Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge Kuhusu Mapendekezo ya Kurejea Katiba ya Tume ya Usafiri wa Anga ya Afrika ya Mwaka 2009

Hon. Prof. Makame Mnyaa Mbarawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkoani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge Kuhusu Mapendekezo ya Kurejea Katiba ya Tume ya Usafiri wa Anga ya Afrika ya Mwaka 2009

WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kabla sijafanya hitimisho la hoja iliyoko mbele, naomba kufanya masahihisho kidogo tu. Wakati natoa hoja yangu nilisema Mkutano wa Kumi na Moja, lakini huu ni Mkutano wa Kumi na Mbili, naomba isomeke hivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote tena, napenda nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutujalia afya njema na kutuwezesha kukutana hapa kwenye Bunge letu Tukufu na kujadili hoja hii iliyo muhimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitumie fursa hii kukushukuru wewe binafsi, kwa jinsi ulivyoongoza majadiliano kwenye hoja hii ya Katiba ya Tume ya Usafiri wa Anga wa Afrika ya Mwaka 2009.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba pia kipekee nimshukuru Mwenyekiti wetu wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Mheshimiwa Selemani Moshi Kakoso pamoja na Waheshimiwa wote, Wajumbe wa Kamati ya Miundombinu kwa jinsi ambavyo walichangia hoja hii na jinsi ambavyo walichambua hoja hii kwanza kuanzia kwenye Kamati mpaka walipokuja hapa Mwenyekiti amechangia vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikiri kwamba hoja hii ni muhimu sana kwa maendeleo na ukuaji wa Sekta ya Anga hapa nchini. Pia, nawashukuru Waheshimiwa wote Wabunge waliochangia hoja hii, tumezichukua hoja zao na tunaenda kuzifanyia kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Hoja za Kamati ya Bunge ya Kudumu zilikuwa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ya kwanza ilikuwa ni kutoa fursa kwa lugha ya Kiswahili itangazwe. Pili, fursa za soko la ajira pamoja na za anga pia, wadau wengine washirikishwe. Yote haya tumeyachukua tunaenda kuyafanyia kazi, tutaboresha zaidi au tutaitangaza zaidi Lugha ya Kiswahili, pamoja tutatangaza zaidi soko la anga hapa Tanzania pamoja na kuwashirikisha wadau.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Dkt. Chamuriho yeye ana wasiwasi tu ambao ameonyesha kuhusu Mkataba wa Yamoussoukro. Ukweli wenyewe kama alivyosema Naibu Waziri, kwamba mkataba wa nchi na nchi unaongozwa na Bilateral Air Service Agreement. Kwa mfano, leo Kenya wamesaini Katiba hii, Rwanda wamesaini Katiba hii, lakini Rwanda yeye haiwezi kutoka ikaenda Nairobi ikachukua abiria kupeleka Mombasa, haiwezi. Kwa sababu inaongozwa baina ya Kenya na Rwanda ni Bi-Service Agreement au Bilateral Service Agreement baina ya Kenya na Rwanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi tunayo na nchi mbalimbali, tuna na Kenya, tuna na Rwanda na nchi nyingine mbalimbali, tunayo mikataba hiyo. Hiyo ndio inaongoza utaratibu wa kutoa abiria kutoka eneo moja kwenda la pili. Leo kwa mfano, KLM inafika Kilimanjaro lakini haiwezi kuchukua abiria wa ndani kutoka KIA kuwaleta Dar es Salaam. Kwa hiyo, tumepokea maoni ya Mheshimiwa Dkt. Chamuriho, tunayaheshimu na tunaenda kuyafanyia kazi, lakini nimhakikishie tu kwamba usaifiri wa anga nchini upo salama na Air Tanzania tutaendelea kuilinda ili iweze kufanya kazi iliyokusudiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya maelezo hayo mafupi, sasa naomba kutoa hoja. (Makofi)

WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, naafiki.