ni ile ile, lakini shukrani kutuongezea kingine basi, ili walau tuendelee kuteseka kwa sababu, sioni kama umekuja na mkakati wa maana sana juu ya kusaidia hatma ya Kigamboni na maendeleo yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lile eneo la Kigamboni ukishaondoka tu pale darajani, pana njia nyembamba kama mrija wa biki. Kwa hiyo, mlipanda pale juu mkafanya kazi ya kisiasa, mka-celebrate mkaondoka, hamkujua watu wakishaondoka mjini basi kule mliko-cross mkasema cross overs sawa, baada ya kuondoka darajani unarudi Kigamboni, barabara pale iko wapi? Usanifu wa kina mnaoita, sijui na upembuzi yakinifu ulishafanyika, wale matajiri wanaomiliki matenki ya mafuta maeneo yale barabara iliyopangwa kutoka daraja la Kigamboni ilipaswa ipite maeneo yale, leo sijui mmekaa meza gani, mmejadiliana namna gani, wananchi wangu wananiambia mmebadilisha msimamo, eti mmeamua kwenda kupitisha daraja tena eneo la makazi ya wananchi ambao hawakufanyiwa tathmini, mnaendelea kutunyonya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nihamie kwenye suala lingine, suala la Serikali kukopa holela; Serikali yetu eti imepata kimbilio la kwenda kukopa fedha China na wao wamejua kabisa ya kwamba wana ajenda yao. Na mkigonga tu hodi wanasema yes, what do you want men? Mmepewa dola milioni 500 kwa ajili ya fedha za maendeleo…
MHE. LUCY S. MAGERELI: ...hizo pesa zikapotea. zikayeyuka.
MHE. LUCY S. MAGERELI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Wakandarasi wanaofanya miradi ya maendeleo hapa Tanzania, wakandarasi wa Kichina, wamedai fedha zao mlishakula! Mkatumia mwanya mwingine kwa sababu mnajua kukopa kiholela mmerudi Uchina, mmeomba dola milioni 500 zingine. Mlikataa msaada wa Marekani wa MCC mkidai ya kwamba eti hamtaki pesa zenye masharti! Mchina alipowapa dola milioni 500 akawaambia sharti la kwanza lazima wakandarasi wa Kichina wote walipwe, ambao wanaidai Tanzania siyo chini ya dola milioni 365. Mmekataa masharti yapi na mmepokea yapi? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba tukubaliane kabisa ya kwamba, kwenye hili lazima muwe waangalifu kwa sababu kwanza mnakopa fedha nyingi sana kutoka source moja! Hatari hata kwa ustawi wa Taifa, hatari hata kwa usalama. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie suala la mizigo bandarini. Naomba nieleze kwa masikitiko kabisa ya kwamba bandari ya Dar es Salaam ina hali mbaya na inekoelekea sijui inakwenda kufa sina hakika, kwa sababu kwa mwezi wa kwanza na wa pili tu kwa takwimu, naomba nirejee, mizigo iliyokuwa inapita kwenye bandari ya Dar es Salaam kutoka Zambia imepungua kwa 42%, container kwa 28%, magari kwa 55%. Mizigo iliyokuwa inakwenda Congo imepungua kwa 9%, container 31%, magari 50%. Mizigo iliyokuwa inakwenda Burundi imepungua kwa 27%, mizigo iliyokuwa inakwenda Malawi imepungua kwa 35.6%, container kwa 11%, lakini mizigo ya Uganda imepungua kwa 77%. Nchi nyingine zikiwa na bandari ndiyo zinazojivunia kwa sababu, ni moja ya mlango wa uchumi... Imeisha? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.