Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo Kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa Bungeni kwenye Mkutano wa Kumi na Mkutano wa Kumi na Moja pamoja na Uchambuzi wa Taarifa za Utekelezaji wa Maazimio ya Bunge kuhusu Sheria Ndogo zilizowasilishwa Bungeni kwenye Mkutano wa Nane na Mkutano wa Tisa

Hon. Mohamed Omary Mchengerwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rufiji

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo Kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa Bungeni kwenye Mkutano wa Kumi na Mkutano wa Kumi na Moja pamoja na Uchambuzi wa Taarifa za Utekelezaji wa Maazimio ya Bunge kuhusu Sheria Ndogo zilizowasilishwa Bungeni kwenye Mkutano wa Nane na Mkutano wa Tisa

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nitumie fursa hii kuwashukuru sana Waheshimiwa Wajumbe wa Kamati kwa maoni na maelekezo ambayo wametupatia Wizara yetu ya TAMISEMI. Lazima nikiri kwamba lengo la Serikali yoyote duniani ni ustawi wa wananchi wake, na hii ndiyo sababu Wizara yetu ya TAMISEMI imedhamiria kuiweka Wizara mikononi mwa wananchi. Tunaposema tunaiweka Wizara mikononi mwa mwananchi, maana yake tunawapa wananchi mamlaka ya kutukagua na kuturekebisha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, msingi huu ni msingi ambao umepatikana katika Ibara ya 8 ya Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 9 na kuendelea mpaka Ibara ya 21, ambayo imewazungumzia wawakilishi wa wananchi katika maeneo yetu. Sauti ya wananchi inawakilishwa na Madiwani na Waheshimiwa Wabunge. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ndani ya Bunge hili, Kamati imepewa mamlaka ya kuwawakilisha Waheshimiwa Wabunge wengine. Kwa hiyo, sisi kama Wizara lazima nikiri kwamba tumepokea maelekezo ya Kamati. Inawezekana maelekezo mengi huko nyuma hayakufanyiwa kazi, lakini siyo wakati wangu. Naomba nilithibitishie Bunge lako tukufu kwamba kazi hii kubwa ambayo Kamati imefanya, sisi Wizara tutahakikisha kwamba yale maelekozo ambayo Kamati imetoa, kwetu sisi Wizara tunakwenda kuyafanyia kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tumekubaliana na wenzangu wote kwamba ule utendaji wa kimazoea sasa tunauacha (business as usual) tunauacha. Ili tuweze kuwawakilisha wananchi vyema kama ambavyo nimesema nchi ni ya wananchi, wawakilishi wa wananchi ndio hawa Waheshimiwa Wabunge, Waheshimiwa Madiwani kwa misingi ya Ibara ya 21 ya Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa hiyo, tutahakikisha sheria zetu, kanuni zetu zinaenda sambamba na tafsiri iliyotolewa katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwathibitishie Waheshimiwa Wabunge, tutahakikisha ile misingi na mifumo ya utungwaji wa kanuni ambayo pengine huko nyuma zilikuwa haziendi vizuri, tutakwenda kuziboresha ili kanuni zetu zote zinazotungwa ziwe ni zile ambazo zinaangalia maslahi ya wananchi wetu katika maeneo yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba niseme mbele ya Bunge lako tukufu kwamba mapendekezo ya Kamati ambayo yametolewa yana msingi wake, kwa sababu Kamati hii ndiyo Kamati ambayo inatoa sauti ya Wabunge wote ndani ya Bunge hili Tukufu. Kwa hiyo, tutakwenda kuyafanyia kazi mapendekezo yote ya Kamati na niwaombe Waheshimiwa Wabunge wajenge matumaini. Tutakwenda kuboresha mifumo yetu ya utungwaji wa kanuni zetu, na pia tutaboresha mifumo yetu ya utungwaji wa sheria zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimeshawaeleza watendaji katika Wizara hii, kila moja wetu kijipanga hasa kwa sababu ni lazima tulinde maslahi ya wananchi wetu. Ninaposema tunakwenda kulinda maslahi ya wananchi wetu, ni kwenda kutunga kanuni na sheria ambazo zinaangalia maslahi ya wananchi wetu katika maeneo yetu mbalilmbali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nilithibitishie Bunge lako tukufu kwamba ninaipongeza Kamati na ninaunga mkono hoja ambazo Kamati imetoa na sisi kama Wizara tutakwenda kujipanga vizuri, mimi na wasaidizi wangu, kuhakikisha kwamba yale mapendekezo ya Kamati yaliyotolewa kwa Wizara yetu hii ya TAMISEMI, ambayo ni Wizara ya wananchi, na kwa kuwa tayari nimeshatoa maelekezo kuirejesha Wizara hii kwa wananchi, tutakwenda kulinda maslahi ya wananchi kwa kuhakikisha kwamba kanuni zinazotungwa ni kanuni ambazo zinalenga kulinda na kutetea ustawi wa wananchi katika maeneo yetu yote nchini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hata katika misingi ya sheria, tutajikita katika kuhakikisha kwamba sheria zetu zinaendana na tafsiri ya Katiba kama ambavyo Katiba imefafanua.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, nakushukuru sana, naunga mkono hoja. (Makofi)