Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Peter Joseph Serukamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia Mpango huu. Mpango huu ni mzuri, hivyo nina mambo machache sana.
La kwanza, ujenzi wa reli mpya ya kati kwa kiwango cha Kimataifa cha standard gauge. Namwomba Mheshimiwa Waziri aseme ni ujenzi wa reli ya kutoka Dar es Salaam mpaka Tabora mpaka Mwanza, kutoka Tabora mpaka Kigoma, kutoka Kaliua mpaka Mpanda mpaka Kalema, kutoka Uvinza kwenda Msongati na kutoka Isaka kwenda Keza. Haya mambo ya kutosema ndiyo baadaye tunabaki hatuna hata pa kumuuliza. Ningemwomba Mheshimiwa Waziri aje kwenye Mpango atakapouleta maana haya ni mapendekezo, aseme. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili ni suala la retention scheme. Mheshimiwa Waziri, nakuomba sana usiingie kwenye historia ya kuua taasisi za nchi hii. Viwanda vya nchi hii vilikufa miaka ile kwa sababu kila fedha inakusanywa inapelekwa Hazina, wanaomba kuagiza raw material mpaka fedha zitoke Hazina, by the time wanapewa pesa ndiyo viwanda vikaanza kufa. Leo mnakuja mnataka kuua Halmashauri, mnataka kuua Taasisi za Serikali! Naomba Wabunge mnikubalie tupinge habari ya kuondoa retention. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitasema, leo mnasema fedha zote ziende Central Bank. Nataka nimuulize Waziri wa Fedha, fedha zinazokusanywa na Pension Funds, wasipoziwekeza Pension Funds hazifi hizi? Pension Funds zinakusanya fedha mnapeleka Hazina, watazalishaje, watalipaje pension? Leo mnasema retention scheme za kwenye airport zote ziende Hazina, kitakachotokea mtawafukuza watendaji, kwa sababu ndege zitashindwa kutua, mtakuwa hamjapeleka OC kwa sababu hela mmekusanya, mmepeleka Hazina.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri zinakusanya fedha za own source, mnasema peleka Hazina, hizi Halmashauri zitakufa, mnasema leo own source zote za TANAPA, za nani ziende Hazina. Kitakachotokea, Mbuga za nchi hii zitaanza kufa mbuga moja baada ya nyingine. Mnataka Bunge hili tuingie kwenye historia ya kuua mbuga za nchi hii? Halafu kama hoja ni kuweka hela Hazina hawajaanza leo. Hebu tukumbushane ilikuwaje miaka ya nyuma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati BOT imeungua, ndiyo wakati hela ziliondoka Hazina, zikapelekwa NBC, alivyokuja Gavana yule Rashid akasema sasa sizitaki hizi fedha. Urasimu ulikuwa ni mkubwa sana. Nasema kama ni fedha za Serikali za Bajeti weka Hazina hakuna atakayekupinga, lakini fedha zinazozalishwa huku, mkisema zote ziende Hazina, mtaua taasisi moja baada ya nyingine. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, halafu, hatuwezi kuwa na contradiction, mnasema D by D, D by D gani sasa? Unless mniambie kwamba sasa hatuzitambui Halmashauri zote. Kwenye Vyuo vya Maendeleo, kwenye shule za sekondari watoto wanalipa pesa wanunue chakula, mnasema peleka pesa zote peleka Hazina, muda wa kununua chakula utakuwa wapi? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho Mheshimiwa Waziri, nchi hii inaongozwa kwa sheria. Ziko taasisi zimeletwa kwa sheria, mnatakaje kuleta mambo kwa decree, mnaamua tu bila kufuata sheria? Ningeomba Waziri wa Fedha, tuletee sheria zote zilizoanzisha taasisi hizi ambazo kwenye sheria kuna mambo ya retention, tuangalie ili tubadilishe sheria za nchi. Haiwezekani mnakaa na TR mnaandika barua, fedha zote zitapelekwa Hazina kesho Jumatatu. Hii ni nini? Mnapewa sekunde.
Mheshimiwa Mwenyekiti, yapo mashirika kufungua akaunti lazima muwaite Board Meeting leo ninyi mnawapa siku nne, wawe wamepeleka fedha BOT. Kuna haraka kweli? Nasema na nawaomba sana Wabunge, hili la Retenteion tulipinge, tunalipinga kwa sababu We have a cause, tunataka kuzuia watu kuua mashirika ya nchi hii na ni kwa sababu watu wa Hazina hamtaki kufikiri. Chenge one, imewapa vitu vya kukusanya mapato, hakuna hata kimoja mmekiandika humu. Bahari kuu iko wapi, kila siku mnatuambia habari ya bahari kuu, tutakwenda kufanya utaratibu, mpaka lini huo utaratibu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, shida ya pale Treasury watu hawataki kufikiri. Angalia vyanzo vya mapato ni vilevile toka nimeingia Bungeni havijawahi kubadilika. Naomba sana niseme tulikubaliana wakati tunaanzisha VAT kwamba VAT itapungua na ningeomba twende 16 wanavyokwenda Wakenya ili tuweze kushindana na Kenya, lakini tumekaa rigid, matokeo yake tunapambana. Nasema viwango vya kodi visiposhushwa hatuwezi kupata compliance, viwango vya kodi vya nchi hii vinatuma watu kukwepa kodi kwa sababu viwango ni vikubwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, watu wa TRA najua wametembea duniani kote kuangalia viwango vya kodi, wakienda duniani kuangalia viwango vya kodi wanaangalia nini? Ukienda Mauritius kodi ziko chini na wanakusanya zaidi yetu, wako mpaka fifteen percent hadi cooperate tax na wanakusanya zaidi, sisi tumekalia kupandisha rate na mnajua kwa nini tunapandisha rate, ni kwa sababu hatutaki kufikiri kutafuta tax base zingine. Tumeji-zero in kwenye tax base ile ile.
Mheshimiwa Mwenyekiti, narudia tena, suala la reli kwetu sisi ni kufa na kupona. Naomba niwaambie Waheshimiwa Wabunge, Walvis Bay wanajenga reli kwenda Congo, Nakara wanajenga reli kwenda Zambia, Wakenya wanakwenda Kigali. Reli zote zikiisha Tanzania hatuna cha kwetu. Haiwezekani Mungu ametuumba Tanzania imewekwa hapa geographically Mungu ana sababu na sisi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumezungukwa na nchi nane, lakini hatutaki kutumia hizo opportunity, tatizo ni nini? Halafu mtatuambia kujenga reli, tukope maana Waziri wa Fedha juzi anasema, hatuwezi kujenga reli hii ni fedha nyingi, nani kasema, fedha nyingi nani anazitoa, fedha ziko duniani tukazitafute….
MWENYEKITI: Mheshimiwa Serukamba, muda wako umekwisha.
MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. (Makofi)