Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nipo. Ahsante sana kwa kunipatia nafasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa naomba niwashukuru viongozi wangu wa CHADEMA kwa kuniona. Naomba nijikite kwenye vipengele viwili. Kipengele cha kwanza utawala bora na cha pili ni TAMISEMI.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikianza na utawala bora. Sisi kama Wabunge ni wawakilishi wa wananchi, tupo hapa kuwawakilisha wananchi. Kama wawakilishi wa wananchi tunapaswa wananchi wetu waone nini tunakifanya humu ndani, lakini hadi sasa hivi sielewi, kama Wabunge kwa nini tumejifungia humu ndani? Sielewi kwa nini tumejifungia humu ndani na tunaogopa nini? Niwaulize Chama cha Mapinduzi kwa nini mnaogopa kutuonesha kwenye luninga?
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili katika utawala bora; watendaji walioko Serikalini wana…..
TAARIFA...
MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, sipokei taarifa kwa sababu sijasoma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mkoa wangu wa Njombe watendaji hawa wanawanyanyasa sana wanawake wajasiriamali na nina ushahidi. Mfano mwaka jana Mkuu wa Wilaya ya Njombe ambaye sasa hivi kwa bahati mbaya ni marehemu, aliwakemea watu wa CHADEMA kwa sababu eti wamevaa mavazi ya CHADEMA wakiwa barabarani na aliwashtaki, hata kesi ilikuwa mahakamani. Kwa hiyo, hii inaonyesha ni namna gani Serikali inavyopendelea wana-CCM.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Katiba yetu, Ibara ya 20 inasema; “Kila mtu ana haki ya kuchagua chama anachokitaka.” Lakini sijaelewa kwa nini Serikali ya CCM inawatenga UKAWA. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine niende moja kwa moja kwenye suala la kilimo, nikiangalia bajeti...
MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Njombe wametengewa kiasi hicho kidogo, naomba unilinde Mwenyekiti muda wangu…
Mheshimiwa Mwenyekiti, upande wa bajeti ya kilimo, Njombe ni kati ya Mikoa ambayo inazalisha chakula kwa wingi, lakini ukiangalia bajeti iliyotengwa kwa ajili Mkoa wa Njombe ni fedha ndogo sana ukilinganisha na maeneo mengine ambyo pengine hata hayazalishi. Hivyo ninaomba Waziri anayehusika kuiongezea bajeti ya kilimo.
Suala lingine ni juu ya ukusanyaji wa mapato. Ukusanyaji wa mapato katika Mkoa wangu wa Njombe kwa kweli unatuchanganya kwa sababu fedha zinazokusanywa kwenye Halmshauri hazieleweki zinafanya kazi gani, wakati mwingine fedha hizo zinazokusanywa hazikusanywi inavyotakiwa. Kwa mfano, pale Njombe kuna magari mengi (mabasi) yanayotakiwa kulipa ushuru, lakini utakuta fedha zilizokusanywa ni kidogo hazilingani na yale mabasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni juu ya elimu. Walimu wengi hawana nyumba na wengine hawajapata mafao yao, lakini wameshastaafu. Hivyo naomba Waziri wa TAMISEMI kuwasaidia watu hawa wa Njombe angalau walimu waweze kupata haki zao hasa wale waliostaafu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ambalo kwa Mkoa wa Njombe kwa kweli ni suala nyeti ni kuhusu miundombinu ambayo kila siku ninaongea. Mkoa wa Njombe ni kati ya Mikoa ambayo inazalisha mazao kwa wingi, ni kati ya ile Mikoa mitano ambayo inazalisha, lakini barabara zake ni mbovu. Sasa hivi watu wanashindwa kusafirisha hata mazao yao kutoka kwenye maeneo ya pembezoni, wanashindwa kuleta mijini kwa sababu barabara zimeharibika sana.
Hivyo basi niombe tena kuifikiria Njombe kwa sababu nimeangalia hapa kwenye bajeti naona fedha kwa ajili ya miundombinu ya barabara ni fedha kidogo sana. In fact katika kupitia hii bajeti karibu mafungu yote ni kidogo. Kwa hivyo, ninaomba Waziri wa TAMISEMI aliangalie hilo kurekebisha hii bajeti angalau kuwaongezea bajeti ya kutosha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee juu ya suala la Mwenge. Mwenge kwa asilimia kubwa mimi kama shahidi unasaidia kueneza magojwa ya UKIMWI. Kwa sababu watu wanalala humo, wanalala wakati mwingine analala hata kwenye makuburi, wanatoa ile misalaba, hivyo naomba mwenge…
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.